Ufufuko : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
Legobot (majadiliano | michango)
d Bot: Migrating 41 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q188681 (translate me)
No edit summary
Mstari 1: Mstari 1:
[[File:Kern Vision des Ezechiel.jpg| thumb |Mchoro wa Leonhard Kern, ''Njozi ya Ezekieli'', kwenye Schwäbisch Hall.]]
[[File:Kern Vision des Ezechiel.jpg| thumb |Mchoro wa Leonhard Kern, ''Njozi ya Ezekieli'', kwenye Schwäbisch Hall.]]
'''Ufufuko''' ni hali ya [[mwili]] kurudi kuishi baada ya kufa, kwa mfano wa kuamka kutoka usingizini.
'''Ufufuko''' (kutoka [[kitenzi]] "kufufua") ni hali ya [[mwili]] kurudi kuishi baada ya [[kufa]], kwa mfano wa kuamka kutoka [[usingizi|usingizini]].


[[Dini]] mbalimbali zinasadiki uwezekano wake, ingawa kwa misingi na mitazamo tofauti.
[[Dini]] mbalimbali zinasadiki uwezekano wake, ingawa kwa misingi na mitazamo tofauti.

Kuna [[visasili]] kuhusu [[miungu]] kufa na kufufuka mara kwa mara, kwa mfano wa [[uhai]] wa [[uasilia]] katika mzunguko wa [[majira]], hasa katika [[majira ya kuchipua]] baada ya [[majira ya baridi]].

Tofauti na [[hadithi]] hizo, [[Biblia]] inafundisha [[uwezo]] wa [[Mungu]] juu ya [[kifo]] cha [[binadamu]], kwamba kupitia [[manabii]] kama [[Elia]] na [[Elisha]], yeye aliwarudishia uhai watu waliokufa tangu muda mfupi.

Baada ya [[nabii Ezekieli]] kupata [[njozi]] kuhusu ufufuko wa [[mifupa]] mikavu iliyozagaa bondeni, [[Wayahudi]] walizidi kukubali kwamba Mungu atafufua wafu wote.

[[Injili]] zinasimulia jinsi [[Yesu Kristo]] alivyofufua [[vijana]] watatu kwa nyakati tofauti: [[binti]] [[Yairo]], [[mvulana]] wa [[Nain]] na [[Lazaro wa Bethania]].

Lakini jambo kuu la [[vitabu]] hivyo ni kwamba mwenyewe aliweza kufufuka [[siku]] ya [[tatu]] baada ya [[Kifo cha Yesu|kufa]] [[Msalaba wa Yesu|msalabani]], tena si kwa kurudia [[maisha]] ya [[duniani]], bali kwa kuingia [[uzima wa milele]] akiwa na mwili mtukufu.

[[Yesu]] alitabiri kwamba atarudi kutoka huko siku ya mwisho ili afufue wafu wote na [[Hukumu ya mwisho|kuwahukumu]].

[[Uislamu]] pia unafundisha kwamba mwishoni kutakuwa na ufufuo wa wafu wote (Yawm al-Qiyāmah, kwa [[Kiarabu]]: يوم القيامة‎‎). Siku hiyo imepangwa na Mungu lakini haijafunuliwa kwa binadamu.


==Tazama pia==
==Tazama pia==
Mstari 15: Mstari 29:


[[Category:Dini]]
[[Category:Dini]]
[[Jamii:Uyahudi]]
[[Category:Ukristo]]
[[Category:Ukristo]]
[[Jamii:Uislamu]]

Pitio la 14:09, 3 Oktoba 2017

Mchoro wa Leonhard Kern, Njozi ya Ezekieli, kwenye Schwäbisch Hall.

Ufufuko (kutoka kitenzi "kufufua") ni hali ya mwili kurudi kuishi baada ya kufa, kwa mfano wa kuamka kutoka usingizini.

Dini mbalimbali zinasadiki uwezekano wake, ingawa kwa misingi na mitazamo tofauti.

Kuna visasili kuhusu miungu kufa na kufufuka mara kwa mara, kwa mfano wa uhai wa uasilia katika mzunguko wa majira, hasa katika majira ya kuchipua baada ya majira ya baridi.

Tofauti na hadithi hizo, Biblia inafundisha uwezo wa Mungu juu ya kifo cha binadamu, kwamba kupitia manabii kama Elia na Elisha, yeye aliwarudishia uhai watu waliokufa tangu muda mfupi.

Baada ya nabii Ezekieli kupata njozi kuhusu ufufuko wa mifupa mikavu iliyozagaa bondeni, Wayahudi walizidi kukubali kwamba Mungu atafufua wafu wote.

Injili zinasimulia jinsi Yesu Kristo alivyofufua vijana watatu kwa nyakati tofauti: binti Yairo, mvulana wa Nain na Lazaro wa Bethania.

Lakini jambo kuu la vitabu hivyo ni kwamba mwenyewe aliweza kufufuka siku ya tatu baada ya kufa msalabani, tena si kwa kurudia maisha ya duniani, bali kwa kuingia uzima wa milele akiwa na mwili mtukufu.

Yesu alitabiri kwamba atarudi kutoka huko siku ya mwisho ili afufue wafu wote na kuwahukumu.

Uislamu pia unafundisha kwamba mwishoni kutakuwa na ufufuo wa wafu wote (Yawm al-Qiyāmah, kwa Kiarabu: يوم القيامة‎‎). Siku hiyo imepangwa na Mungu lakini haijafunuliwa kwa binadamu.

Tazama pia

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.