Majadiliano ya mtumiaji:Riccardo Riccioni

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Fransisko wa Asizi[hariri chanzo]

Riccardo, salam. Nd. Riccardo, ile makala ya Fransisko wa Asizi, umeandika safi sana na inaeleweka. Lakini je vipi kuhusu mwaka aliozaliwa huyu bwana unaujua? Natumai utakuwa umeitafsiri kutoka wiki zingine ama sivyo? Natumai ndivyo!! Basi kama utaweza kuandika mwanzo kabisa mwaka aliozaliwa itakuwa bora zaidi. Labada nikupe mfano mdogo: Fransisko wa Asizi (tarehe na mwaka aliozaliwa) alikuwa mtakatifu kutoka nchini Italia. Asizi alizaliwa katika mkoa wa Umbria, wilaya ya Perugia, Italia.... Kisha unaweka kama ndugu na mambo mengine!! Haya basi kama hujaelewa labda umwulize Kipala atakupa habari zaidi!! Kingine usisahau kuweka InterWiki katika makala yako kama ipo katika wiki zingine-[[it:Fransisko of Asizi]] (sijui kwa lugha ya Kitaliano wanahitaje) lakini inategemea na lugha vyovyote vile inaswihi. Kingine kuweka vichwa katika makala, hili nenda kaangalie makala yako utaona nimefanya vipi mpaka kimekuja kichwa cha habari-Fransisko wa Asizi. Sina mengi na nakutakia kheri ya mwaka mpya na furaha tele moyoni!!--Mwanaharakati 05:08, 7 Januari 2008 (UTC)[jibu]

Kuna kitu nimesahau kukueleza. Kuweka jamii au category katika makala, mfano: [[Category:Watakatifu wa Italia]] au [[Category:Watakatifu]] na nyingine ya mwaka aliozaliwa -unaweka mabano kama hayo kisha unaadika (Waliozaliwa 19 na...) kama kafa unaandika Waliofariki (mwaka aliokufa). Natumai utakuwa umeelewa!!--Mwanaharakati 05:20, 7 Januari 2008 (UTC)[jibu]

Ushauri[hariri chanzo]

Salam. Ukiwa bado humchanga katika wiki hii, ni vyema ku-login kabla ya kuumba makala!!! Nimeona baadhi ya makala umeandika bila ku-login, kisha nikafikiri ni Kipala aliyefanya hiyo hivyo, kwani yeye ndiye huwa na kawaida hiyo!! Basi endelea na kazi yako Ndugu, wako katika ujenzi wa Wikipedia,--"Mwanaharakati" (talk) 12:19, 28 Februari 2008 (UTC)[jibu]

Mpangilio wa makala[hariri chanzo]

Salaam! Kuna mapendekezo kuhusiana na muundo wa makala na vichwa vyake. Naomba angalia hapa kwa maelezo zaidi....--"Mwanaharakati" (talk) 12:43, 11 Machi 2008 (UTC)[jibu]

Salaam! Tukiwa tunaendelea na mada yetu ya vichwa vya habari katika makala, labda nikueleze kingine nimekiona! Ni vyema wakati wa kutaka kumwachia mtu ujumbe katika kurasa ya majadiliano, uwe unaanzia chini na sio juu. Ukifanya hivyo inakuwa rahisi mtu kufahamu ujumbe upo wapi. Vinginevyo uangalia mabadiliko ya mwisho ndiyo utajua ujumbe upo wapi. Pendekezo: Ni vyema uwe unaweka (au kuacha ujumbe wako kuanzia chini). Vichwa vya habari: Labda nikuonyeshe namna ya kuweka vichwa vya habari

==Hapa unaweka maelezo husika na kichwa cha habari hiki==

Hapa chini yake unaaza kuelezea vile habari kama kilivyo kichwa chake cha habari.

Naomba angalia makala hii :Maangamizi makuu dhidi ya Wayahudi wa Ulaya na vichwa vyake vya habari, labda utapata mwelekeo mzuri zaidi. Ukiwa unaona bado huja elewa basi nijulishe au mwulize mkabidhi yoyote atakupa maelekezo zaidi! Kila lakheri....--Mwanaharakati (majadiliano) 04:18, 25 Machi 2008 (UTC)[jibu]

Viungo vya nje[hariri chanzo]

Salam. Ndugu Riccardo, hamna uwezekano wa kupata viungo vya nje katika makala unazo-changia? Maana naona makala nyingi umeandika bila ya viungo vya nje, wakati ukiziangalia katika Wikipedia zingine unazikuta wamewekea viungo vya nje. Je vipi utafanya ili uweze kuweka hata viungo vya nje katika baadhi ya makala utakazo changia-zenye kuhitaji viungo vya nje?--Mwanaharakati (majadiliano) 11:57, 27 Machi 2008 (UTC)[jibu]

Salaamu Ricardo,nafurahi sana kuona kazi yako. Nina neno kuhusu ualimu naomba utazame ukurasa wa majadiliano huko. ̰-Kipala (majadiliano) 19:12, 27 Machi 2008 (UTC)[jibu]

Hongera ya makala 7,000[hariri chanzo]

Salam nyingi zikufikie Nd. Riccardo! Ninapenda kukupa hongera kwa kusukuma wiki yetu juu ya kiwango cha makala 7,000! Nafurahia kuona tumefikia makala elfu saba. Naona kama naota kufikia kiwango hicho, ingawaje si nyingi hivyo lakini tumefika!. Basi tuendelee kushauriana na kuvumiliana!--Mwanaharakati (majadiliano) 07:32, 21 Aprili 2008 (UTC)[jibu]

Fransisko[hariri chanzo]

Ricardo, niliandika hapa kitu juu ya umbo la makala lakini nimeifuta tena kwa sababu sijaona ya kwamba umeshabadilisha mwenyewe. --Kipala (majadiliano) 11:19, 14 Mei 2008 (UTC)[jibu]

Vitabu vya Biblia[hariri chanzo]

Riccardo salaam, nimeona umechapa kazi kan bisa kuhusu vitabu vya Biblia. Ombi langu ni: tujaribu kushikamana pamoja. Labda umeona ya kwamba hata Oliver na mimi tumeshaanza makala kadhaa juu ya vitabu vya Biblia lakini sijandelea kwa muda mrefu. Hapa naona kuna mamabo mawili yanaofaa tukumbuke: tupatane juu ya majina na jamii.

  • Kwanza tukiwa na makala nyingi napendekeza tutumie jamii za "Vitabu vya Agano la Kalre" na "Vitabu yva Agano Jipya" zote mbili chini ya "Category:Biblia". Menginevyo jamii zitajaa mno tukiweka kila kitu chini ya Biblia. Vile vile misahafu naona tutumie hii wka ngaziy a juu maana yake tukitaja vitabu vya dini mbalimbali si sehemu za kila kitabu cha kila dini (kwa mfano upande wa Uhindu tunapata nyingi mno, kama vile upande wa Ukristo).
  • Pili naomba ukiongeza kumbuka makala za

kwa sababu hapa kuna orodha na tukiunda makala kwa jina tofauti orodha hizi si msaada tena. Au tunafanya kazi mara mbili, linganisha Kumbukumbu la Sheria (Biblia) na Kumbukumbu la Sheria. Kumbe makala imeshakupatikana tayari. Basi sasa tuunganishe. Halafu ona jinsi nilivyofanya kwa Ruth: wewe uliandika Kitabu cha Ruth halafu nikaweka kiungo cha #REDIRECT kutoka orodha inapoandikwa kw< umbo la "Ruthu". Unaonaje? --Kipala (majadiliano) 14:43, 2 Juni 2008 (UTC)[jibu]

Salaaam! Namna ya kuelekeza ukurasa mmoja kuelekeza kwingine ni:
  • #REDIRECT [[andika ukurasa unaotaka ku-redirect hapa]].
Mengineyo, waone wataalamu wa "Dini", yaani Kipala! Ushauri: Naona mara nyingi ukiandika

ujumbe, huwa hakuna jina lako linalotokea katika ukurasa wa majadiliano wa mtu uliyemwachia ujumbe. Fanya hivi: --~~~~ kisha yenyewe itaandika jina lako, muda, tarehe n.k. Kazi njema na kila lakheri! Wako katika ujenzi wa Wikipedoia hii ya Kiswahili,--Mwanaharakati (majadiliano) 10:56, 3 Juni 2008 (UTC)[jibu]

Salamu!!!!! Baba Riccardo, napenda kujua kwa nini Bibilia nyingine zina vitabu 72 na nyingine zina vitabu 66? Pole na Kazi na Mungu akubariki.--TELESPHORY (majadiliano) 15:39, 27 Machi 2015 (UTC)[jibu]
Ndugu Asante sana.--TELESPHORY (majadiliano) 16:16, 27 Machi 2015 (UTC)[jibu]

Kutia sahihi[hariri chanzo]

Salam, Riccardo. Kuna kitu nimeona wakati wa kumaliza kuandika, jina lako linatoka bila kiungo. Hapa naona mambo mawili: Huenda akawa umeilemaza ile sehemu ya kuweka automatic link(angalia "mapendekezo yangu - raw signature"). Pia inawezekana ukawa unakosea namna ya kujisajilisha ili uweze kupatikana katika viungo hivi vya wiki. Angalia mfano huu tena kwa njia ya picha kisha uwe unafanya hivyo:

Faili:Kutia Saini.JPG
Fuata hizi alama kama zilivyo.

Samahani lakini kama nitakuwa na kukera katika kukumbushia namna ya kijisajili. Kazi njema na natumai utakuwa umeelewa! Endapo ukiwa bado, basi nijulishe...--Mwanaharakati (majadiliano) 13:07, 12 Juni 2008 (UTC)[jibu]

Salaaam! Riccardo, nimeona makala nyingi ukiwa unaandika vichwa vya habari kwa "herufi kubwa". Kwani haiwezekani kuandika herufi ndogo?? Unaombwa ufuate format ya wikipedia jinsi inavyokwenda! Usijisikie vibaya pale unapoelezwa kwani tupo katika kuboresha makala zetu! Hata mimi nilikuwa nafanya kama unavyofanya, lakini Kipala akanieleza namna ya kufanya vyema!!! Basi tushirikiane katika kazi ili tuwe wabora zaidi. Mengineyo: Ujumbe wa juu natumai umeuona, na kama umeona naomba nifute ile picha!--Mwanaharakati (majadiliano) 10:06, 13 Juni 2008 (UTC)[jibu]
Umefaulu. Ila usiandike jina lako, yenyewe itaandika jina lako na muda uliacha ujumbe ule. Hongera na kazi na tuendelee kushauriana! Wako katika ujenzi wa Wikipedia hii,--Mwanaharakati (majadiliano) 10:30, 13 Juni 2008 (UTC)[jibu]

Masharti ya makala[hariri chanzo]

Salaam Riccardo umefanya kazi kubwa ya kutunga makala mengi juu ya vichwa vyenye maana. Nashukuru. Lakini naona tatizo juu ya makala kadhaa kulinganana na masharti ya kamusi elezo. Kwa upande mmoja makala kuhusu maazimio ya mtaguso wa pili wa Vatikani hayafuati muundo wa makala. Maana yake mwanmzoni hazielezi waziwazi neno hili ni nini bali zinaanza na maelezo juu ya nia au mawazo ya Mtaguso. Hii haisaidii kueleweka vema. Halafu kuna jambo la pili nimeona mara nyingi namna ya mahubiri inayochanganywa na habari. Hii si mtindo wa kamusi elezo. Labda kama ukiandika kwa ajili ya homepage ya kanisa lako ingekuwa sawa. Lakini hapa tunahitaji maelezo yaliyo wazi kwa mtu yeyote. Kama Waislamu, Wakristo wa madhehebu mengine na watu wanaokanusha dini wanafanya hivihivi wikipedia yetu haieleweki tena. Naona haja kuleta masahihisho hapa. Ningeomba usinedelee kuandika makala kwa muundo huohuo bali tujitahidi pamoja kuleta mpanglio unaofaa. Napenda kurudia ya kwamba naona makala yote yanahusu mada muhimu lakini hatuna budi kusaidiana kutunza kiwango cha ubora fulani.--Kipala (majadiliano) 17:09, 15 Juni 2008 (UTC)[jibu]

Nimesahihisha kidogo mwanzo wa makala kuhusu "Dei Verbum". Pamoja na muundo niliona mafundisho au mahubiri ya kidhehebu. Ilikuwa vema ya kwamba ulinikumbusha juzi ya kwamba haikuwa sahihi kuonyesha mafundisho ya Kiprotestant juu ya idadi ya vitabu vya Agano la Kale. Nimekubali kabisa. Vivyo hivyo hakuna mahali hapa kuingiza mafundisho ya kidhehebu juu ya madhehebu mengine.
Mfano: Si kweli ya kwamba viongozi Waprotestanti walikataa ualimu wa kanisa; kinyume chake ualimu huu unasisitizwa sana! Tofauti ilikuwa ya kwamba wakati ule Waprotestanti hawakukubali Kanisa Katoliki kuwa kanisa kweli. Sasa tuna kazi ya kueleza mawazo haya katika makala juu ya historia ya kanisa au historia ya mafundisho ya kidini na hapo ni sawa. Lakini haifai kurudia matamko ya upinzani wa kidhehebu ndani ya makala kama hii, isipokuwa kama ni kweli sehemu ya kichwa fulani. Lakini inapaswa kuelezwa kama maoni fulani si kama habari halisi. Tuhurumie wasomaji wetu wanaotoka katika mazingira mbalimbali. Naomba tuelewane hapa na kusaidiana. --Kipala (majadiliano) 17:09, 15 Juni 2008 (UTC)[jibu]

Agano la Kale[hariri chanzo]

Ricccardo, asante kwa kunikumbusha. Samahani lakini sina uhakika unalenga nini yaani makala gani. Pale nilipoangalia nakuta vitabu vipo bila shaka unamaanisha sehemu nyingine ambako sioni. Naomba fanya hivi: weka kiungo (link) pale unapoandika kwenye ukurasa wangu ili nifike palepale. Mfano: Agano la Kale kuna vitabu vyote unavyotaja. Je wewe unalemha nini hasa? (halafu: Kuanzia kesho kutwa sitakuwepo kwa wiki 4 - naomba uvumilivu wako). --Kipala (majadiliano) 22:30, 16 Julai 2008 (UTC)[jibu]

Nimeelewa. Ilikuwa Template:Biblia_AK. Nimesahihisha. Halafu ilikuwa nini juu ya kulinganisha "Biblia ya Kiebrania" na "Agano la Kale"? --Kipala (majadiliano) 07:42, 17 Julai 2008 (UTC)[jibu]
Nimejibu ujumbe wako hapa!--Mwanaharakati (majadiliano) 15:10, 25 Agosti 2008 (UTC)[jibu]

Hi Ricardo Riccioni[hariri chanzo]

Hi! How are you? Could you please help me add a couple of sentences to the Kiswahili version of this interesting article?

Thanks so much! -Ivana Icana (majadiliano) 22:30, 6 Septemba 2008 (UTC)[jibu]

Could you please send me the artical Sen2006 (majadiliano) 10:38, 15 Oktoba 2018 (UTC)[jibu]

yes, i can. give me your your sentences Nestory kamal (majadiliano) 13:25, 11 Desemba 2021 (UTC)[jibu]

Riccardo, salam. Eti, umefikia wakati wa wewe kujiwekea viwango vya lugha uzifahamuzo katika ukurasa wako wa mtumiaji! Hapa kuna orodha chache ya mifano hai yenye kuonyesha lugha unazozijua. Angalia hizi:

Haya, katika kila kodi ya lugha, kwa mfano: sw-2 au 3, ni kiwango cha lugha unachokifahamu. Ikiwa en-2, 3, 4, ni namna ya kutaja vyema uwezo wa ujua wako wa lugha! Ukiona unajua zaidi ya namba 1,2,3 basi ongeza hadi nne katika kila kodi ya lugha, halafu ukimaliza kopi hayo mabano yote kisha nenda ka-paste katika ukurasa wako wa mtumiaji! Chukua hizi:

{{Babel|it|sw-3|en-3|es-3|fr-2|la-1}}

Karibu sana!--Mwanaharakati (Longa) 05:54, 13 Oktoba 2008 (UTC)[jibu]

Tayari nsihaongeza msingi wa lugha "A" katika Kihispania! Ni kama uonavyo hapo juu. Natumai kwa hili tushamalizana, kwa maelezo mengine zaidi, tafadhali uliza tu ukijisikia wataka kuuliza! Kila la kheri.--Mwanaharakati (Longa) 13:08, 1 Novemba 2008 (UTC)[jibu]

Riccardo Riccioni, salam. Namna ya kuweka picha ni rahisi sana ndugu yangu! Hebu fuata taratibu hizi kisha tuone kama tutafaulu katika kuelekezana huku. Andika:

[[Image:Jina la picha.jpg, .png, .svg, .gif n.k.|thumb|hapa weka kulia au kushoto (kwa Kiingereza)|ukubwa wa picha=250px n.k.|Maelezo ya picha, kisha]]

Kingine: Ukitaka kutumia formula hiyo, tafadhali usi kopi na hayo maandishi yaliyoandikwa. Chukua maelezo matupu bila ya nowiki! Haya, tazama picha jinsi inavyokuja kwa hapa: [[Image:Flag of Italy.png|thumb|left|15px|Bendera ya Italia]]. Ukiona bado hujaelewa, basi nijulishe nitakuelekeza zaidi!--Mwanaharakati (Longa) 13:21, 10 Novemba 2008 (UTC)[jibu]

