Mtaguso wa kwanza wa Laterano

![]() |
Sehemu ya mfululizo kuhusu |
Mitaguso mikuu ya Kanisa Katoliki |
---|
![]() |
Mtangulizi (50 hivi) |
Roma ya Kale (325–451) |
Mwanzoni mwa Karne za Kati (553–870) |
Mwishoni mwa Karne za Kati (1122–1517) |
Nyakati za uvumbuzi mwingi (1545–) |
Mtaguso wa kwanza wa Laterano unahesabiwa na Kanisa Katoliki mtaguso mkuu wa tisa katika historia yake, wa kwanza kufanyika Magharibi. Ulianza tarehe 18 Machi ukamalizika tarehe 11 Aprili 1123.
Mahali pake ni kwenye Kanisa kuu la Roma huko Laterano, mtaa wa Roma (Italia) alipokuwa anaishi askofu wake. Hukohuko baadaye ilifanyika mitaguso mingine minne ya Karne za Kati. Umuhimu wa kanisa hilo ulipungua hasa baada ya Papa kuhamia Vatikano.
Historia
[hariri | hariri chanzo]Mtaguso uliitishwa na Papa Callixtus II (1119-1124) mnamo Desemba 1122, mara baada ya Mapatano ya Worms, ya kwanza kufanyika kati ya Papa na Dola Takatifu la Kirumi, iliyofurahisha sana wanakanisa, hata mwaka huo ulitajwa kuwa mwanzo wa kipindi kipya.
Mapatano hayo yalikomesha desturi ya walei kuteua viongozi wa Kanisa na wa utawa, yakitenganisha shughuli za kiserikali na zile za kidini, na kukubali kwamba mamlaka ya kiroho inatokana na daraja takatifu.
Ili kuthibitisha mapatano hayo, Papa alialika Roma maaskofu wote wa Magharibi. Waliohudhuria kweli walikuwa zaidi ya 900, wakiwemo maaskofu zaidi ya 300 na maabati 600 hivi. Papa mwenyewe aliendesha vikao.
Hakuna hati za mtaguso, ila matunda yake. Tunachojua ni kwamba Mapatano hayo yalisomwa yakapitishwa rasmi, pamoja na kanuni 22 au 25, ambazo nyingi zilikuwa zimeshapitishwa zamani.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Medieval Sourcebook: First Lateran Council Ilihifadhiwa 14 Agosti 2014 kwenye Wayback Machine.: Kanuni za mtaguso na ufafanuzi wake.
- Mtaguso wa kwanza wa Laterano katika Catholic Encyclopedia
![]() |
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mtaguso wa kwanza wa Laterano kama historia yake, matokeo au athari zake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |