Maria Magdalena Postel

Maria Magdalena Postel, ambaye jina la kiraia kwa Kifaransa lilikuwa Julie Françoise-Catherine Postel (Barfleur, Ufaransa, 28 Novemba 1756 - Saint-Sauveur-le-Vicomte, 16 Julai 1846) alikuwa mwanamke ambaye mwaka 1807 alianzisha shirika la Masista wa Shule za Kikristo wa Huruma (Congrégation des sœurs des Écoles chrétiennes de la Miséricorde) kwa ajili ya malezi ya Kikristo ya wasichana fukara [1].
Alitangazwa na Papa Pius X kuwa mwenye heri mwaka 1908 akatangazwa na Papa Pius XI kuwa mtakatifu tarehe 24 Mei 1925.
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Mwaka 1774 huko Barfleur Julie Postel alifungua shule ya wasichana ambayo wakati wa mapinduzi ya Ufaransa ilitumika kwa shughuli za kidini za siri za Wakatoliki waliokataa masharti ya serikali yaliyo.
Baada ya dhuluma kwisha, aliendelea kufundisha na kufanya kazi nyingine za huruma.
Alipofikia umri wa miaka 51 aliweka nadhiri kwa jina la sista Maria Magdalena akaandaa uanzishaji wa shirika.
Miaka ya kwanza mafanikio yalikuwa madogo, lakini mwaka 1830 alifaulu kununua monasteri ya zamani huko St-Sauveur-le-Vicomte iwe makao makuu.
Shirika lilikubalika rasmi mwaka 1837 likabaki chini ya usimamizi wa mwanzilishi hadi mwaka wake wa mwisho.[3]
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/91039
- ↑ Martyrologium Romanum
- ↑ Donald Attwater. The Penguin Dictionary of Saints (Penguin Reference Books), 1965; pp. 237-38.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- Pierre de Crisenoy, Sainte Marie-Madeleine Postel, Paris, Bonne Presse, 1938
- Georges Grente, Une Sainte normande, Marie-Madeleine Postel, Paris, Bonne Presse, 1945
- Abbé François-Augustin Delamare, Vie édifiante de la très honorée supérieure Marie-Madeleine, née Julie Postel, réédition le Livre d'histoire, 2005; ISBN 2-8437-3726-5
- Wilhelm Hünermann Die Seilerstochter von Barfleur: Lebensbild der heiligen Maria-Magdalena Postel. Freiburg im Breisgau: Herder, 1956
| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