Ndugu, sijaelewa. Pole! Kwanza sijui nowiki ni nini. Pili sijui picha niichukue wapi. Tatu nijueje ukubwa. Nilichoelewa ni kulia na kushoto... Pamoja na hayo, naona unapenda kufahamu niko wapi: si mbali na wewe, naishi Morogoro, hivyo itakuwa rahisi kukutana siku yoyote... Nimetekeleza agizo lako kuhusu Holy See. Natumaini inatosha. Kama ningeweza, ningeweka picha nzuri iliyopo mwanzoni mwa makala hiyo kwa Kiitalia! Pia katika user page yangu ya Kiingereza nimepandisha maksi zangu za Kiswahili kwa kuandika 4. Mbona mimi ni Mtanzania? Ila nimeona template hiyo haipo katika Kiitalia na Kiswahili. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 23:19, 15 Novemba 2008 (UTC)[jibu]
Duh! Ebwana eeeh! Basi mie sikujua kamama wewe ni Mtanzania. Lakini mbona una jina la Kiitalia (hata lugha yako ya kwanza ni Kiitalia!). Basi naona unge badilisha ile sehemu ya Kiswahi uweke (sw tupu bila namba!) Maana wewe ni Mswahili? Aaah, nahisi umekaa Tanzania mda mrefu, kiasi hata ujue Kiswahili kama Mzawa! Haya, basi eti picha ujuaelewa? Naona unge fungua ile picha na uitazame kama inatoka Wikimedia Commons (Commons ni mradi unaopakia picha kwa ajili ya Wikipedia zote au hata mieadi yote ya Wiki!). Basi tazama hii jinsi nilivyoongeza picha halafu muda mwingine ufanye kama hivyo. Pale utaona maandishi ya kijani (hayo ndiyo niliongeza mimi!). Ukiona bado hujaelewa, basi niulize tena kisha nitakueleza vyema! Na kuhusu mie, nina kaa huku kwetu shamba Kiwalani! Bwana akubariki,--Mwanaharakati (Longa) 12:19, 17 Novemba 2008 (UTC)[jibu]

Ombi la la tafsiri ya makala[hariri chanzo]

Salam nyingi zikufikie Nd. Riccardo Riccioni popote ulipo! Naomba kama utapata muda wa kuweza kutafsiri makala ya Holy See kutoka lugha ya Kiingereza au Kitaliano kama utapenda! Nataka kujua kuhusiana na hiyo Holy See, yaani uandike makala ya Holy See katika Wikipedia hii, ikiwezekana kwa Kiswahili itakuwa bora zaidi ama unaonaje?--Mwanaharakati (Longa) 13:21, 10 Novemba 2008 (UTC)[jibu]

Mambo mbalimbali[hariri chanzo]

Ndugu Riccardo, salaam! Nakushukuru kwa jumbe zako kadhaa za siku zilizopita, na sina budi kukuomba radhi kwa kimya yangu. Upande wa Carl Hinton, nitaendelea kuangalia sehemu ambazo amenakilisha tu kutoka katika "Biblia Inasema". Nimesafiri bila nakala yangu ya kitabu hicho kwa hiyo itanichukua muda kadhaa kabla sijaweza kuendelea na kazi hii ya ufutaji tena. Upande wa kichwa cha makala mbalimbali, mimi sioni shida, hasa kwa vile makala za zamani zitarejea zile za kisasa. Ila kuhusu "vita" nakubaliana na Ndugu Muddyb kwamba neno hili liendelee katika ngeli ya nomino ya 9 (yaani kihusishi chake kiwe "ya", siyo "vya"). Nyakati hubadilika. Kwa vyovyote turejee moja kwa nyingine. Basi, nakushukuru kwa kazi yako inayonifurahisha sana (mbona umehangaika ingewezekana kunichukiza? Haikufanya hivyo hata kidogo!). Na kazi njema! Baba Tabita (majadiliano) 14:27, 10 Novemba 2008 (UTC)[jibu]

Mtaguso[hariri chanzo]

Ndugu Riccardo, salaam. Naomba uangalie maoni kwenye ukurasa wa majadiliano ya Talk:Mtaguso Mkuu na pia makala ya Mitaguso_ya_kiekumene. Ningefurahi tukiweza kushirikiana katika jambo hili. --Kipala (majadiliano) 08:51, 18 Novemba 2008 (UTC)[jibu]

Hongera ya makala 8,000[hariri chanzo]

Salam nyingi zikufikie Nd. Riccardo! Ninapenda kukupa hongera kwa kusukuma wiki yetu juu ya kiwango cha makala 8,000! Nafurahia kuona tumefikia makala elfu nane. Nikikumbuka vile ulivochangia kwa hali na mali ili walau nasisi Waswahili tufikie elfu kadhaa, Naona sasa tumesogea! Shukrani za dhati zikufikie na tuendelee kushauriana na kuvumiliana--Mwanaharakati (Longa) 14:31, 19 Desemba 2008 (UTC)[jibu]

Badiliko la baadhi ya viungo![hariri chanzo]

Riccardo, salam! Kuna mabadiliko katika baadhi ya viungo vyetu! Sasa hivi kuna baadhi ya viungo vyetu vinatumika kwa Kiswahili. Kwa mfano CATEGORY hii sasa hivi ipo kama JAMII au picha, zamani ilikuwa Image:jina la picha. hiyo na hiyo. Lakini sasa ni Picha: halafu jina.... Ila zote zinafanya kazi, yaani kwa Kiswahili na Kiingereza! Lakini bora zaidi tukitumia kwa lugha yetu, au wewe unaonaje?--Mwanaharakati (Longa) 09:04, 24 Desemba 2008 (UTC)[jibu]

Mpendwa, nafurahi kuona maendeleo hayo ya lugha yetu. Tusonge mbele bila ya kugeuka nyuma! Ila sehemu nyingine kuna makosa: kwa mfano ukarasa badala ya ukurasa. Naomba nyinyi wataalamu mrekebishe. Kuhusu picha nimefaulu kuziingiza kwa njia tofauti na ile uliyonielekeza, yaani nazikopi kutoka lugha nyingine, ila mara mojamoja inashindikana. Mah! Hatumalizi kujifunza... Kuhusu uraia wangu, ni kama ulivyoelewa: nilizaliwa Italia, lakini nipo Tanzania tangu mwaka 1984. Nimekuwa raia tangu mwaka 1997. Asante. --196.45.46.171 06:44, 25 Desemba 2008 (UTC)[jibu]
Sawa, lakini hujaonyesha uo ukurasa wenye jina la "UKARASA". Ni bora kuonyesha kiungo kile ambacho umeokiona kinamakosa! Ahsante--Mwanaharakati (Longa) 05:42, 27 Desemba 2008 (UTC)[jibu]
Kwa mfano hapa pembeni na hapa chini katika Majadiliano ya mtumiaji. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 16:04, 29 Desemba 2008 (UTC)[jibu]

Galileo[hariri chanzo]

Hongera na asante kwa masahihisho ya maana! Nakiri nina udhaifu wa kupitia tena hasa nikiandika usiku manane wakati mwingine sioni makosa (tahajia, muundo wa sentensi). Basi tuendelee kusaidiana. Kitu kidogo: nashauri usitumie "jamii" badala ya "category". Najua inatakiwa kuwa sawa lakini bado kuna mdudu ndani yake --Kipala (majadiliano) 22:11, 29 Desemba 2008 (UTC)[jibu]

Ndugu,kweli nimeona unafanya kazi kubwa usiku, na si mara mojamoja kama mimi... Hongera na heri kwa mwaka mpya! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 22:33, 29 Desemba 2008 (UTC)[jibu]
Ni vyema kutoa sababu zinazopelekea shida ya JAMII au CATEGORY. Kuna tatizo lolote lililotokea au kutofautisha, kuleta tabu, au kutoonekana kwa makala pindi utakapoweka kiungo cha JAMII badala ya CATEGORY? Naomba nifahamishwe ili niende kuwaeleza wale Madevoloper wa MediaWiki haraka iwezekanavyo--Mwanaharakati (Longa) 05:49, 30 Desemba 2008 (UTC)[jibu]
Mimi sijaona tatizo lolote. Sasa mmeniweka njia panda: nionekane mkaidi kwa Kipala au kwa Muddy Blast? --196.45.46.171 13:34, 31 Desemba 2008 (UTC)[jibu]

Ndugu Riccardo. Hongera kwa kazi njema! Miezi miwili iliyopita, ndugu wetu Kipala aliuliza kuhusu hatimiliki ya makala ya Historia ya Wokovu. Nadhani ni wewe uliyeandika makala hiyo kwa sehemu kubwa kabisa. Ikiwa umenakilisha kutoka kitabu fulani na kuvunja hatimiliki, naomba urekebishe na kufupisha makala. Hata hivyo imekuwa ndefu mno kwa ajili ya kamusi elezo. Tukazane kusaidiana na kazi njema. Umesalimiwa na Baba Tabita (majadiliano) 16:22, 23 Januari 2009 (UTC)[jibu]

Ndugu, usiwe na wasiwasi: mwandishi wa makala hiyo ni mimi mwenyewe tu. Ni kweli kwamba ni ndefu, lakini historia ya binadamu ni ndefu zaidi... ni vigumu kusimulia miaka elfu kwa nusu saa! --196.45.46.171 06:41, 25 Januari 2009 (UTC)[jibu]

Hongera ya makala 9,000[hariri chanzo]

Riccardo, salam. Ni siku 43 nyuma, yaani, 19 Desemba 2008 hadi tar. 2 Februari 2009 - 9,000. Leo tuna makala 9,000. Inazidi kuifanya Wikipedia yetu kuwa vilevile ya pili kama jinsi ilivyozoeleka! Sina maneno mengi, ila ni kukutakia furaha ya kufika hapa tulipo! Pia, maisha mema na kazi kwa ujumla. Kila la kheri. --Mwanaharakati (Longa) 16:25, 2 Februari 2009 (UTC)[jibu]

Mpendwa, bado kidogo kufikia 10,000 na kupanda chati katika wiki za lugha nyingine... Bahati mbaya, sina muda mwingi kukuungia mkono katika harakati zako. Halafu siku hizi napoteza muda kuboresha makala zilizopo kuliko kuanzisha mpya. Asante! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:45, 4 Februari 2009 (UTC)[jibu]

Riccardo Riccioni, salaaaaam! Wikipedia yetu imefikisha makala 11,000! Ni furaha iliyoje? Basi tu, niseme tujitahidi kuendeleza na kushauriana kwa kila jambo litakalosaidia Wikipedia yetu kuwa juu! Kila la kheri.--Mwanaharakati (Longa) 15:51, 9 Aprili 2009 (UTC)[jibu]

Tuzo ya Barnstar[hariri chanzo]

Barnstar Hongera: Umepewa Tuzo ya Barnstar!

Kwa juhudi ya kazi zako hapa katika Wikipedia ya Kiswahili!--Mwanaharakati (Longa) 14:37, 27 Aprili 2009 (UTC)[jibu]

Ukifanyakazi kwa kiasi kikubwa katika Wikipedia, basi unastahili pongezi ya TUZO YA WIKI kila unapochangia zaidi! Ukifungua ukurasa huo, utaona maelezo marefu kuhusu BARNSTAR kwa lugha ya Kiitalia! Kila la kheri.--Mwanaharakati (Longa) 13:06, 30 Aprili 2009 (UTC)[jibu]

Jamii za Juu na Chini[hariri chanzo]

Riccardo Riccioni, salam! Kuna tatizo nimeliona, kaka. Ukianzisha JAMII, unatakiwa pia uweke JAMII za chini. Kwa mfano: JAMII ya JUU

  • Jamii:Nyimbo za Tupac

JAMII ya CHINI

  • Jamii:Nyimbo msanii kwa msanii

Kifupi hakuna jamii bila mwenziwe. Na ikiwa hakuna uwezekano wa kupata mwenziwake, ni afadhali zisiumbwe! Bimaana, JAMII YA WANAMUZIKI WA TANZANIA, ipo chini ya WATU WA TANZANIA. Natumai ya kwamba utakuwa umenielewa namna jinsi nilivyoeleza. Kazi njema.--Mwanaharakati (Longa) 05:07, 4 Mei 2009 (UTC)[jibu]

Nimemteua Mwanaharakati achaguliwe kuwa msimamizi mkuu pamoja nasi (b'crat). Naomba upige kura kwenye ukurasa wa wakabidhi. Asante! --Baba Tabita (majadiliano) 07:17, 28 Mei 2009 (UTC)[jibu]

Nimemteua Flowerparty achaguliwe kuwa mkabidhi pamoja nasi. Naomba upige kura kwenye ukurasa wa Wakabidhi. Ahsante! --Mwanaharakati (Longa) 10:34, 9 Julai 2009 (UTC)[jibu]

Hongera ya makala 12,000[hariri chanzo]

Riccardo, salam! Hongera kwa kusukuma Wikipedia yetu na kufikisha makala zaidi ya 12,000! Ninatumainia kuona michango yako mengine kibao kuliko hiyo uliyoifanya hapo awali!. Siku takii lolote lile, isikuwa kheri ya maisha. Wako kijana mtiifu, MuddybA.K.A.--Mwanaharakati (Longa) 13:02, 25 Julai 2009 (UTC)[jibu]

Riccardo, bila samahani kwani mjadala huu ni wetu wote! Kuhusu kungongeza mbegu: ni vyema pia kuongeza mbegu kwani hata ile Wikipedia ya Kiitalia ilipiga hatua kubwa kwa kufuatia mbegu zilizowekwa (niliyajua haya wakati ninaandika makala kuhusu matoleo ya Mawikipedia - ya Kiitalia umekuwa kubwa baada ya kujaza mbegu za miji na vitongoji vya Ufaransa). Hivyo tunakaribisha mbegu kedekede. Lete tu, kaka! Kuhusu picha: Pole kwa kusahau tena. Picha ukitaka ije hapa ni lazima uhakikisha kwamba hiyo picha ipo kwenye commons? Ikiwa ipo, basi suala lake ni dogo sana, kaka yangu. Ni kiasi cha kubadili tu kama umeitoa kutoka Wikipedia ya Kiitalia (jinsi ulivyoeleza "Immagine" badilia kuwa [[Picha:jina la faili.jpg/ siyo lazima iwe .jpg hata kama ipo .png, .svg, .gif na kadhalilika|thumb|righ/left/centre - vyovyote vile|ukubwa wa picha/mfano 250px|maelezo ya picha.]] Umeelewa?--06:31, 27 Julai 2009 (UTC)

Ndugu Riccardo, salaam! Narudi sasa hivi kutoka kwako nyumbani (ziara ad limina apostolorum..) naona swali lako kwenye ukurasa wa Muddy kuhusu picha. Kila picha iliyopo kwenye commons inaonekana ukibadilisha tu "immagine" kuwa ""picha" kwenye jina lake. Majina ya Kiingereza hupokelewa vile bila mabadiliko kama picha iko kwenye commons. Lakini picha nyingi ziko tu kwenye wikipedia ya lugha fulani. Hapa kua njia ifuatayo: a) unanakili picha kwa kompyuta yako (je hii unajua? rightclick - save image as - halafu uiweke mahali unapojua kwa mfano desktop) b) katika sw.wikipedia unapakia picha: bofya "pakia faili" kwenye orodha upande wa kushoto-chini, fuata maelezo kwenye fomu c) nashauri kufuta picha baadaye kwenye mashine yako kusudi usijaze nafasi iliyopo mno.

Wasalaam --Kipala (majadiliano) 09:30, 28 Julai 2009 (UTC)[jibu]

Ushauri uliokokotezwa. Ukipakia picha kutoka Wikipedia zingine usisahau kuiwekea mabano ya hatimili (license tag). Bimaana usipofanya hivyo, siku hizi tumepata mtu wa kushughulikia picha (Flowerparty) ninamashaka ataiondoa ikiwa haina maelezo yeyote ya hatimiliki! Pole kwa mengi tuliokueleza!--Muddyb MwanaharakatiLonga 13:19, 7 Agosti 2009 (UTC)[jibu]

Riccardo, salaam! Si umeona kwamba tumekuwa wa kwanza katika Afrika - na taarifa hizo ulinieleza hapo juzi. Leo hii tumefikia 13,000!!! Basi hongera na tuendelee kushauriana!--Muddyb MwanaharakatiLonga 08:03, 18 Agosti 2009 (UTC)[jibu]

defaultsort[hariri chanzo]

Bila samahani. Machoni mwangu, 'Defaultsort' maana yake ni kuorodhesha kufuatana na alfabeti. Kwa hiyo naona, mtakatifu ambaye hana jina la familia, aorodheshwe chini ya jina lake la kwanza na siyo chini ya jina lake la mahali wala la baba. Tunaweza kuongeza ubini ila tusiuweke kwanza katika 'Defaultsort'. Au unasemaje? Kila la kheri, --Baba Tabita (majadiliano) 10:56, 3 Septemba 2009 (UTC)[jibu]

Riccardo, salam. Unaweza kuchungulia majadala huu mara moja?--Muddyb MwanaharakatiLonga 13:10, 4 Septemba 2009 (UTC)[jibu]
Labda ni mimi ambaye sijakuelewa vizuri. Ungalikuwa umeniorodheshea makala za watakatifu hao watatu ili niangalie mimi mwenyewe, ningalikuelewa haraka zaidi. Kwa vyovyote inaonekana kama tumeelewana hatimaye. Ila katika tamaduni zetu kuna tofauti kati ya jina la familia na jina la baba. Ndiyo maana, tukiangalia ubini, hatuelewi kitu kilekile. Hata hivyo, ni vizuri kumworodhesha mtu yeyote katika 'Defaultsort' kulingana na jina lake ambalo chini yake amejulikana vizuri zaidi - liwe jina binafsi au jina la familia (sijamkuta mtu anayejulikana chini ya ubini). Wasalaam, --Baba Tabita (majadiliano) 13:16, 4 Septemba 2009 (UTC)[jibu]
Ah - nimeanza kuelewa. Umebadilisha mfululizo wa majina ya watu fulani baada ya kubadilishwa nami. Ukiangalia k.m. Mtakatifu Alberto Hurtado, wikipedia nyingine, hata ya Kiitalia na ya Kiingereza, zinamworodhesha chini ya H, na siyo chini ya A. Tufuate mifano yao. Asante! --Baba Tabita (majadiliano) 13:42, 4 Septemba 2009 (UTC)[jibu]

