Manaeni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Manaeni akiomba

Manaeni (au Menachem) alikuwa nabii na kiongozi mmojawapo wa Kanisa la kwanza huko Antiokia, jiji la Siria katika Dola la Roma (leo nchini Uturuki).[1]

Katika kutoa taarifa hiyo, Luka mwinjili (Mdo 13:1) anaeleza kwamba alikuwa ndugu wa kunyonya wa Herode Antipa, mtawala wa Galilaya na Perea katika karne ya 1. Hiyo iliweza kumaanisha udugu wa kambo[2] au urafiki wa kudumu tu.

Mwaka 39 Herode Antipa alisafiri kwenda Roma ili kujipendekeza kwa Kaisari Kaligula, kumbe alilazimishwa kubaki ugenini moja kwa moja (Yosefu Flavius, "Ant.", XVIII, vii, 2).

Wakati huohuo Kanisa la Antiokia lilianzishwa na Wakristo wenye asili ya Kiyahudi lakini wa lugha ya Kigiriki, waliotawanyika baada ya dhuluma iliyoanza kwa kifodini cha Stefano mjini Yerusalemu (Mdo 11:19-24). Inafikiriwa kwamba Manaeni alikuwa mmojawao.

Inawezekana alikuwa pia kati ya mashahidi waliompa Luka taarifa mbalimbali, hasa juu ya huyo Herode na ikulu yake (taz. Lk 1:2), na juu ya mwanzo wa Kanisa la Antiokia.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu[3].

Sikukuu yake huadhimishwa na Waorthodoksi tarehe 23 Mei[4] lakini na Wakatoliki tarehe 24 Mei[5]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1.  "St. Manahen". Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company. 1913.
  2. e.g. American Standard Version, Living Bible
  3. https://www.santiebeati.it/dettaglio/93010
  4. Ὁ Προφήτης Μανὴν. 23 Μαΐου. ΜΕΓΑΣ ΣΥΝΑΞΑΡΙΣΤΗΣ.
  5. Martyrologium Romanum May 24 Archived 12 Oktoba 2011 at the Wayback Machine.
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Manaeni kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.