Riccardo, salaam! Husika na kichwa cha habari hapo juu ni sanduku la kujumlishia habari za Watakatifu kama jinsi wanavyoweka katika Wikipedia zingine. Dhumuni la kuandika ujumbe huu ni kukutaka utoe msaada wako wa kutfasiri baadhi ya maeno yaliyomo kwenye kigezo hicho. Binafsi najua kuandika kaziliwa wapi/kufa na kadhalika. Mengine kama "feast" (ndani yake kuna maneno kama "calender of saints"). Si kazi kubwa saana. Lakini ningependa tufanye pamoja kwa sababu kazi hii inakuhusu sana wewe. Ni katika kutaka kuboresha makala zako zaidi, kaka yangu. Ukiwa tayari, basi nijulishe! Unaonaje?--Muddyb MwanaharakatiLonga 09:52, 5 Septemba 2009 (UTC)[jibu]

Riccardo, salaam! Pole kwa kuchelewa kukujibu! Muda mzuri ni ule wa saa nane au saa tisa. Lakini zaidi ni saa nane naona itakuwa poa zaidi. Ukiona saa nane tu - basi utaona nimebadilisha baadhi ya vitu na kuviorodhesha kwenye ukurasa wa majadiliano husika na kigezo hicho. Wasalaaam!--Muddyb MwanaharakatiLonga 05:59, 7 Septemba 2009 (UTC)[jibu]
Basi kwa sasa hivi unaweza?--Muddyb MwanaharakatiLonga 08:31, 7 Septemba 2009 (UTC)[jibu]
Riccardo: ukitazama yale majadiliano ya lile jedwani utaona mabadiliko kidogo. Je, unaweza kuendeleza zile sehemu zilizosalia?--Muddyb MwanaharakatiLonga 09:49, 7 Septemba 2009 (UTC)[jibu]

Riccardo, salaaaam! Ninapenda kukutaarifu kwamba Wikipedia yetu imefikisha zaidi ya makala 14,000! Ni matumaini yangu kwamba tutafika elfu 15,000? Mmmh, ni safari ndefu! Labda tu nitoe pongezi zako kwa kuendeleza zaidi makala za dini na jamii? Haikuwa kazi rahisi, lakini uliweza! Basi hongera kwa kuliwezesha na kila la kheri katika maisha! Ni mimi mdogo wako mtiifu.--Muddyb MwanaharakatiLonga 14:47, 11 Septemba 2009 (UTC)[jibu]

Riccardo, salam! Ahsante kwa kutupia jicho na kusahihisha makala ya Matengenezo ya Kiprotestanti. Halafu ingekuwa vizuri zaidi ukamalizia kuandika makala ya Matengenezo ya Ukatoliki. Niliiona makala ile kule kwenye Wikipedia ya Kiingereza Rahisi. Wameelezea kama jinsi ilivyo ile ya Uprotestanti. Je, ungependa kuanzisha makala hiyo? Ni mimi mdogo wako,Muddyb, au,--Muddyb MwanaharakatiLonga 08:28, 5 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]
Riccardo, kumradhi kwa kukitelekeza kigezo cha Mtakatifu. Nilijaribu kitu fulani lakini maarifa yangu yalisimama kimwendelezo. Si kitu. Ngoja nipitie tena ili nione wapi nilikwama hapo awali.--Muddyb MwanaharakatiLonga 08:40, 5 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]
Nimebadilisha mfumo wa jedwali la Kigezo:Walimu wa Kanisa‎. Hebu tazama na uniambie kama inafaa?--Muddyb MwanaharakatiLonga 09:57, 5 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]

mradi wa Google kwa ajili ya wikipedia yetu[hariri chanzo]

Bwana Riccardo, salaam!
Nimepata mawasiliano kutoka Christine Moon huko Palo Alto, California. Yeye anafanya kazi kwa shirika la Google, nao wameanza kupanga mradi au huduma kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Tanzania na Kenya ili waelimishwe kuandika makala kwa wikipedia ya Kiswahili. Kumbe!
Christine sasa ametualika kumwandikia maoni yetu, angalia tovuti hiyo:
http://docs.google.com/Doc?docid=0AbIPJ9Nv6udZZGd6MndwcGdfMzFkODNzOG0zYw&hl=en
Bahati mbaya yeye haelewi Kiswahili, kwa hiyo itakuwa lazima kumwandikia kwa Kiingereza. Ukihitaji msaada wangu upande wa kumwandikia, karibu unijulishe. Asante kwa michango yako!
Ni wako katika ujenzi wa lugha yetu, --Baba Tabita (majadiliano) 07:57, 10 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]

Kanisa la Armenia[hariri chanzo]

Riccardo, salam. Kwanza nitoe shukrani zangu nyingi za dhati kwa msaada wako juu ya masawazisho ya makala zenye athira ya kidini. Nimeona maranyingi ukisawazisha (na hata kupanua makala hizo). Leo hii, nimeonelea angalao uandike makala moja au mbili za katika hicho kichwa husika hapo juu - kwa sababu niliona umeiweka sawa kwa kiasi kikubwa. Je, ungeweza angalao kuandika kitu kama labda: Kanisa la Kifalme la Armenia au lile la Katoliki? Yaani, dhumuni la kusema hivi ni kwa sababu kile kiungo au ile maana ya kutofautisha makala zile bila hata kuwepo ni sawasawa na bure! Nitakuwa mwenyekushukuru iwapo utanisaidia kwa hili. Zile makala zingekuwa za kawaida, kwa mfano muziki au filamu, basi ningeendelea mwenyewe. Lakini masuala ya kidini, aah, sijui kitu kwa kweli. Ni hayo tu. Wako,--Muddyb MwanaharakatiLonga 10:55, 13 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]

Riccardo, salaam! Haya, kwanza ahsante kwa kuanzisha makala zile za kidini kama jinsi nilivyoomba hapo juu. Pili, nimeona maranyingi ukiandika "waamini" badala ya "waumini." Sasa hapa sijajua kama ni Kiswahili kipya? Maana, nimezoea kuona wakiandika waumini na si "waamini". Je, hiyo ni sawa?--Muddyb MwanaharakatiLonga 12:55, 19 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]
Muddyb mpendwa, nimefikiria swali lako. Sina hakika, lakini naona neno waumini linamaanisha wafuasi wa dini fulani, wakati waamini linasisitiza zaidi kuwa ndio wanaoamini ufunuo fulani, tofauti na wasiouamini. Ningesema waumini ni neutral zaidi. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 08:25, 26 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]

majadiliano kuhusu utafsiri wa istilahi[hariri chanzo]

Bwana Riccardo, salaam! Nimeanzisha majadiliano mapya kuhusu utafsiri wa istilahi ya wikipedia yetu hapa. Naomba uyaangalie na kuchangia maoni yako. Asante! --Baba Tabita (majadiliano) 09:54, 23 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]

Salaam Riccardo, nimesoma na kukubali hoja lako kuhusu aina na kundi/jamii. Umenishtusha kidogo ktika mfano mmoja uliyotoa kuhusu maharagwa na nafaka. Niliandika makala za maharagwe, jamii kunde na nafaka; kwangu kunde na nafaka ni makundi mawili tofauti. Sina neno ukipumzisha watakatifu kidogo na kuingia kwenye mboga. Ila tu nashukuru kwa maelezo ya ndani aidi --Kipala (majadiliano) 04:08, 26 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]
Ndugu, usihangaike. Biolojia yangu iliishia darasa la kumi tu. Ukiona maharagwe si nafaka,inawezekana nimekosea kutoa mfano. Afadhali nisijaribu kugusa kurasa za mambo nisiyoyajua. Tena watakatifu na mambo ya dini wananivutia zaidi... SHALOM! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 08:20, 26 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]
Baada ya muda mrefu narudia suala hilo kwa kusema nimesoma kamusi ya Kiswahili Sanifu: inasema haragwe ni nafaka... --Riccardo Riccioni (majadiliano) 04:46, 19 Septemba 2010 (UTC)[jibu]

Uchaguzi Mpya[hariri chanzo]

Salam, Riccardo. Unaombwa upige kura katika ukurasa wa wakabidhi wa Wikipedia. Mmoja kati ya wachangiaji wenzetu (Mr Accountable) amejiteua kuwa mkabidhi! Ili kumpgia kura, tafadhali fungua hapa. Ahsante sana.--Muddyb MwanaharakatiLonga 18:39, 28 Novemba 2009 (UTC)[jibu]

Salam, Riccardo! Ahsante kwa masahihisho na ongezeko lako la kwenye makala ya Baptisti. Kwa kweli makala imekaa vyema kabisa. Tatizo langu lipo palepale - sijui mengi kuhusu dini. Ikiwa tunapata msaada kama huo, basi mambo yatakuwa mazuri.--MwanaharakatiLonga 16:33, 5 Machi 2010 (UTC) [jibu]

Eeeh, kweli. Lakini kwa bahati mbaya tafsiri ile sijaitunga miye! Nilisoma kutoka katika kamusi ya TUKI niliyonayo kwenye kompyuta yangu. Ili sema Baptist - SW = Baptisti. Lakini bila kutafakari juu ya uitaji wa wanadini jinsi wafanyavyo, basi ikawa imetokea. Ahsante sana na ni tumaini kila niandikapo makala za dini, basi utawasawazisha!--MwanaharakatiLonga 11:35, 6 Machi 2010 (UTC)[jibu]
Afadhali ulivyoliona hilo! Binafsi nilijaribu, lakini hali yangu haikuwa vyema tena - nikaona bora kutumia muda huo kuanzisha makala mapya kuliko kuendelea na zile. Labda tutarekebisha! Kuhusu Kipala, sifahamu kwa sababu ni muda sasa hatujazungumza kuhusu mahali alipo. Ninatumai yupo kulekule Iran! Ila tu kazi zimembana!!! Salam teeele kutoka mjini Dar es Salaam, Tanzania. Wako,--MwanaharakatiLonga 07:16, 8 Machi 2010 (UTC)[jibu]

Translation request[hariri chanzo]

Hello.

Can you translate and upload the articles en:Azerbaijan Soviet Socialist Republic and en:Azerbaijan Democratic Republic in Swahili Wikipedia?

Yours sincerely, Karalainza (majadiliano) 15:50, 29 Mei 2020 (UTC)[jibu]

Kanisa la Scientology[hariri chanzo]

Salam, Riccardo! Unaweza kunieleza au hata kuandika makala kuhusu kichwa cha bari hapo juu? Ningependa kujua ni dhehebu la namna gani. Wako katika ujenzi wa Wikipedia yetu,--MwanaharakatiLonga 06:54, 19 Machi 2010 (UTC) [jibu]

Salaaam! Ahsante kwa itikio lako la vitendo!!! Ni tumaini lako kwamba nimefurahi, basi kweli nimefurahi!!! Shukrani tena. Wako,--MwanaharakatiLonga 13:43, 23 Machi 2010 (UTC)[jibu]

Hongera ya makala 18,000[hariri chanzo]

Salam, Riccardo Riccioni! Hongera ya makala 18,000! Kumbe tumefika - japokuwa kuna mengi ya kusahihisha na kufuta pia. Lakini si mbaya tukipongezana! Tuendeleeni jamani.--MwanaharakatiLonga 09:13, 31 Mei 2010 (UTC) [jibu]

Wafiadini wa Uganda[hariri chanzo]

Naona kama makala hii inataka kujadili habari za "Wafiadini wa Uganda" ipanushwe kidogo kulingana na pande zote zilizohusika yaani Wakatoliki na Waanglikana. Sasa inaonekana kama habari ya upande mmoja tu inayotaja upande mwingine kandokando. Sawa nikiongeza? Kipala (majadiliano) 11:06, 13 Juni 2010 (UTC)[jibu]

Questionnaire[hariri chanzo]

Nadhani labda wewe umepata pia maswali yale ya Rachel - hapa majibu yangu: Mtumiaji:Kipala/questionnaire - Kipala (majadiliano) 19:08, 30 Juni 2010 (UTC)[jibu]

Kura ya kuamua juu ya wakabidhi waliopotea[hariri chanzo]

Karibu kutembelea ukurasa wa wakabidhi na kuamua juu ya wenzetu waliopewa haki za wakabidhi lakini hawakuonekana tangu miezi mingi: Wikipedia:Wakabidhi#Kura_ya_kuondoa_wakabidhi_waliopotea. Tuliwahi kujadili swali hili mwaka uliopita (tazama kwenye ukurasa unaotajwa, juu ya pendekezo) ; sasa njia imeonekana. Kipala (majadiliano) 05:27, 1 Oktoba 2010 (UTC)[jibu]

Salamu na viungo vya mwili[hariri chanzo]

Riccardo, salaam, nafurahia jinsi unavyochungulia makala nilipoandika na kuboresha Kiswahili na tahajia. Sana nina ombi. Nliwahi kuanzisha makala juu ya viungo vya mwili na hao vijana wa mashindano ya makala za afya waliendelea. Makala hizi zote zinahitaji kuangaliwa kwa sababu Wakenya (nadhani) waliunda sentensi za ajabu kidogo na pia mara nyingi walikosa viungo. Nikiingia hapa nakiri udhaifu: kwa Wasafwa na Wanyakyusa nilipojifunza Kiswahili na baadaye Nairobi sijasikia kitu kingine ila "mkono" na "mguu". Kumbe. Sasa nimetengeneza picha ya mkono nikilenga ktaja sehemu zake kuanzia bega kupitia kisugidi hadi kiganja. Lakini ninahisi ya kwamba sina uhakika kwa sababu sina uzoefu kutaja sehemu zile (yooote mkono!) na kamusi zangu si wazi sana; mara nyingi maelezo si kamili, yanaingiliana maana au kuna maneno kadhaa na mimi sijui lipi ni afadhali. Je unajua wewe majina haya au unaweza kuchungulia kidogo? Tuanze kumaliza mkono baadaye inafuata mguu na mengine! Namwuliza pia Muddy ni vema kusikia jinsi wanavyosema Dar. Asante ndimi wako Kipala (majadiliano) 08:38, 10 Aprili 2011 (UTC)[jibu]

Asante kwa maneno yako ya kunitia moyo. Kuhusu viungo vya mwili mimi pia nina shida kuelezea sehemu mbalimbali, labda hata kwa Kiitalia! Sidhani nitaweza kukusaidia. Shalom! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:03, 11 Aprili 2011 (UTC)[jibu]

Bunda vijijini[hariri chanzo]

Je kuna wilaya ya Bunda vijijini?? Kama iko naomba habari na marejeo kwa ajili ya makla za wilaya / Mkoa wa Mara. Kama la, makala ya Jimbo Katoliki la Musoma isahihishwe. Kipala (majadiliano) 11:05, 22 Januari 2012 (UTC)[jibu]

Sidhani... ni haraka tu ya kuandika! Samahani! --41.221.34.70 08:04, 25 Januari 2012 (UTC)[jibu]
Pamoja na hayo, hatujaingiza mikoa (k. mf. Njome, Simiu) na wilaya mpya za Tanzania (k. mf. Gairo, Nyasa). --41.221.34.70 08:10, 25 Januari 2012 (UTC)[jibu]
Asante kwa jibu. Kuhusu mikoa na wilaya mpya - niko mbali. Unaweza kuanzisha makala ?Kipala (majadiliano) 13:08, 25 Januari 2012 (UTC)[jibu]
Sina DATA za kutosha. --41.221.34.70 14:26, 28 Januari 2012 (UTC)[jibu]
Hatimaye serikali imetoa tangazo rasmi kuhusu mikoa mipya 4 na wilaya 19 (si tena 21!), ingawa lenyewe lina utata kama jamaa alivyolalamikia katika ukurasa juu ya Wilaya ya Wanging'ombe. Naomba ukurasa kuhusu mkoa wa Simiu usogezwe kwa kuandika Simiyu. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 18:04, 10 Machi 2012 (UTC)[jibu]

Barnstar kwa ajili yako![hariri chanzo]

Barnstar kwa Ajili ya Mchangiaji Asiyechoka

Hongera kwa juhudi zako!--MwanaharakatiLonga 07:57, 21 Agosti 2012 (UTC) [jibu]

Ndugu Muddy, asante kwa pongezi zako. Nazipokea kwa mikono miwili kutoka kwako, bosi! Ni kweli sijachoka kuchangia Wiki. Ila nasikitika kuona umepunguza kasi zako, na pengine nawaza kuwa nimesababisha mimi mwaka juzi. Hivyo napata moyo ninapoona matendo kama hili na lile la kuupandisha chati ukurasa juu ya mpendwa wetu Bikira Mariamu. Mungu atujalie daima amani! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:49, 26 Agosti 2012 (UTC) [jibu]

Hapana, Riccardo! Hamu imepungua yenyewe natural. Sijui kwanini - naona bora nicheze na Facebook kuliko kuja Wikipedia ya Kiswahili. Huwa najitahidi hivyo-hivyo tu. Usijali. Nitajitahidi nirudie kama zamani - ila tu, hizi zama zingine! Nimetumikia Wikipedia hii kwa miaka minne mfululizo bila kusimama! Labda umefika wakati wa kupumzika huku nikijisukuma polepole huenda ile mojo ya zamani ikarudi! Narudia tena, hahusiki na kupotea kwangu. Hii ni hiari yangu na wala silazimishwi. Kila la kheri, mzee wangu!--MwanaharakatiLonga 16:18, 28 Agosti 2012 (UTC)[jibu]

Uzoroastro[hariri chanzo]

Salaam nimeona makala nimefikiri umbo la jina Zoroasta / Uzoroasta labda ingefaa zaidi. Jinsi ilivyo naona sasa tatizo ya kwamba umetumia jina "Zoroaster" lakini dini kama "Uzoroastro" ambako ninahisi Kiitalia iliingilia kidogo. Unaonaje? Kipala (majadiliano) 11:46, 1 Novemba 2012 (UTC)[jibu]

Ndugu Kipala, ni furaha kila ninapoona unaendelea kujitokeza katika wiki yetu. Kuhusu jina la dini hiyo, inawezekana athari ya Kiitalia, lakini pia jina la Kiingereza Zoroastrianism limechangia. Sina shida ukipenda kubadilisha jina liwe rahisi zaidi. Samahani, niliwahi kuandika ombi la kurekebisha picha uliyoswahilisha ya mwaka wa Kanisa, kwa kuandika Siku Tatu Kuu za Pasaka badala ya Ijumaa Kuu - Pasaka: ni mtazamo mpana zaidi, unahusisha karamu ya mwisho na Jumamosi Kuu katika umoja wa fumbo la Pasaka. Asante. Amani kwenu! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:07, 2 Novemba 2012 (UTC)[jibu]

Riccardo, salaam. Ni siku nyingi sana zimepita na sijapata kujua hali yako na hata kuomba msaada wa hapa na pale. Haya, leo nimekuja na shida kidogo. Ninaomba urekebishe hiyo makala kama unaelewa jamaa alitaka kumaanisha kitu gani. Nimeona mambo yanayokuhusu - ndiyo maana nimekuja kwako. Tafadhali saidia kupanua makala hiyo ili iwe Kiwikipedia zaidi na kuleta maana vilevile. Wako, Muddyb, au--MwanaharakatiLonga 09:54, 4 Juni 2013 (UTC) [jibu]

Ni kweli, hatuwasiliani sana, ingawa ninahitaji bado maelekezo yako ya kiufundi. Kwa mfano, nikitaka kuongeza kati ya lugha zangu Kihehe, nitumie kifupisho kipi? HH? Au hairuhusiwi? --Riccardo Riccioni (majadiliano) 08:05, 6 Juni 2013 (UTC)[jibu]
Haya, kama nimeweza kukuelewa - unajaribu kumaanisha zile lugha zako za ukurasa wa mtumiaji? Ikiwa ndiyo, basi naona hili hapa: katika msimbo wa lugha ya Kihehe kimataifa ni "heh". Sasa utatazama kama hatua yako ni "Heh" 1, 2, au 3! Ukijibu tu, nitakutengenezea kigezo cha lugha hiyo haraka iwezekanavyo. Ukiona unaweza kuendelea mwenyewe, basi sawa tu. Wako Muddyb au,--MwanaharakatiLonga 12:00, 7 Juni 2013 (UTC)[jibu]

Aiuto per favore![hariri chanzo]

(Kiitalia) Scusami, signor Riccioni.
Il mio italiano non è buono.

(Kiingereza) Can you help me with a small translation?
My page en:Le Monde's 100 Books of the Century
What is a good Swahili name for the page?
(Ho scritto anche la pagina italiana it:I 100 libri del secolo di le Monde.)
Mille grazie. Nel Canada, Varlaam (majadiliano) 15:28, 15 Julai 2013 (UTC)[jibu]

Hello again.
The table now looks like this.
It is always best to check the words with someone who really speaks the language.
Nambari ? Mada ? Mwandishi Mwaka
1 The Stranger
Mgeni
Albert Camus 1942
Because there is only a limited amount of information available in Swahili, the page has working links into enwiki.
Thanks again, Varlaam (majadiliano) 19:22, 17 Julai 2013 (UTC)[jibu]

Vandalism(o)[hariri chanzo]

Greetings again. I just repaired some vandalism to the Tanzania article, but I did not issue any warning, since I do not speak the language.

Fransisko wa Asizi:
I saw his name at the top of this page.
I saw St. Francis's robe in the museum in Assisi.
You feel that you are in the presence of greatness.
Varlaam (majadiliano) 23:49, 19 Julai 2013 (UTC)[jibu]

Bureaucrats.
Perhaps swwiki works differently from other projects. In other projects, it is usually experienced editors, rollbackers, admins who issues warnings, not bureaucrats specifically.
I think a lot of projects have a template, with mature and reasonable wording, and then any responsible person can use that template, and simply add his name to its words.
But I have not tried to discover how swwiki handles this problem.
Best regards, Varlaam (majadiliano) 06:35, 21 Julai 2013 (UTC)[jibu]
We don't have many editors in this Wiki. Feel free to provide any kind of help on that aspect. Surely I'm not an admin, but what if things happened and I need to take action for? Also you're allowed to create the tamplate and happily to have it translated into Kiswahili. With best regards,--MwanaharakatiLonga 10:25, 22 Julai 2013 (UTC)[jibu]

Wiki Indaba conference[hariri chanzo]

Salaam, P.Riccardo. Kuna mpango wa mkutano mjini Johannesburg mwezi wa pili mwakani, angalia http://wikiindaba.net/index.php?title=Main_Page - pia, umeombwa kujibu maswali yao kwenye tovuti la Google docs: https://docs.google.com/forms/d/1zEk6hw4IiQYVrdJGYphPhQHOQFi4wdOIXvzVj9vy_gU/viewform Asante kwa msaada wako. Wasalaam, --Baba Tabita (majadiliano) 12:32, 4 Novemba 2013 (UTC)[jibu]

Wilaya mpya, kata[hariri chanzo]

Salaam Riccardo! Naone umeshaanza kuhariri makala kadhaa za wilaya mpya. Mimi nimeangalia matokeo ya sensa naona hapa kuna orodha kamiliy a kata na wilaya kwa hali ya 2012. Kuna mabadiliko mengi. Kwa sasa naandaa orodha ya kata zota za wilaya zote; maana kuna wilaya mpya lakini pia kata mpya katika wilaya zote. Je unaweza kusaidia hapa? Nikipata email yako naweza kukutuma faili za excel na word penye orodha hizi. Asante. Kipala (majadiliano) 21:57, 27 Novemba 2013 (UTC)[jibu]

Mzee, nitasaidia kidogo kadiri ya nafasi. Anwani yangu ni ndugurikardo@yahoo.it SHALOM! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:04, 29 Novemba 2013 (UTC)[jibu]

Asante ![hariri chanzo]

Napenda kukushukuru kwa kuchungulia mara kwa mara michango yangu! Kwa kweli naona A) kuna udhaifu upande wangu kurudia kusoma kwa makini yale niliyoandika na B) ilhali nakaa mbali na Waswahili siku hizi Kiswahili changu kimedhoofika kiasi - kwa hiyo: Asante! Kipala (majadiliano) 21:26, 17 Desemba 2013 (UTC)[jibu]

Mzee, nafurahi kuchangia juhudi zako kwa ajili ya Afrika Mashariki. Hapa juu nilijibu ombi lako kuhusu wilaya mpya. Vipi, bado uko Iran? Ningependa kujua unafanya nini huko. Anwani yangu ya e-mail ni hii hapa juu. Heri za Noeli! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:18, 22 Desemba 2013 (UTC)[jibu]

Update on Upcoming Wiki Indaba Conference[hariri chanzo]

Hello Sir. My name is Rexford Nkansah, currently serving as a Wikipedian in Residence at the Africa Centre in Cape Town.

The Wikimedia Foundation has shared with us the incredible number of edits that you have done on this Wikipedia. You have are one of those with the high contribution to this Wikipedia.

As one of the highest contributors to one of the languages of the African continent, I want to inform you about the upcoming Wiki Indaba Conference which is similar to Wikimania, however, its designed by Africans for Africans.

This message is to inform you about scholarship to attend application currently open. You're invited to apply for scholarship to attend this conference.

Please see the main Wiki Indaba Website for more details on Eligibility and Deadline – look at www.wikiindaba.net for more details. And like the facebook page for updates.

Please don't hesitate to get in touch should you have any questions.

my contact is rexford[@]wikiafrica.net

Naomba ushirikiano wako![hariri chanzo]

Mpendwa, nakuomba uangalie baada ya siku 2,3 kurasa hizi mbili:

1. Wikipedia:Wakabidhi#Kusafisha_orodha_ya_Wakabidhi_mwaka_2014
2. Wikipedia:Ukurasa_wa_jumuia#Wiki_Indaba_2014

Kuhusu 1) napendekeza kuwachagua wakabidhi wapya na kuondoa wale waliomo katika orodha ya wakabidhi lakini hawakuwepo tangu miaka 2.

Kuhusu 2): nahitaji msaada na mawazo yenu. Nitashiriki kwenye mkutano wa Wikimedia mwezi wa Juni. Inaonekana mimi ndipo mchnagiaji wa pekee kutoka Wikipedia yetu. Ninajitahidi kupeleka mawazo ya jumuiya yetu. Naomba michango!

Nitaongeza karibuni mawazo yangu kuhusu mambo ninayoona kuwa na maana kwa mtazamo wangu. Ujumb huu natuma kwa wachangiaji wanaoonekana katika orodha ya wachangiaji hai waliochangia zaidi ya mara 3 katika siku 30 zilizopita!

Ndimi wako Kipala (majadiliano) 20:27, 13 Mei 2014 (UTC)[jibu]

Hongera na Pole![hariri chanzo]

Nd Riccardo, sijui kama umeona ya kwamba umepigiwa kura kupewa madaraka ya mkabidhi katika wikipedia hii? Nataka kufunga kura sasa karibuni wote walioshiriki walisema NDIYO. Ni cheo kidogo zaidi nafasi ya kufanya kazi... Namshukuru Mungu ya kwamba umejiunga nasi! Kipala (majadiliano) 07:20, 22 Mei 2014 (UTC)[jibu]

Ndugu, sikuona chochote. Imekuwaje? Ninachoweza kusema ni kuwa sina utaalamu zaidi wa kompyuta, hivyo mambo mbalimbali ya Wiki kwangu bado ni mafumbo... Nadhani nitakachoweza kufanya ni kuendelea kama sasa. Kwa vyovyote, asante kwa walionipa kura, kwa wale wasionipa na hasa kwako. Amani kwenu!
Ingekuwa msaada sana kama unashiriki tu kila unapoingia A) kuwapa watumiaji mapya waliojiandikisha alama ya {{karibu}} na B) kila unapoona makala mpya kuitazama na ukiona haifai au kama una mashaka kuweka alama ya {{futa}} juu kabisa ya makala na kuiingiza katika Wikipedia:Makala kwa ufutaji. C) ukiona makala iliyoharibiwa kwa kuingiza matusi au fujo tupu ni vema kumzuia huyu aliyeandika. Kuzuia anwani zisizoandikishwa ina faida ndogo to mara nyingi ni internet cafe lakini mimi nambana hata hivyo kwa muda. Hata kama unafanya A) pekee itasaidia. Kipala (majadiliano) 20:37, 23 Mei 2014 (UTC)[jibu]
OK, nitajifunza... --Riccardo Riccioni

Article request questions[hariri chanzo]

Hi, Riccardo! Do you do article requests in Swahili? There are some aviation-related articles and articles about Kenya on the English Wikipedia which do not yet have Swahili versions. If you are interested I can give you a list.

Thank you WhisperToMe (majadiliano) 07:57, 19 Agosti 2014 (UTC)[jibu]

Caro Riccardo, Pace!

Ho visto che hai fatto alcune modifiche alla pagina del nouvo vescovo della mia diocesi, grazie! Ti chiedo, quando avessi 5 minuti, di inserire qualche notizia o nota per ampliare la pagina.

Ti ringrazio per l'aiuto e ti auguro buona domenica. Grazie ancora e a presto

Rei Momo (majadiliano) 12:48, 31 Agosti 2014 (UTC)[jibu]

Grazie mille! Rei Momo (majadiliano) 14:51, 31 Agosti 2014 (UTC)[jibu]

Kupakia mafaili, Sogora ya kupakia?[hariri chanzo]

Wikimedia Commons logo

Hello! Sorry for writing in English. As you're an administrator here, please check the message I left on MediaWiki talk:Licenses and the village pump. Thanks, Nemo 19:22, 18 Septemba 2014 (UTC)[jibu]

Kigezo Ukristo![hariri chanzo]

Salaam. Mzee wangu, ile kazi uliyonituma nimeimaliza! Sasa zimeungana na kama ulivyotaka! Kila la kheri..--MwanaharakatiLonga 14:54, 22 Septemba 2014 (UTC) [jibu]

Hello! Could you translate an article about boycott of Russian goods in Ukraine for the Swahili Wikipedia? Thanks for the help. --Trydence (majadiliano) 16:00, 16 Oktoba 2014 (UTC)[jibu]

Rosetta / Churyumov–Gerasimenko[hariri chanzo]

Rafiki, umenishinda!! Nafungua makala nataka kuingiza habari - kumbe iko tayari! Asante!! --Kipala (majadiliano) 08:58, 13 Novemba 2014 (UTC)[jibu]

Ndugu Kipala, asante kwako. Tunaendeleza ulichoanzisha wewe. Sikiliza, tangu mliponichagua kuwa sysop nimejitahidi kufanya nilichoweza, lakini nimeona shida moja: niki-patrol kurasa mpya natoa maoni yangu katika ukurasa wa majadiliano, lakini baadaye naona kimya. Mara chache nimeambiwa nikate shauri mimi nisisubiri, lakini mara nyingine ni muhimu kusikia nyinyi mnasemaje. Au niandike katika ukurasa wako mwenyewe? --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:14, 15 Novemba 2014 (UTC)[jibu]

Kuhusu mkutano wa Machi 2015 na mawasiliano na WMF[hariri chanzo]

Salaam naomba utazame hapa: Majadiliano_ya_Wikipedia:Wakabidhi#Mawasiliano_na_ofisi_ya_WMF_-_Wikimedia_Foundation_.2F_Asaf_Bartov na kuchangia. Kipala (majadiliano) 09:56, 3 Desemba 2014 (UTC)[jibu]

Asante kwa ushauri woote! Sasa naomba lete pendekezo na namba. Binafsi sijali nyota sana pia sina picha siku hizi nyota ina maana gani TZ. Mende wachache (au bila - ikiwezekana), usafi kiasi, vyumba vilivyoona rangi mpya karne hii... Mimi nahitaji kiasi fulani ninayoweza kutaja, je unaweza kuulizia? Nitashukuru!! Kipala (majadiliano) 08:30, 3 Januari 2015 (UTC)[jibu]
Riccardo, samahani nikirudia ombi langu la hapo juu. Unaweza kunipa makadirio yoyote kuhusu gharama ya malalo? Asante Kipala (majadiliano) 18:46, 10 Januari 2015 (UTC)[jibu]

Habari gani?[hariri chanzo]

Ubarikiwe, ndugu! Kipala (majadiliano) 13:55, 21 Machi 2015 (UTC)[jibu]

AutoWikiBrowser[hariri chanzo]

Ndugu, kiungo cha hiyo programu ni https://en.wikipedia.org/wiki/Wikipedia:AutoWikiBrowser - ubarikiwe! --Baba Tabita 14:08, 21 Machi 2015 (UTC)[jibu]

Kitabu cha Historia ya Kanisa[hariri chanzo]

Ninavyoona hakimiliki ziko kwangu. Kilichapishwa na "Motheco Publishers" - sijui kama bado wako lakini hakuna mapatano kati yetu yale yote yalikuwa kimdomo tu na watu ambao hawako tena leo. Nisingekuwa na tatizo kuiweka kwenye wikitabu ukiona inaweza kufaa (nilisita maana sijaridhika tena) lakini kule kumefungwa.Kipala (majadiliano) 13:53, 3 Aprili 2015 (UTC)[jibu]

Mchango wa mawazo[hariri chanzo]

Ndugu Riccardo Riccioni, kuna makala nimetunga, lakini kumbe yapo mengine (ijapokuwa ile yangu imetanuka zaidi). Tafadhali tupieni jicho hapo: Majadiliano:Uislamu nchi kwa nchi.. Kisha fanyeni uamuzi..--MwanaharakatiLonga 19:07, 15 Aprili 2015 (UTC) [jibu]

Shukrani kwa masahihisho[hariri chanzo]

Ndugu Riccardo, salaam. Shukrani sana kwa masahihisho. Siku nyingi zimepita bila kuhariri na nahisi shida za hapa na pale.. Tuvumiliane hivyohivyo. Eh, tena nitafurahi kama utaendelea kuweka lugha sawa. Uwezo wangu umepungua kiasi kikubwa sana!--MwanaharakatiLonga 15:47, 17 Aprili 2015 (UTC) [jibu]

Ndugu Riccardo, salaam. Nimeanza kuchoka na Silausi alivyochoka pia Ndg Muddyb. Huyo Silausi akiendelea kubadilisha makala bila kufuata mashauri yetu na kanuni za Wikipedia:Umaarufu, nitamzuia kwa muda kadhaa. Bahati mbaya inaonekana kama ataanzisha akaunti nyingine tena alivyofanya baada ya kuzuiliwa kama Mtumiaji:Lusajo Chicharito Brown. Unaonaje? Wasalaam, Baba Tabita (majadiliano) 16:45, 29 Juni 2015 (UTC)[jibu]

Tukimtambua, naona tumzuie kwa jina lolote na kufuta kurasa zake zote. Atachoka tu. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:39, 30 Juni 2015 (UTC)[jibu]

Wingi wa ushanga![hariri chanzo]

Salaam, Ndugu Riccardo. Eti wingi kirai au neno "Ushanga" ni aje?--MwanaharakatiLonga 08:00, 4 Agosti 2015 (UTC) [jibu]

Vipi? Si shanga? Walau nasikia hivyo, ila sijaangalia kamusi yoyote. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:49, 6 Agosti 2015 (UTC)[jibu]
Basi nilifanya hivyo, lakini katika makala ya masafa marefu ulibadili wingi wake na kuweka umoja wake.. Niliandika biashara ya shanga (wingi) ukaweka "ushanga" (umoja). Swali, waliuza shanga au ushanga? Biashara zilivyo - sidhani kama watafsiri masafa marefu kwa kitu kimoja. #SamahaniLakini. Wako--MwanaharakatiLonga 06:40, 7 Agosti 2015 (UTC)[jibu]
Sijui ilikuwaje. Sasa nimerekebisha kwa kuwela kiungo kwenda umoja, na labda ndivyo nilivyotaka kuboresha makala yako. Pole kwa usumbufu. Mara nyingi tunafanya kazi kwa hofu ya umeme kukatakata! Amani kwako. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:49, 7 Agosti 2015 (UTC)[jibu]

Tafadhali uangalie jamii kuhusu mfumo wa kuanzisha makala[hariri chanzo]

Mpendwa, nakuomba kuaangalia ukurasa wa Jumuiya. Tuliomba wikimedia ya kutpa mfumo wa kuzuia watumiaji wasiojiandikisha wasianzise makala mapya. Kusudi lilikuwa kupunguza idadi ya makala mabaya yasiyotosheleza masharti ya wikipedia ilhali tuko wachache mno kuziangalia. Wikipedia kubwa kadhaa zinatumia utaratibu huu (kama en:wikipedia) lakini sisi tunapaswa kupeleka ombi kwa kamati fulani. Kamati hii wametupa nafasi kwa kipindi ha miezi 6 tu inayokwisha karibuni. Sasa wanakamati wamekuja wanadai tujieleza au watarudisha mfumo huu nyuma. Mimi nikiwa 1 kati ya wachache wanaochugulia makala mapya naona itaturudisha nyuma. Naomba mchangie! Sanaaaaa!! Kipala (majadiliano) 23:35, 10 Septemba 2015 (UTC)[jibu]

Ndugu zangu, hongera ninyi nyote kwa kufikia makala 30,000, kazi nzuri! Mlifanya mbio za nyika kweli. Nilisafiri kwa hivyo sikuiona sasa hivi. Tuendelee mpaka hatua ijayo: 40,000. ChriKo (majadiliano) 17:53, 24 Septemba 2015 (UTC)[jibu]

RE:Infobox Country[hariri chanzo]

Salaam Ndugu Riccardo. Ahsante kwa pongezi (ijapokuwa sijioni miongoni mwa hao wanaostahili! Kuhusu vigezo tajwa hapo juu, kwanini usimuulize Kipala? Yeye ndiye alikuwa anaumba (nadhani) kama sio kuumba, basi kutumia mara kwa mara. Au labda ungefuata kimoja kizuri kisha tumia kama msingi wa maumbo ya baadaye. Wako, Muddyb au--MwanaharakatiLonga 14:25, 25 Septemba 2015 (UTC) [jibu]

Mwendokasi![hariri chanzo]

Salaam Ndu. Riccardo Riccioni! Ninahisi sasa punde sitokushika tena. Mwendokasi huu ni zaidi ya garimoshi la umeme. Hongera na makala ya Historia ya Afrika. Sikupati tena.. Ila pongezi sana. Wako,--MwanaharakatiLonga 07:10, 1 Oktoba 2015 (UTC) [jibu]

Elimu ndio msingi wa maisha ya binadamu.

Nakuasa ndugu tujaribu kukumbuka hata kidogo hawa wenzetu wanaofanya mtihani wa kidato cha nne Mungu awape uzima tele na kuwakumbusha yale ya msingi waliyoyafanya kwa kipindi cha miaka minne walipokuwa shuleni,pia awalinde katika kufanya mtihani wa mwisho wa kumaliza shule kwa 0,level.

Tunaomba uiombe shule yetu katika kipindi hiki kigumu mitihani ya taifa

TUITUNZE AMANI YETU HAPA NCHINI TULIYOJALIWA NA MWENYEZI MUNGU

SHUKRANI[hariri chanzo]

Tunakushuru ndugu Riccardo kwa kutupa malezi bora hapa shule na tunamuomba mungu akujalie maisha maisha malefu zaidi na akupatie nguvu ili uendele kuifanya kazi yake BWANA

Mpendwa, uliniandikia kwenye ukurasa wangu nikajibu sijui kama uliiona. Kama la angalia hapa: Majadiliano_ya_mtumiaji:Kipala#Kujisomea. Nitafurahi kuona jibu lako!! Kipala (majadiliano) 17:56, 15 Novemba 2015 (UTC)[jibu]

meanings of mafuta[hariri chanzo]

Hello, nice to meet you and sorry for writing in English. I noticed that you had removed interwiki links at that page which are bound with a concept oil. I probably understand why you did so, because the term mafuta has at least two meanings: “oil / olio” and “grease / grasso”. Do I think right about it? If so, I would like to add this page to the links of d:Q10379768, which treats the both above-mentioned meanings. Your sincerely, Eryk Kij (majadiliano) 04:17, 7 Januari 2016 (UTC)[jibu]

May be, but I don't understand those languages. If you are certain, link them with Swahili mafuta. I think I removed the links because now we use Wikidata. But if I did a mistake, let you undo my deletion. All the best! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:44, 9 Januari 2016 (UTC)[jibu]

Kazi ya Mcdonaln Aloyce Fute[hariri chanzo]

Ndugu Riccardo, salaam. Ikiwa MCDONALN ALOYCE FUTE ni mwanachama wa kilabu chenu huko Morogoro, labda umwambie kwamba haileti faida kubwa akiendelea kuanzisha makala nyingi za miaka kabla ya Kristo kama hata wanahistoria wataalamu hawajui kitu kuhusu miaka ileile (ukiangalia wikipedia ya Kiingereza utakuta kwamba miaka kadhaa haina makala). Tuingize habari zifaazo katika makala zetu. Wasalaam, --Baba Tabita (majadiliano) 13:05, 23 Januari 2016 (UTC)[jibu]

Ndugu, ni kweli unavyosema. Mcdonaln ni mwanafunzi wetu wa kidato cha tatu, hivyo anachangia anavyoweza. Acha kwa sasa azoee kazi na kuipenda. Baadaye atatoa mchango wa thamani zaidi. Shalom! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 06:21, 24 Januari 2016 (UTC)[jibu]
Ndugu Riccardo, ni sawa azoee. Lakini sasa kuanzisha makala za miaka ya KK bila yaliyomo hakutamfundisha kuipenda kazi ya wikipedia. Nilimshauri aingize angalao tukio moja kwa kila mwaka ili wasomaji wapate faida. Mpaka sasa hajajibu, anaendelea kuanzisha makala mpya tu bila habari. Naomba uongee naye ana kwa ana. Lazima aendelee katika michango yake badala ya kuanzisha makala tupu tu. Asante. --Baba Tabita (majadiliano) 19:42, 14 Februari 2016 (UTC)[jibu]
Ukisikia maneno ya kiutuzima ndiyo haya! Yaani, hivi, Dokta Stegen anajaribu kutueleza ya kwamba tuumbe makala yenye faida na si kuandikaandika miaka tu bila maana. Nimekuelewa uzuri kabisa!--MwanaharakatiLonga 15:06, 15 Februari 2016 (UTC)[jibu]
Mtoto ni mtoto, acha akue! Mwenyewe ataona kuna kazi nzuri kuliko hizo za kiroboti... Umeona mwenzake Daren Jox ameshaanza kuingiza picha na maneno mbalimbali? Tuwape muda. Muhimu wasiharibu. Kama kazi ni za bure, hata Wikipedia nyingine zinazo. Pia hizi fremu zinaandaa na kukaribisha michango, kama tunapoweka viungo kuelekea kurasa ambazo hazipo. Yeyote atakayependa kuingiza habari za miaka hiyo KK watakuta fremu iko tayari, wasihitaji kwenda kutafuta kwenye wiki nyingine, kunakili na kubandika. Kuhusu kujibu, nitamuambia, lakini katika hilo pia tuelewe kwake ni kazi mpya. Naomba tusianze vita bure! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:31, 17 Februari 2016 (UTC)[jibu]
Haya, asante, mzee. Nitamwacha. Wewe ni mwalimu wake. Nisimkatishe tamaa mwanafunzi wako. Kweli tusiwe na vita! Wako katika kuendeleza elimu mtandaoni, --Baba Tabita (majadiliano) 09:09, 17 Februari 2016 (UTC)[jibu]

NAOMBA MSAADA WA NAMNA YA KUWEKA PICHA[hariri chanzo]

Asante sana. Lakini pia napata shida kuweka picha. picha zinapatikana katika wikipedia ya Kiingereza. nawezaje kuzitumia pia katika kurasa zangu? --JERRYN159

Fungua makala penye picha unayopenda kwa kugonga "Edit source". Sasa utaona sehemu ya picha. Picha inafungwa katika mabano mraba [[,,,,]]
Kwa mfano: [[File:Poland1939 GermanPlanMap.jpg|thumb|Map showing the deployment and planned advances ..(text)...]]
Sasa unanakili sehemu yote pamoja na mabano mraba "[[ ...]]" na kuibandika katika makala ya Kiswahili mahali unapotaka.
Hatua zinazofuata ni
a) unafuta matini ya kiingereza kuanzia mstari baada ya neno "thumb|" yaani thumb|Map showing the deployment and planned advances ..(text)...]]
b) sasa unaweka badala yake matini ya Kiswahili, kwa mfano: thumb|Ramani inayoonyesha mpangilio na mipango ya kusogea ...]]
c) sasa bofya "onyesha hakikisho la mabadiliko" na utazame ulichofanya. Kama unakubali gonga "hifadhi ukurasa". Kama hukubali sahihisha na kuangalia tena hadi unaridhika.
d) ukiridhika bofya "hifadhi ukurasa". Kipala (majadiliano) 01:49, 16 Februari 2016 (UTC)[jibu]

Famouse Ukrainian People or maarufu Kiukreni[hariri chanzo]

Hello Riccardo Riccioni! Sorry for writing in English. I don`t understand Swahili. I ask you to contribute with translation into the Swahili language. Could you or other users of your wikipedia translate some articles, that dedicated for prominent figures in Ukraine. The list shown on the page Wikipedia:Makala zilizoombwa. It is equipped interlanguage links and given pronunciation on Latin alphabet.--Yasnodark (majadiliano) 11:36, 10 Aprili 2016 (UTC)[jibu]

Askofu Isuja[hariri chanzo]

Ndugu Riccardo, naona kwamba umeweka siku ya leo kama tarehe ya kufariki kwa Askofu Isuja. Nimesikitika sana kusikia hivyo. Habari hiyo imetokea wapi? Asante kwa kazi yako yote kwa ajili ya wikipedia yetu. Wako katika kujenga elimu, --Baba Tabita (majadiliano) 17:53, 13 Aprili 2016 (UTC)[jibu]

Ndugu, habari ni ya kweli: alifariki katika hospitali ya Itigi. Habari niliipata kwanza kwa mwalimu wetu aliyepewa kipaimara na marehemu, halafu nimeikuta tayari katika ukurasa wa Wikipedia juu ya Isuja. Baadaye kwa wengine pia. Apumzike kwa amani. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:11, 14 Aprili 2016 (UTC)[jibu]
Asante kwa kunijulisha. Lugha yake ya mama, yaani lugha ya Kirangi, nimeifanyia kazi tangu 1996. Warangi watamkumbuka sana. Apelekwe mahali penye raha ili apumzike kutoka kazi zake zote. --Baba Tabita (majadiliano) 20:24, 14 Aprili 2016 (UTC)[jibu]

Mto Kongo[hariri chanzo]

Salaam uliingiza masahishi katika makala wakati bado nahariri. Ili kuokoa nyongeza zangu nilipaswa kuhifadhi upya na mabadiliko yako sasa yamepotea. Pole. Kipala (majadiliano) 10:06, 1 Mei 2016 (UTC)[jibu]

Vandalism[hariri chanzo]

Hi. I noticed a user that is vandalising pages, including your user page. You are one of the local admins that is active here, so let me know if you want some help with this user, of if you prefer to handle it yourself. -- Tegel (majadiliano) 10:46, 1 Mei 2016 (UTC)[jibu]

Salaam ilhali mimi ni mdhaifu sana katika mambo ya hisabati naomba kama uwezekano upo umwonyeshe mwalimu wa hisabati ukurasa huu logi (labda umpe ukiuchapisha) na kumwuliza kama chaguo ya maneno ni sahihi, kama maelezo hadi hapo ni sahihi na labda pia kama inaweza kusaidia, au ni nini iliyokosewa au kukosekana. Kipala (majadiliano) 18:50, 1 Mei 2016 (UTC)[jibu]

msaada tafadhali[hariri chanzo]

Please write here question in english language why me blocked in russian wikipedia, then wikipedia talk and then wikimail (they not understood what happened and just blocked everywhere) this very easy write (likely me block and in kiswahili wikipedia). CYl7EPTEMA777 (majadiliano) 08:12, 9 Mei 2016 (UTC)[jibu]

Unisamehe mzee wangu[hariri chanzo]

Salaam tele kutoka mjini, Dar es Salaam. Ninaomba unisamehe mzee wangu kwa kutoweka jamii au kuumba jamii ambazo ninaziweka. Nimeona mara kadhaa umeingia kila mahali na kuweka jamii husika. Siku mingi sijaja humu vilevile furaha yangu kuona nyendo zangu kuna wakubwa wanaangalia! Ubarikiwe sana. Wako, --MwanaharakatiLonga 07:40, 14 Mei 2016 (UTC) [jibu]

Tunakuhitaji sana, hivyo tunafurahi kukusoma tena. Amani kwenu! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:51, 14 Mei 2016 (UTC)[jibu]

msaada tafadhali[hariri chanzo]

Please write here (this talk user page) question in english language why me blocked in russian wikipedia, then wikipedia talk and then wikimail (they not understood what happened and just blocked everywhere) this very easy write (likely me block and in kiswahili wikipedia). CYl7EPTEMA777 (majadiliano) 22:11, 17 Mei 2016 (UTC)[jibu]

Grazie mille[hariri chanzo]

Carissimo Riccardo, grazie mille per il tuo aiuto. Sai, quest'estate, ero a Pesaro il 24 agosto, e sono stato svegliato all'alba dal terremoto. Il mio letto ha tremato per 30 secondi come una barca!!! Che paura!!!

Ma sono ancora qui, e devo pregare per tutti quelli che non ci sono più.

Grazie ancora per l'aiuto e a presto!!!

Rei Momo (majadiliano) 22:27, 8 Septemba 2016 (UTC)[jibu]

Com'è piccolo il mondo, mons. Borromeo era lodigiano come me ed è stato vescovo di Pesaro, e il mio parroco, abito a Caselle Landi, ha il papà di Montalto! Pace anche a te, fratello! Rei Momo (majadiliano) 13:42, 9 Septemba 2016 (UTC)[jibu]
Yaaaaahhhhhh, mi bastava qualcuno che mi desse il la. Non credo di riuescire a farle tutte, ma comincio subito!!! Rei Momo (majadiliano) 14:27, 10 Septemba 2016 (UTC)[jibu]

Fattoooooo!!! Per favore, mi tradurrest le 4-5 parole che ho inserito in questa pagina? Grazie mille per il tuo aiuto prezioso!!!

Rei Momo (majadiliano) 14:48, 10 Septemba 2016 (UTC)[jibu]

(eccetto 3), cioè le 2 diocesi e l'abbazia che seguono il rito bizantino. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:12, 10 Septemba 2016 (UTC)[jibu]
Grazie per l'aiuto, ma non capisco cosa vuoi dire con eccetto 3. Rei Momo (majadiliano) 15:16, 10 Septemba 2016 (UTC)[jibu]
era quello che avevo aggiunto io. La traduzione delle tue parole la trovi in Jimbo kuu la Pesaro. Buona Domenica! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:19, 10 Septemba 2016 (UTC)[jibu]

Caro Riccardo, Pace!

Qui, nella Bassa Padana, si muore di caldo, a Caselle Landi ci sono ancora 35°C!!!

Ho aperto queste due nuove pagine, e ti chiedo qualche minuto del tuo tempo, per favore, per vedere se ci sia qualcosa da limare. Grazie mille per l'aiuto prezioso!

Rei Momo (majadiliano) 15:39, 11 Septemba 2016 (UTC)[jibu]

Grazie ancora e pace a te, em comunhão! Rei Momo (majadiliano) 21:27, 12 Septemba 2016 (UTC)[jibu]

How to improve Swahili-wikipedia?[hariri chanzo]

I dont speak Swahili, sorry, but I wrote a little piece on Donald Trump anyway, using google translation. Its good if you can check and improve. He is the newly elected American president, as you know. Also, if you can check Astrid Lindgren it would be good. She is a very famous author of childrens books, known worldwide for her stories. See English wikipedia etc. Another thing I have thought about is that all the African wikipedia-versions are very undeveloped. Including swahili, although its a quite big language. I would like to get in touch with people with whome I can talk (in English) about this, and strategies for improvement. One thing that I have thought about is that there should be some people in Tanzania, Kenya and Uganda that are paid to have courses on wikipedia. For example in local groups at home, or in schools. What do you think? --Mats33 (majadiliano) 16:59, 11 Novemba 2016 (UTC)[jibu]

Speaking of improving Swahili Wikipedia, are you for real? Or you've just wrote so Riccardo could have the Trump's article cleared out?--MwanaharakatiLonga 07:36, 12 Novemba 2016 (UTC)[jibu]
Hi Mats33, kindly describe where your interest in sw:wiki comes from. Where are you active and visible on wikimedia? Kipala (majadiliano) 12:09, 12 Novemba 2016 (UTC)[jibu]

Warsha, ombi la makala[hariri chanzo]

Salaam, nitashukuru ukioata nafasi kumwuliza mwalimu wa chuo kama aliona email yangu. Sijapata jibu tangu kuandika wiki 2 sasa.

Halafu ombi: Tunahitaji makala za jando na unyago. Naomba usaidie. Kipala (majadiliano) 21:03, 17 Novemba 2016 (UTC)[jibu]

Mnaijeria wa chuo alikuwa anasubiri e-mail yako. Halafu akatuma watu kuniulizia. Niliposikia hivyo, nilimtumia ujumbe kwamba mimi nilipata nakala, halafu nikamtumia. Sijajua kama sasa ameipata au alikosea kunipa anwani yake. Kuhusu makala hizo, nitajaribu. Shalom! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:14, 18 Novemba 2016 (UTC)[jibu]

Asking to a permission/advice/review[hariri chanzo]

Hi. I have a question. I would like to translate some articles to Swahili (mostly about computer science). But I don't speak Swahili. So, I've found the non-native Swahili speaker, making translations for money. But since I don't speak Swahili at all, I can't rate these translations by myself. The examples may be found on my page. Is the quality of the articles satisfactory? Should I place such articles to the public categories? Or should I place them in the sandbox or somewhere for review? Or the translations are just bad, and I search another translator? (Repost from Majadiliano ya mtumiaji:Malangali) --DoctorXI (majadiliano) 12:32, 22 Desemba 2016 (UTC)[jibu]

Could you, please, recommend a good translator from English? For example, for $18 per 1800 characters (1 page). --DoctorXI (majadiliano) 14:23, 23 Desemba 2016 (UTC)[jibu]

Translation[hariri chanzo]

Hello, could you please translate Automatic refresh (Aggiornamento automatico) to Kiswahili? Thanks -XQV- (majadiliano) 20:07, 13 Januari 2017 (UTC)[jibu]

Where is it? --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:11, 14 Januari 2017 (UTC)[jibu]
It's not an article. I just need the sentence translated. -XQV- (majadiliano) 11:46, 14 Januari 2017 (UTC)[jibu]
I don't know the approved translation. I would try "upyaisho wa kujichipua", but it is very enigmatic! Let you ask somebody other. Thank you! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:01, 15 Januari 2017 (UTC)[jibu]

Share your experience and feedback as a Wikimedian in this global survey[hariri chanzo]

Kura kuhusu wikisource[hariri chanzo]

Salaam kuna Pendekezo: Tuanzishe kitengo cha WikiSource NDANI ya wikipedia yetu unaombwa kuiangalia na kupiga kura! Kipala (majadiliano) 02:06, 29 Januari 2017 (UTC)[jibu]

Matumizi ya namba[hariri chanzo]

Ndg. Riccardo, salaam. Je, ungeweza kumwelezea mwanafunzi wako Macdonaln Aloyce Fute jinsi ya kurejea makala za namba kwa makala za miaka? Tena mambo ya namba tasa nilivyofanya kwa namba kuanzia 540 hadi 556. Nitashukuru sana! Wasalaam, --Baba Tabita (majadiliano) 09:45, 30 Januari 2017 (UTC)[jibu]

Kazi ya miaka ni rahisi, ila kuhusu namba tasa sidhani ataweza... Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:29, 31 Januari 2017 (UTC)[jibu]
Asante! Hata akifanyia kazi miaka tu, itakuwa msaada mkubwa. Nami nitaendelea na namba tasa. ... Amani na iwe kwenu pia! --Baba Tabita (majadiliano) 15:41, 31 Januari 2017 (UTC)[jibu]

Neptuni / Kausi[hariri chanzo]

Salaam, naona umehamisha makala ya Neptun kwenda "Kausi". Ukisoma Majadiliano:Sayari utaona ya kwamba naona sababu za kuamini hili ni kosa. Sijakuta ushuhuda wowote ya kwamba kuna jina la "Kausi" kwa ajili ya sayari hii. Kwa bahati mbaya kosa lililotokea wakati wa kutunga orosha ya sayari kwa KAST limeenea hadi vitabu kadhaa vya shule ya msingi. Naona "Kausi" ni kosa lakini je tufanyeje?? Kipala (majadiliano) 20:21, 12 Februari 2017 (UTC)[jibu]

Miezi iliyopita nilipendekeza badiliko hilo baada ya kuona kamusi 2-3 za mwisho, ikiwemo KKK, zimepitisha jina Kausi. Kwa kuwa hakuna aliyepinga, nimechukua hatua ya kuunganisha kurasa mbili katika jina jipya ambalo linazidi kuzoeleka. Kinachobaki ni kutafiti limetoka wapi... --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:04, 13 Februari 2017 (UTC)[jibu]
Samahani pendekezo hili sijaona. Umeleta wapi? Mimi nakumbuka tu majadiliano hapa Majadiliano:Neptun, ilhali Neptune hapakuwa na majadiliano. Pia nikiangalia "Kausi" katika Kamusi Kuu ya Kiswahili, maelezo yake ni wazi si Neptuni. "Kausi - aina ya nyota ambayo hutumiwa na waganga wa kienyeji kupigia ramli, bao". Maanake hii "Kausi" (bado nimetafuta asili ya neno katika kamusi zangu) ilijulikana kwa wazee lakini Neptuni haikujulikana maana haionekani bila mitambo kwa hiyo haina matumizi katika mapokea na shughuli za waganga wa kienyeji. Kipala (majadiliano) 20:52, 13 Februari 2017 (UTC)[jibu]
Kumbe nimepata mwanga! Kausi inatokana na Kiarabu القوس al-qaus inamaanisha upinde yaani zodiaki inayoitwa kwako nyumbani sagittario. Narejea makala ya Knappert, AL-NUDJUM katika THE ENCYCLOPAEDIA OF ISLAM, LEIDEN BRILL 1997, VOLUME VIII NED — SAM, uk 105. nukuu hapo:
"Swahili astrologers concentrate first and foremost on the signs of the Zodiac, Buruji za Falaki, whose names are all from Arabic: Hamali, Aries - Mizani, Libra - Thauri, Taurus - Akarabu, Scorpio - Jauza, Gemini - Kausi, Sagittarius - Saratani, Cancer - Jadi, Capricornis - Asadi, Leo - Dalu, Aquarius - Sumbula, Virgo - Hutu, Pisces
... The Swahili names of the Planets are: Mercury, Utaridi; Venus, Zuhura; Mars, Mirihi; Jupiter, Mushitari; and Saturn, Zohali."
Naona kitabu cha rejeleo kuu ni J. Knappert, List of names for stars and constellations, in Swahili, xxxv/1 (Dar es Salaam, March 1965) . Basi nitajarib kuipata. Sasa naelewa jinsi gani sehemu ya orodha ya sayari zimepata majina kama Sumbula au Saratani: zimetungwa na watu ambao ama walisikia au kusoma majina ya zodiaki na kuyatumia kwa sayari kwa kukamilisha oeodha - bila kujua wanachofanya. Je tunaweza kusema swali la Kausi limepata jibu?Kipala (majadiliano) 23:53, 13 Februari 2017 (UTC)[jibu]
Kwa rejeo lako, NGUMU kusema jibu limepatikana!--MwanaharakatiLonga 07:46, 14 Februari 2017 (UTC)[jibu]
Napata picha ya uhakika sasa: Kausi ni jina la "buruji ya falaki" (kwa lugha ya Waswahili asilia wenyewe) yaani kundinyota za zodiaki inayoitwa "sagittarius" kwa Kilatini/Kiingereza. Kwa hiyo ni jina linalojulikana kabisa katika utamaduni wa Waswahili lakini si kwa sayari (ambayo haiwezekani kwa Neptuni). Kama watu wameitumia kwa sayari ya Neptuni ni kosa. Marejeo kwa kujisomea hapa: J Knappert, fungu "In East Africa", makala AL-NUDJUM katika THE ENCYCLOPAEDIA OF ISLAM, LEIDEN BRILL 1997, VOLUME VIII NED — SAM, uk 105

Kipala (majadiliano) 11:20, 14 Februari 2017 (UTC)[jibu]

Your feedback matters: Final reminder to take the global Wikimedia survey[hariri chanzo]

(Sorry to write in English)

WMCon 2017 Berlin[hariri chanzo]

Ndugu, salaam. Nataka kukujulisha tu kwamba nimealikwa kuhudhuria Wikimedia Conference 2017, nami nikajisajili tayari. Sitahudhuria rasmi kwa ajili ya wikipedia yetu bali kama mwanakamati wa LangCom. Wasalaam, --Baba Tabita (majadiliano) 20:58, 4 Machi 2017 (UTC)[jibu]

Ombi la MetaWiki[hariri chanzo]

Salaam, Naomba munichangie msaada wa kukubali ombi langu la kupewa laptop kule Meta-Wiki. Kiungo hiki hapa. Wako,--MwanaharakatiLonga 13:13, 17 Machi 2017 (UTC) [jibu]

Samahani, lakini mimi pia nimeomba: watakubali niunge mkono ombi lako? --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:25, 17 Machi 2017 (UTC)[jibu]
Sijajua. Tumuulize Kipala?--MwanaharakatiLonga 13:37, 17 Machi 2017 (UTC)[jibu]
Badili hii: STATUS weka OPEN badala ya sasa iko DRAFT----MwanaharakatiLonga 13:40, 17 Machi 2017 (UTC)[jibu]

Status

Grazie mille /Asante sana! Gaudio (majadiliano) 20:19, 23 Machi 2017 (UTC)[jibu]

PIRLA CHI LEGGE

Buongiorno Padre Riccardo, spero tutto bene lì da voi, qui abbastanza bene per ora, ringraziando Dio stanno iniziando le belle giornate e mi posso dedicare alla campagna e a Wikipedia. Le scrivo per chiederle una cortesia se può e vuole e ha tempo per me. Grazie al web ho avuto modo di conoscere amici di Uganda, Kenya e Tanzania grazie anche al nostro amato parroco don Apollinaris che è di quelle zone (di Moshi per l'esattezza), e ultimamente sto aggiornando tutte le pagine dei due borghi dove vivo e lavoro e dove ovviamente il sacerdote presta servizio. Mi chiedevo se le andrebbe di ampliare e/o aggiornare le pagine di Coreca eCampora San Giovanni, giusto e non più di 20 minuti del suo prezioso tempo. Oltre a questo, presto o forse in queste ore, un mio amico di Facebook proveniente dal Kenya si iscriverà nella Wikipedia Swahili, su mio suggerimento gli ho detto che lei potrà aiutarlo i primi tempi, bene detto questo spero di avere sue notizie quanto prima, un caro saluto da Coreca e Campora San Giovanni. A presto!--Luigi Salvatore Vadacchino (majadiliano) 06:31, 5 Mei 2017 (UTC)[jibu]

Ushauri kwa vijana[hariri chanzo]

Salaam naomba ukipata nafasi waambie vijana waangalie wanachooweza kuuona kwenye kurasa zao za majidiliano. Pia waangalie tena kurasa walizowahi kuandika. Maana naona wengine wanatunga makala hovyo, hata kuhusu mada ambazo ziko tayari hakuna njia ili kufuta. Mengine ya awali hawaangalii tena. Nilimwandikia DANIEL DE SANTOS maelezo marefu, nahisi hajaona. Wengine tatizo lilelile. Asante Kipala (majadiliano) 14:19, 17 Juni 2017 (UTC)[jibu]

Asante, ndugu. Naendeleza kazi yako. Nikiwa nao, nawaelekeza na kuwaita waone namna ninavyoboresha maandishi yao. Polepole tutafika! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:10, 17 Juni 2017 (UTC)[jibu]
Asante, kweli tutafika! Kipala (majadiliano) 19:53, 17 Juni 2017 (UTC)[jibu]

Ndugu Riccardo salaam,
Baada ya salaam, nikupe pole na kazi nyingi!
Ombi sasa,
Binafsi ningeliweza kuipanua makala hii, lakini naona kama sekta yako.
Bora niheshimu upanuzi wake ufanywe na mtu mqenye maarifa ya juu katika masuala ya dini kuliko kupapachia!
Najua utaiboresha katika viwango vizuri. Isitoshe: una faida za lugha nyingi tu.
Wako,
--MwanaharakatiLonga 05:13, 12 Septemba 2017 (UTC) [jibu]

OK bosi! Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 08:45, 12 Septemba 2017 (UTC)[jibu]
Ebwana eh! Nimekoma nayo! Sio mchezo kabisaaa. Ahsante sana. Yaani, upo fasta balaa! Ubarikiwe mzee wangu. Naona umeniita bosi, hahahaha, sawa bwana! Nimefurahi sana, miaka 10 sasa tuko ote na hujabadili mwendo! Tazama:

2008 = 643
2009 = 1,311
2010 = 728
2011 = 801
2012 = 1,458
2013 = 934
2014 = 2,371
2015 = 3,734
2016= 4,745
2017 = 5,302
Au chungulia haririo zote hapa: kiungo cha kuonesha haririo zako zote.. Ahsante sana kwa kushiriki pamoja kujenga wiki yetu hii!--MwanaharakatiLonga 14:31, 12 Septemba 2017 (UTC) [jibu]

Sikutegemea kuona takwimu hizi zote! Kumbe umenionyesha njia rahisi ya kutathmini kazi yangu. Asante sana kwa kunitia moyo, nami nakuambia nimefurahi kuona wewe pia umekazana tena. Tusirudi nyuma katika kuenzi lugha yetu. Amani kwenu! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:24, 13 Septemba 2017 (UTC)[jibu]
Ahsante sana. Usihofu mzee wangu!--MwanaharakatiLonga 03:49, 17 Septemba 2017 (UTC)[jibu]

Salaam tena, Ushauri wangu, bora tu, utafsiri cha juu hapo ambacho kishakamilika na kimeunga kurasa nyingi! Ushauri tu!--MwanaharakatiLonga 03:46, 17 Septemba 2017 (UTC) [jibu]

Kabisa![hariri chanzo]

Kweli hatimaye. Kabisa ndugu. Tumerudi!! --Ndesanjo (majadiliano) 05:33, 3 Oktoba 2017 (UTC)[jibu]

Annullamento[hariri chanzo]

Prima di annullare andrebbe controllato. Quel quadro é di un anonimo. Si capisce dal titolo, dalla pagina su commons e dal sito ufficiale di palazzo Barberini dove sta. per favore correggi. Pierpao Pierpao (majadiliano) 07:15, 14 Novemba 2017 (UTC)[jibu]

Fatto. Il problema è stato che hai cambiato le parole swahili usando non so quale lingua... sembrava un vandalismo. Comunque grazie di darci una mano. Pace a te! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:22, 14 Novemba 2017 (UTC)[jibu]
Vero, ho scritto in polacco. Grazie e scusa. Ho messo le fonti su Commons.--Pierpao (majadiliano) 08:28, 14 Novemba 2017 (UTC)[jibu]

Interior design[hariri chanzo]

Vipi. Ile makala ya interior design. Je ipi ndio sahihi hasa? Usanifu wa ndani au ubunifu wa ndani. Au kuna neno jingine? --Ndesanjo (majadiliano) 10:42, 14 Novemba 2017 (UTC)[jibu]

Nitaangalia, lakini sidhani "ubunifu wa ndani". Walau usanifu wa ndani unarandana na "usanifu majengo". --Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:53, 15 Novemba 2017 (UTC)[jibu]

Nakala ya Rayvanny[hariri chanzo]

Asante kwa kunisaidia kuikamilisha nakala ya Rayvanny.Boy Addi (majadiliano) 16:23, 29 Novemba 2017 (UTC) Boy Addi (majadiliano) 16:23, 29 Novemba 2017 (UTC)[jibu]

Pitia Kurasa la Tarrus Riley[hariri chanzo]

Tafadhali pitia kurasa mpya niliyo andika na uchangie.Pliz check on my new article Tarrus Riley and make editings and contributions. Boy Addi (majadiliano) 19:43, 30 Novemba 2017 (UTC)[jibu]

Tuna makala ya Wakelti na umbo hili la jina limeshatumiwa mara kadhaa linganisha hapa: Maalum:VingoViungavyoUkurasahuu/Wakelti.

Je ingekuwa vigumu kuhamisha hata makala hii kuwa "Makanisa ya Kikelti"?? 'Kipala (majadiliano) 10:05, 27 Januari 2018 (UTC)[jibu]

Salaam,
Habari za masiku!
Naona si kazi kubwa sana.
Ngoja nikufanyie fasta uone! Ni namna ya kuvuta tu.. Nipe dakika 2 zote zitaisha kwa Argentina. Ila hizo zingine nitahitaji AutoWikiBrowser.. Ngoja nitaza kwanza.--MwanaharakatiLonga 11:44, 8 Februari 2018 (UTC) [jibu]

Riccardo salaam. Niliona makala inayoitwa Fati, nikashangaa. Sijawahi kuona au kusikia neno hili, hapa Kenya hasa. Neno hili hutumika sana kwenu Tanzania? Nikisoma kuhusu chakula ninaona mafuta tu, au pengine shahamu. ChriKo (majadiliano) 17:41, 2 Machi 2018 (UTC)[jibu]

Ndugu, aliyeandika ni mwanafunzi wa kidato cha pili. Hata mimi nilipoona kichwa hicho nilitikisa kichwa nikamuambia lakini sikupenda kumkatisha tamaa. Lakini pia si mara ya kwanza kusikia neno hilo katika mazingira ya shule. Kama unaona neno lingine, hamisha tu. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:10, 3 Machi 2018 (UTC)[jibu]
Asante sana, Riccardo. Nimefahamu sasa. Nitahariri makala hii na nyingine zinazotaja neno hili. ChriKo (majadiliano) 18:52, 3 Machi 2018 (UTC)[jibu]

Asante kwa makala za milima! Je habari zao unapata wapi? Kuna chanzo kinachoweza kutajwa? Kipala (majadiliano) 17:33, 5 Machi 2018 (UTC)[jibu]

Halafu: ukipenda kufuatilia: angalia Jamii "milima ya Tanzania" kwenye cebwiki. Ninavyojua huyu aliyetunga Cebuano ni mtu mmoja to kutoka Uswidi aliyetumia takwimu mbalimbali halafu akatunga makala zote kwa njia ya bot! Ila tu sijaelewa bado ni wapi alipopata data katika yale anayotaja. Linganisha ceb:Bigoro_Hills na Milima_ya_Bigoro. Anatumia http://www.geonames.org/about.html (sijaiujua bado, ina habari nyingi sana! - labda unaweza kuweka wanafunzi wachukue data hapa?) Kipala (majadiliano) 17:49, 5 Machi 2018 (UTC)[jibu]
Ndiyo, natumia wiki ya cebuano, ingawa siijui... Pia mara nyingine kuna makosa au tofauti, lakini basi, nadhani kwa kiasi kikubwa ni sawa. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:06, 6 Machi 2018 (UTC)[jibu]

Huna mpinzani bwana![hariri chanzo]

Salaam tele,
Tunakuunga mkono kiaina, japo siku hizi shughuli zinanichosha kuliko zamani. Ila nitajihidi kufanya kama awali.--MwanaharakatiLonga 20:43, 17 Machi 2018 (UTC) [jibu]

Kupanda mbegu[hariri chanzo]

Salaam,
Ndugu, hakika unanihamasisha kuanza kupanda mbegu. Japo sijui nitapanda mbegu za mti gani.
Naona kama wazo la kuanza kuzipanda linanijia.
Nimekumbuka, nadhani nina kiporo cha Uislamu kwa nchi. Labda niingize idadi tu badala ya maneno mengi? Kuimaliza Afrika ilinichukua mwaka mzima!
Nitajaribu!
Ahsante sana kwa hamasa yako.
--MwanaharakatiLonga 11:06, 2 Aprili 2018 (UTC) [jibu]

Ndiyo ndugu, tupande mbegu. Polepole zitakua. Kweli, upande wa dini, kitu kikubwa ni idadi ya waumini kati ya wakazi wote. Asilimia walau inaleta picha fulani. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:49, 2 Aprili 2018 (UTC)[jibu]
Nitafuata ushauri wako. Shukrani mno!--MwanaharakatiLonga 11:53, 2 Aprili 2018 (UTC)[jibu]

Majimbo ya Sudani[hariri chanzo]

Salaam mzee wangu, Riccardo Riccioni!
Naona unaendeleza kasi yako ileile. Vizuri
Ila kuna jambo kidogo nataka kuuliza. Hivi yale majimbo uliyowekea (mabano) una mpango wa kuunda makala ya kujitegemea?--Muddyb Mwanaharakati Longa 13:53, 15 Aprili 2018 (UTC) [jibu]

Ndugu, asante kwa pongezi! Kuhusu mabano nimeyaweka kwa sababu baadhi ya majimbo yana jina la mji au mto. Hivi nimependa kutofautisha. Labda kwa mengi haikuwa lazima, lakini basi, nimetumia mtindo mmoja kwa yote. Salamu za amani! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:03, 16 Aprili 2018 (UTC)[jibu]

Hongera ya makala 41000[hariri chanzo]

Hongera kwa kutusukuma juu ya 41000!! Kipala (majadiliano) 19:50, 2 Mei 2018 (UTC)[jibu]

Safi sana!--Muddyb Mwanaharakati Longa 08:20, 3 Mei 2018 (UTC)[jibu]

ufahamu zaidi kuhusu neno Qadash na Hagios[hariri chanzo]

Habari ndugu Riccardo Riccioni napenda ufafanuzi zaidi juu yahaya maneno mawili, amboyo ni neno la kiebrania Qadash pamoja na neno la kigiliki Hagios. Ahsante Enock John (majadiliano) 08:54, 7 Mei 2018 (UTC)[jibu]

Carissimo Riccardo, Pace!

Ho visto che hai creato tu questa pagina, tempo fa! Bravissimo! Volevo segnalarti che, da qualche tempo, Gregorio III è patriarca emerito, l'attuale patriarca è Youssef Absi (senza mettere il "I", per favore). Poi, volevo chiederti, se puoi anche aggiungere che l'Arcieparchia di Gerusalemme dei melchiti è retta, attualmente, da mons. Yasser Ayyash. Grazie mille per il tuo prezioso aiuto, a presto.

Rei Momo (majadiliano) 06:30, 15 Juni 2018 (UTC)[jibu]

Categorie duplicate[hariri chanzo]

Ciao! Nel tempo libero mi occupo di sistemare i collegamenti interwiki delle categorie in diverse lingue. Passando di qui ho notato che Jamii:Georgia (nchi) e Jamii:Georgia sembrano essere la stessa categoria: potresti unirle nel modo migliore? Grazie mille e a presto, --Epìdosis (majadiliano) 12:47, 6 Julai 2018 (UTC)[jibu]

Idem: Jamii:Watu wa Wales e Jamii:Watu wa Welisi. Grazie ancora, --Epìdosis (majadiliano) 12:54, 6 Julai 2018 (UTC)[jibu]
E non riesco a capire se Jamii:Wanauchumi (e sottocategorie) siano duplicati di Jamii:Wachumi (e sottocategorie). Scusa per il tempo che ti faccio perdere! --Epìdosis (majadiliano) 13:03, 6 Julai 2018 (UTC)[jibu]
Grazie della collaborazione. Sto provvedendo. Pace a tutti! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:08, 6 Julai 2018 (UTC)[jibu]
Anche Jamii:Malambo e Jamii:Lambo. Grazie a te! --Epìdosis (majadiliano) 13:30, 6 Julai 2018 (UTC)[jibu]

Kuangalia makala ya kufutwa[hariri chanzo]

Salaam, ndugu! Tumeona ya kwamba Oliver anachukua likizo. Sasa tulikuwa na mfumo ya kwamba tunaangaliana katika makala yaliyopendekezwa kwa ufutaji. tulipatana mmoja analeta mapendekezo lakini asifute mwenyewe isipokuwa ni jambo ambalo halina maswali. Menginevyo mwingine aamue. Ilhali Oliver hapatikani kwa muda huu naomba uingie wewe! Tazama hapa: [[1]].- --Kipala (majadiliano) 18:00, 7 Julai 2018 (UTC)[jibu]

Ndiyo, nimeona. Sijui anaumwa nini. Kuhusu ufutaji, mara nyingine nimefuta ukurasa peke yangu, ama kwa sababu ni za wanafunzi wangu ama kwa sababu ilikuwa wazi kwamba hazifai: kichwa na matini yote kwa Kiingereza au Kivietnam! Kuhusu ombi lako, sawa, nitashika nafasi hiyo kwa muda aliosema Oliver. Jumapili njema katika amani ya Mfufuka! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:17, 8 Julai 2018 (UTC)[jibu]

Taasisi ya samaki?[hariri chanzo]

Riccardo salaam. Wakati nilipofanya mabadiliko kwenye sanduku ya samaki, nilijiuliza kama Kiswahili ina istilahi kwa "shoal" au "school of fish". Nikatafuta kwenye kamusi kadhaa. Inaonekana kama neno la kawaida ni kundi, lakini TUKI (English - Swahili) inatoa pia usheha kwa "shoal" na kamusi ya Willy Kirkeby inatafsiri "school of fish" kwa taasisi. Nilishangaa na kwenye Google sikuweza kupata mifano ya maneno haya yakimaanisha "shoal" au "school". Unajua kwamba maneno haya yanatumika kwa maana hii? ChriKo (majadiliano) 11:25, 9 Septemba 2018 (UTC)[jibu]

Kamusi yangu ya ENglish-Swahili inasema "school2 n (of fish) kundi (kubwa la samaki)". Taasisi surely is different, it is an institute where they teach about fish. Kipala (majadiliano) 15:05, 9 Septemba 2018 (UTC)[jibu]
Hata yangu inasema hiyo, lakini angalia kitomeo cha "shoal2": n kundi la samaki, usheha. Kitomea cha "I. school" kwenye Kirkeby: n: of fish or marine animal: taasisi (-). Sijui ameipata wapi? ChriKo (majadiliano) 16:46, 9 Septemba 2018 (UTC)[jibu]
Katika Madan English-Swahili (1903) ninakuta "School (of fish) kundi (ma), wingi". Taasisi itakuwa ni kosa. lakini naweza kuwauliza wavuvi, maana naishi sasa ufukoni moja kwa moja, wako nje. Usheha unawezekana, Kamusi ya Visawe (2008) ina "Usheha: halaiki, umati, unasi, umma, msoa, umayamaya, kaumu, kundi kubwa (la watu)", crosschecking here with "Wingi: halaiki, umati, usheha, umayamaya, unasi, kaumu, jamii, umma, hadhara, ulufu". Basi nadhani unaweza kwenda na Usheha, lakini subiri nitauliza Wavuvi. Kipala (majadiliano) 17:39, 9 Septemba 2018 (UTC)[jibu]
Asante kwa mchanganuo huu. Ndiyo, waulize wavuvi tafadhali. ChriKo (majadiliano) 20:00, 9 Septemba 2018 (UTC)[jibu]

Makala ya afya ya MJ[hariri chanzo]

Salaam, Ndugu Riccardo, nimeona umeunganisha makala ya afya ya Michael Jackson na makala yake nyengine kuhusu maisha, muziki na mambo mengine. Kifupi hizo zilikuwa makala mbili tofauti. Wala haikuwa na haja kuziunganisha. Wikipedia ya Kiingereza ina makala yake maalumu kuhusu afya ya MJ. Nami nikafanya hivyo hapa kwenye Wikipedia ya Kiswahili. Sioni sababu ya kuiunga hata kidogo. Basi unganisheni na makala za albamu, singo na mengineyo. Wikipedia karibia zote wametenga makala ya afya na muziki. Sisi tumechanganya yote mahali pamoja. Mkanyanyiko mtupu.--Muddyb Mwanaharakati Longa 07:19, 7 Oktoba 2018 (UTC) [jibu]

Pole kwa kukuchukiza! Siku zile nilijaribu kuweka sawa makala zenye mashaka kwa kufuata mapendekezo yaliyokuwepo, mojawapo la kuuunganisha hizo mbili za MJ. Kama unapenda kuzitenganisha tena, mimi sina shida. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:30, 7 Oktoba 2018 (UTC)[jibu]

Mkabidhi mpya. pendekezo[hariri chanzo]

Naomba angalia hapa Wikipedia:Jumuia#Mkabidhi_kwa_Jadnapac (Halafu: Je unaona nafasi kuja Dar mwisho wa Novemba kwa warsha ya Astronomia, Ijumaa- Jmosi?). Kipala (majadiliano) 21:39, 30 Oktoba 2018 (UTC)[jibu]

Si rahisi. Labda kwa ajili yako nikijua mapema tarehe. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:00, 31 Oktoba 2018 (UTC)[jibu]

Vyanzo, Kenya[hariri chanzo]

Salaam naona umeanza kushughulika miji ya Kenya, asante! Ila tu unatumia namba bila kutaja vyanzo. Ni vema ukiweza kukumbuka. Kwa vyote vya Kenya nimetengeneza tanbihi ifuatayo inayoweza kuwekwa: <ref>[https://www.knbs.or.ke/download/volume-1a-population-distribution-by-administrative-units-2/?wpdmdl=3765 Sensa ya Kenya 2009], tovuti ya [[KNBS]], ilitazamiwa Januari 2009</ref>

Kipala (majadiliano) 18:28, 7 Januari 2019 (UTC)[jibu]

Document your culture with Wiki Loves Love 2019 and win exciting prizes![hariri chanzo]

Please help translate to your language

Africa has many beautiful festivals, ceremonies and celebrations of love and we need your help to document these! They are the core part of African culture and in order to make sure this way of life followed by our ancestors remain among us, we need to have them online to make sure they are preserved. Join hands with Wiki Loves Love that aims to document and spread how love is expressed in all cultures via different rituals, celebrations and festivals and have a chance to win exciting prizes!! While uploading, please add your country code in the Wikimedia Commons upload wizard. If you want to organize an on-site Wiki Loves Love event, then contact our international team! For more information, check out our project page on Wikimedia Commons.

There are several prizes to grab. Hope to see you spreading love this February with Wiki Loves Love!

Imagine...The sum of all love!

Wiki Loves Love team 07:34, 4 Februari 2019 (UTC)

Continental shelf[hariri chanzo]

Salaam, tuna majadiliano kuhusu "tako la bara". Muddy haipendi, ChriKo ana mawazo. Je unaweza kuwauliza alimu wa jiografia kama wanajua Kiswahili cha continental shelf, na wangependelea nini? Nilianza makala kwa kutumia "tako la bara" (sikumbuki kam niliikuta au niliitunga kwa jaribio la kutafsiri), sasa nilikuta matumizi ya "kitako" kwa "msingi, chanzo, kiti cha kitu", na chriko alipendendekeza "mwambao wa bara" (ambayo mim sidhani inafaa). naomba jaribu kuwauliza. Kipala (majadiliano) 07:59, 6 Februari 2019 (UTC)[jibu]

Asante, mchango wako kuhusu tako la bahari naona sasa tu maana ulichangia mahali ambako sikutegemea. Kuhusu visiwa nilianza lakini sasa nasita kwa kwa sababu nilitambua sikutafakari vema labda tushauriane tena (na toba yangu kurudia kila kitu..). tatizo ninaloona tukiwa na vitu vingi katika jamii moja hatuna budi kuvipnga kwa vikundi vidogo. Kwa hiyo ni nilianza jamii:Visiwa vya Ziwa Viktoria (inayounganishwa katika Jamii:Ziwa Viktoria na pia Jamii:Visiwa vya Tanzania) nikaona naweza kufuta mengine. Mpaka kuona ya kwamba tukiendelea na visiwa vya ziwa tutapata pia visiwa vya Kenya na Uganda, kumbe sikufikiri adi mwisho. Subiri, nirudi nyumbani (niko kwenye kikao cha kuchosha) na kutafakari upya.--Kipala (majadiliano) 12:51, 10 Februari 2019 (UTC)[jibu]

Naona umebandika pendekezo la kufuta kwa makala mbalimbali. Ila tu usipopeleka jina kwenye ukurasa wa Wikipedia:Makala_kwa_ufutaji zitabaki tu maana maana si rahisi kuzitambua. Baada ya kuweka tangazo {{futa}} unaweza kubofya ile "hapa" ya buluu na kuandikisha makala mle kama sehemu mpya. Kipala (majadiliano) 07:17, 19 Februari 2019 (UTC)[jibu]

Ndiyo, najua utaratibu huo, ila ukiangalia utakuta kurasa nyingi ambazo zinaweza kufutwa. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 08:44, 19 Februari 2019 (UTC)[jibu]

Monte San Valentín[hariri chanzo]

Ehi ciao, sei Italiano? Ho visto che hai spostato la pagina "Cerro San Valentin" a "Monte San Valentin", ma la grafia corretta in spagnolo è "Monte San Valentín", con l'accento acuto. Potresti spostarla tu per piacere?

Ehm... Ma se parli Italiano perché non rispondi? Lo spostamento della pagina non riguardava la parola "Monte" ma l'accento su "Valentín", quindi chiamalo pure "Cerro", "Monte", "Mlima" o come ti pare, l'importante è aggiungerci l'accento acuto per rendere l'ortografia spagnola corretta. Grazie!

Sì, ero italiano. Non ti ho risposto perché tu non hai firmato. Devi sapere che il Kiswahili non ha accenti nello scritto, quindi diventa quasi impossibile cercare la pagina con l'í. Però ho messo l'accento nel testo, dove è indicato il nome in Spagnolo. Penso che basti. Pace a te! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:58, 1 Machi 2019 (UTC)[jibu]

Ho capito. Be', non voglio intromettermi nelle scelte di questa versione di Wikipedia perciò non insisterò, però non è un discorso di caratteri e diacritici esistenti in Swahili, perché si tratta di un nome straniero che viene scritto come nella lingua originale. In tutte le altre lingue di Wikipedia questa pagina ha l'accento, anche in quelle in cui l'accento non esiste, tipo il Polacco ma anche l'Esperanto che è una lingua artificiale. Su questa enciclopedia ho trovato per esempio la pagina su "Édith Piaf" scritto con l'accento, così come in quella italiana ci sono quelle su "Anders Ångström" o "Karol Wojtyła". Se preferisci non lasciare diacritici per questa particolare pagina come ho detto non insisterò a convincerti a farlo, ma sarebbe un'eccezione ingiustificata sia fra le altri wiki per questa voce sia fra le altre voci in questa wiki. Grazie comunque per avermi dato una risposta educata e civile, non tutti lo fanno qua dentro. Pace a te :-) --151.48.68.205 (majadiliano) 19:59, 7 Machi 2019 (UTC)[jibu]

Jambo, Mimi ni mpya kwa Wikipedia.Nahitaji msaada tafadhali.Niliandika makala ya Kiswahili na napenda unisome na kunisaidia kurekebisha. Asante.

Jambo mojawapo ni kwamba ukituma meseji kama hiyo ongeza saini yako mwishoni kwa kubofya hapo juu alama ya tatu ili itokee kama kwangu hapa. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:12, 28 Machi 2019 (UTC)[jibu]

Asante kaka Riccioni kwa kugundua mchango nilioifanya katika eneo bunge la Limuru. Kwa swala la kuongeza data katika majimbo na maeneo bunge ya huku Kenya, nitafanya jitihada ya kuhariri. Mimi bado ni mwanafunzi wa Shule Ya Upili Anestar, Lanet-Nakuru , Kidato cha 3 na kwa sababu tumekuja likizo ya wiki nne nitakuwa huku mara kwa mara. Huku twasema zote, lakini hutegemea. Maeneo bunge ni tofauti na majimbo huku. Majimbo ni kama Nakuru,Mandera,Narok,West Pokot ambayo ni 47 na eneo bunge ni kama Kabete,Limuru, Malindi, Lanet na mengine ambazo ni 290.

Kunradhi kwa kurudisha ujumbe wako baada wa muda mrefu 😁.

Peace man --RazorTheDJ (majadiliano) 15:28, 6 Aprili 2019 (UTC)[jibu]

Asante pia kwa kuchangia pakubwa kwa ukuaji wa Swahili Wikipedia. Bila nyinyi, Wikipedia haingekuwa ilivyo sasa. Tutakapo shikilia usukani siku zijazo, tutafanya hata makubwa zaidi.

Nina swali, mtakuwa na warsha ya Swahili Wikipedia siku gani? Nitafurahi sana kukiwa nayo, nitafanya juu chini kuhudhuria. Sarufi yangu inaweza kuathiriwa na sheng kidogo lakini nitakuwa mwanaisimu kama wewe 😁 Kuwa na siku yenye fanaka. Salamu nyingi kutoka kwa mamangu huku Nairobi,Kenya --RazorTheDJ (majadiliano) 07:29, 7 Aprili 2019 (UTC)[jibu]

Kweli tunatumaini mtashika usukani na kufanya makubwa kuliko sisi. Kuhusu warsha, hatujapanga, lakini utajua tu. Amani kwako na kwa mama! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:16, 11 Aprili 2019 (UTC)[jibu]

Uliniuliza kwa nini nilibadilisha. Kwa kweli sijui wala sikumbuki. Nikiitazama siwezi kuwaza mabadiliko yana kusudi gani. Hata nina mashaka kama ni kweli mabadiliko yangu, lakini siwezi kuwaza jinsi gani mwingine aliweza kuhariri kwa jina langu. Kama kosa langu, basi nisamehe. Nimeirudisha jinsi ulivyoiacha. Asante kwa kuuliza. Kipala (majadiliano) 10:49, 12 Aprili 2019 (UTC)[jibu]

Tarafa ya Abengourou[hariri chanzo]

Hello Ndugu Riccardo, Thank you very much for your kind works on the stubs i am currently proposing about Côte d'Ivoire. Could you, please, correct this draft concerning the departments of Côte d'Ivoire, before its possible publication ? Thanks in advance. --Zenman [Majadiliano] 10:45, 8 Mei 2019 (UTC)[jibu]

Please, don't use "vikoa" but "kata". Moreover, try to link to other Wikis. Thank you again! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:39, 9 Mei 2019 (UTC)[jibu]
Again, thanks a lot for your corrections and advices. On the current Ivorian territorial division, we have the following situation:
  • 14 districts (Wilaya)
  • 31 Regions (Mikoa)
  • 108 Departments (Tarafa)
  • 510 Sub-prefectures (Kata)
I'am about to create the articles of the 14 Districts (Wilaya) and up-to-date the 108 departments (Tarafa). However, this requires that current articles on departments (also named here Wilaya) be renamed as Tarafa.
Am I allowed to do it? --Zenman [Majadiliano] 10:16, 10 Mei 2019 (UTC)[jibu]
The only problem is that in Tanzania and many other countries the districts are subdivision of Region, not the contrary. This is way the departments were called Wilaya. But we have to accept the Ivorian terminology. So, go on. Peace to you! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:01, 10 Mei 2019 (UTC)[jibu]

Ciao caro, come stai? Quì abbiamo avuto un maggio completamente piovoso, adesso, forse si starà meglio!

Per favore, noto che in questa città c'è il seminario maggiore, magari può servire nella pagina, me lo aggiungeresti, tu, per favore? Grazie mille, un caro saluto, in comunione!

Rei Momo (majadiliano) 09:38, 2 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Ehilààààà, più veloce della luce. Grazie mille!!! Hai una mail? Il mio sito è reimomo.it Rei Momo (majadiliano) 09:53, 2 Juni 2019 (UTC)[jibu]
Sono qua in computer room con un po' di studenti della nostra secondaria; cerco di appassionarli a Wikipedia in Swahili... Oggi la Messa sarà di sera. Il mio indirizzo e-mail è: ndugurikardo@yahoo.it. Pace e bene alla vostra repubblica! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:58, 2 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Wanafunzi?[hariri chanzo]

Ndugu, kuna watu wanafanya warsha ya kuandika kwenye Wikipedia? Naona kuna makala nikadhani labda ni wanafunzi wanajarijaribu hivi.--Ndesanjo (majadiliano) 13:05, 9 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Ndiyo, ni wanafunzi wa Alfagems Morogoro. Niko nao. Wengine wameshapiga hatua, wengine bado. Ndio kesho ya Wikipedia yetu. Wakikosea, narekebisha. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:06, 9 Juni 2019 (UTC)[jibu]
Ni vizuri nimeuliza. Nilishangaa kidogo. Nilifuta moja ya mwanafilamu Kanumba baadaye ninaona makala nyingine na majina mapya zinajitokea. Nikaona si kawaida, ngoja niulize. Hongereni. Ni vizuri sana. Tutawaidia. Wape salamu. Kweli hawa ndio wahahari wa kesho. --Ndesanjo (majadiliano) 13:14, 9 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Shikamoo Baba,

I'm again coming back to ask your help. Would you, please, have a look at these two drafts (SLM2 ; SLM3) that could serve as models for other articles to create? Asante sana. --Zenman [Majadiliano] 11:48, 10 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Merci beaucoup pour vos contributions. Je voudre entendre le significance de "Imara" dans le box. Paix à tous! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:21, 10 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Merci beaucoup pour vos corrections et conseils. J'ai supprimé le "Imara" dans l'infobox. Asante sana. --Zenman [Majadiliano] 23:09, 12 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Administrative division of Côte d'Ivoire[hariri chanzo]

Hello Riccardo Riccioni, Can you, please, give your opinion on this question? Thanks in advance. --Zenman [Majadiliano] 18:45, 21 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Cellulitis[hariri chanzo]

Eti ugonjwa wa Cellulitis kwa Kiswahili ni nini?--Ndesanjo (majadiliano) 08:53, 27 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Kamusi ya tiba: " cellulitis n selulitisi: inflamesheni ya tishu areola (tishu unganishi)". Binafsi simpendi sana huyu aliyetunga kamusi hii maana alikuwa mvivu kiasi, akitumia kimsingi maneno ya Kilatini tu na kuyaswahilisha kidogo mwishoni. Ila tu hatuna nyingine kwa hiyo twende naye. Ndesanjo: tafadhali andikisha email yako hapa, nitakutumia kmusi hii Kipala (majadiliano) 21:55, 27 Juni 2019 (UTC)[jibu]
Asante Kipala kwa kujibu kwa niaba yangu. Bila kuangalia kamusi hiyo ya kivivu nilikuwa nafikiria kutohoa "selulaiti". Amani kwenu! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 06:44, 28 Juni 2019 (UTC)[jibu]
Samahani kwa kukanyaga shamba lako! Nilipoona swali la Ndesanjo kwenye "mabadiliko ya karibuni" nilikuwa nimefungua kamusi ile, badi nilikuwa mbioni... Kipala (majadiliano) 16:43, 28 Juni 2019 (UTC)[jibu]
Hakuna shida kabisa. Hapa tunasaidiana. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:58, 29 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Barua pepe yangu[hariri chanzo]

Riccardo salaam. Umeona barua pepe niliyokutuma hivi karibuni? Ningependa kupata maoni yako juu ya majina ya wadudu wale. Asante. ChriKo (majadiliano) 15:52, 28 Juni 2019 (UTC)[jibu]

Majibu niliyopata kwa sasa ni haya:
  • Aphid = Kidukari
  • Cricket = Nyenje
  • Fire ant = Majimoto
  • Moth = Nondo
  • Bumblebee = Nyukibambi
  • Bird grasshopper = Parare
  • Palm weevil = Sururu
  • Sand flea = Tekenya
  • Mealybug = Kidung'ata
  • White fly = Nzi Mweupe

Kazi njema na amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:16, 10 Julai 2019 (UTC)[jibu]

Asante sana. Natumaini nitapata majina mengine tena. Hawajui majina ya "true bug" na "cicada"? Amani kwako. ChriKo (majadiliano) 15:48, 10 Julai 2019 (UTC)[jibu]
Jana mwalimu aliniuliza kuhusu 'cicada'. Nikamueleza kidogo kwa sababu hata Italia yupo (anaitwa cicala), na Watanzania wengine wanamfahamu, ila majina wanayotumia ni tofauti. Baadhi wanamuita "nyenje" jina ambalo hapa juu limetumika kwa Cricket na wengine tena wanalitumia kwa Mende... Tutaendelea na utafiti. Amani kwa wote! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:03, 11 Julai 2019 (UTC)[jibu]
Kwa kuendelea kuuliza kuhusu Cicada, nimejibiwa kuwa jina lake ni Nyenje, Nyenze au Chenene. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:43, 20 Julai 2019 (UTC)[jibu]
Asante sana kwa juhudi zako. Ndiyo, hata mimi nilipata majina haya. Inaonekana kama watu wanachanganya wadudu hao kwa sababu wanapiga kelele iliyo takriban sawa. ChriKo (majadiliano) 19:48, 27 Julai 2019 (UTC)[jibu]
Riccardo salaam. Ninarudi kwako ili kukuuliza mara nyingine tena kwamba jina "kunguni-mgunda" linaweza kutumiwa kutafsiri "true bugs". Walimu hawa hawana maoni kuhusu jina hili? Amani kwako. ChriKo (majadiliano) 15:04, 7 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]
Ndugu, nimemuuliza mwalimu mmoja. Ameridhika na jina hilo. Hongera na amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 08:48, 8 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]
Asante sana. Nimeshatoa ukurasa wa oda Hemiptera (Mdudu Mabawa-nusu). ChriKo (majadiliano) 15:28, 8 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]

spam links[hariri chanzo]

Hi Riccardo! I removed some additional spam links by one of the accounts we talked about last week here. However I noticed many times when he spammed a url he wrote the link direct in english (ie. instead of [www.google.com mbwa], they wrote [www.google.com dog]. Would you mind taking a look and translating the actual words where I removed the bad spam links? Thanks! Praxidicae (majadiliano) 14:39, 10 Julai 2019 (UTC)[jibu]

Thank you per your work. As I wrote, I do what I can. OK, I'll try doing what you said too. Peace to you! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:08, 11 Julai 2019 (UTC)[jibu]

Kiswahili poaǃ[hariri chanzo]

Ndugu naona Kiswahili changu kinanitoka kidogoǃ Hahaha. Asante kwa masahihisho yako. Kweli lugha umeipata kabisa. --Ndesanjo (majadiliano) 08:12, 18 Julai 2019 (UTC)[jibu]

Haika mbe! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:34, 18 Julai 2019 (UTC)[jibu]

Hello there[hariri chanzo]

Are you doing good Kitereza (majadiliano) 19:34, 20 Agosti 2019 (UTC)[jibu]

templates[hariri chanzo]

Hey, I saw a bunch of issues with templates, especially cite book/journal and this is probably what is causing it. Praxidicae (majadiliano) 18:14, 23 Agosti 2019 (UTC)[jibu]

I don't undertand what you have said because the templates are mysterious to me!!! Let's inform Kipala or Muddyb. Peace to you. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:08, 24 Agosti 2019 (UTC)[jibu]
Hello Praxidicae, care to fix it for us? Your help would be greatly appreciated!--'Muddyb Mwanaharakati' 'Longa' 07:08, 27 Agosti 2019 (UTC)[jibu]
I'm apparently wrong about that but the issue with the book template is because it requires =title in the template, I will work on them later today. :) Praxidicae (majadiliano) 11:32, 27 Agosti 2019 (UTC)[jibu]
Thanks. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:33, 27 Agosti 2019 (UTC)[jibu]
I'll work on the template itself but this is what is basically required: * {{cite book |last=Creighton |first=Oliver |year=2005 |title=Medieval Town Walls: An Archaeology and Social History of Urban Defence|location= |publisher= |isbn=978-1-85760-259-3}}. Another good option if you don't feel like filling all of it out yourself (I never do) is to reFill. It doesn't appear to be enabled on this wiki, so I'll also look into that. :) Praxidicae (majadiliano) 11:44, 27 Agosti 2019 (UTC)[jibu]
Thanks again and peace to you. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:46, 27 Agosti 2019 (UTC)[jibu]
It might be helpful if you name the templates you came about. We hve swahilized a number of templates but find the recent ones a bit complicated. Thus have to look for work-arounds. Kipala (majadiliano) 19:40, 27 Agosti 2019 (UTC)[jibu]

Reminder: Community Insights Survey[hariri chanzo]

RMaung (WMF) 18:58, 20 Septemba 2019 (UTC) [jibu]

Ndugu kwa bahati mbaya umeharibu kazi! Sijamaliza nilikuwa nilihifadhi hatua ya kwanza tu (kwa hiyo bado Kiswahili kibaya!) nikaendelea na kupumzika - basi inaonekana yote imepotea. Basi. - Je uliona email yangu?Kipala (majadiliano) 09:47, 18 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]

Basi nimeweza kuitengeneza, kumbukumbu ya laptop ilikuwa nayo. Tena kosa langu: nilipoona "Edit conflict" sikuchagua version yangu. Kipala (majadiliano) 10:07, 18 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]

Mfumo katika soka[hariri chanzo]

Ndugu Riccardo natumai uko salama, kuna makala inayohusu mifumo katika soka "formation" nilijaribu kutafsiri kutoka lugha ya kiingereza, nilivyochapisha utangulizi haukua na marejeo kabisa pamoja na jamii, nilikuta notification kwamba ukurasa huo utafutwa, niliongeza vilivyokosekana kwa kutafsiri kipande kingine chenye marejeo, kwa upande wa jamii niliweka michezo hii ilikua ijumaa ya tarehe 18, hadi leo hii bado naona kuna ujumbe wa kufuta makala hiyo.--Innocent Massawe (majadiliano) 05:36, 21 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]

Ndugu, usiogope, mradi haijafutwa! Tutaipitia upya. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 06:42, 21 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]

Tawimto[hariri chanzo]

Naona umeanza kusahihisha uwingi wa tawimto kuwa "matawimto". Una uhakika ??? Tawimto ni mto ambao ni tawi la mfumo wa mto mkubwa zaidi. Kama ni mingi ni mito - ha hii naona ni neno kuu. Kwa hiyo si lazima "mito" ionyeshe uwingi? Sikioni inaumia kidogo nikiona "matawimto mikubwa" (Syr Darya). Kipala (majadiliano) 13:07, 25 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]

Labda umesahau kwamba jambo hilo la neno linalotokana na mawili tulilijadili katika warsha wa astronomia, nikapewa majibu ya hakika: ni mafungunyota, mafunguvisiwa n.k. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:25, 25 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]
Sawa kabisa, hii ninakumbuka sana. Ila tu: fungunyota ni fungu moja lenya nyota nyingi, kundibyota vilevile, kwa hiyo kama mafungo mengi - unapata umbo.

Tawimto si tawi moja lenye mito mingi, wala mto moja mwenye matawi mengi (kinyume chake katika ufafanuzi!) - ni mto mmoja lenye tabia ya kuwa tawi la mto mkubwa zaidi. Kwa hiyo naona mantiki halingani. Ama iwe "matawimito" au "tawimito". Basi nitajaribu kuuliza aruspicina di Tataki. Kipala (majadiliano) 20:31, 25 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]

Nakubali kwamba kuna tofauti na fungunyota, lakini jibu lilikuwa kwamba -a inayofuata ni lazima ilingane na fungu, si nyota, kwa hivyo iwe la, si za. Kama ni hivyo, wingi wake ni ya kutokana na mafungu. Sasa naona kuhusu tawimto ni vilevile. Labda tunaelewa tofuati neno hilo. Wewe unalisoma kama mtotawi, mto ulio tawi la mwingine. Mimi naona ni tawi la mto. Yaani hapa neno mto unajumlisha mto mkuu na matawi yake yote. Basi, uulizie TATAKI, bila kusahau suala la "virusi za UKIMWI". Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:53, 27 Oktoba 2019 (UTC)[jibu]
Angalau jibu moja (aliandika sms), angalia Majadiliano:Tawimto. Amani! Kipala (majadiliano) 22:07, 1 Novemba 2019 (UTC)[jibu]

Vigezo vya Msanii kuwekwa Wikipedia[hariri chanzo]

Nahitaji kujua Vigezo vya msanii kuwekwa Wikipedia. Je anatakiwa awe na umaarufu wa kiasi gani..? au awe ametoa nyimbo ngapi zilizomo katika kurasa za Google na YouTube..? Naomba msaada katika hili Mikuyu Denis (majadiliano) 15:55, 31 Desemba 2019 (UTC)[jibu]

Ndugu, si suala la idadi ya nyimbo. Unaweza ukaandika mmoja tu ukawa maarufu mara, au ukaandika nyingi lakini hazivutii watu... Vigezo vya umaarufu alikwishakupa Kipala ukamuambia aache ubaguzi! Ubaguzi gani? Ndiyo namna ya kumjibu mzee wa watu aliyetufanyia kazi kuuubwwa miaka zaidi ya 10? Hivyo uonyeshe huyo msanii amejulikana kweli na watu wengi: kwa mfano kwamba magazeti yanamzungumzia. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 08:40, 1 Januari 2020 (UTC)[jibu]

Klabu ya Wikipedia katika sekondari ya Alfagems[hariri chanzo]

Habari za siku. Samahani nauliza kuhusu program ya wikipedia kwa hapo shuleni, siku ile hatukufikia muafaka kama naweza kuwa nakuja kwa vipindi vya wikipedia. Magotech (majadiliano) 05:47, 13 Februari 2020 (UTC)[jibu]

Ndiyo, karibu sana Jumapili saa 8:00 kamili. Tutakuwa na mashindano ya utunzi bora wa makala. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:03, 13 Februari 2020 (UTC)[jibu]
Asante, ntajumuika nanyi! Magotech (majadiliano) 11:53, 14 Februari 2020 (UTC)[jibu]
Habari, sawa ntazipitia. Pia wanafunzi waliniambia leo kuna kipindi cha wikipedia naomba kujua itakuwa sangapi. Ikiwezekana naomba ratiba ya wiki nzima tafadhali Magotech (majadiliano) 06:01, 18 Februari 2020 (UTC)[jibu]
Klabu ya Wikipedia ni Jumapili tu. Siku nyingine zote kuanzia saa 8:00 mchana wanafunzi wanaruhusiwa kwenda chumba cha tarakilishi kujisomea lolote. Kama ukipenda klabu iwe siku tofauti na Jumapili, tunaweza kuibadilisha, lakini iwe mara moja kwa juma. Asante kwa ushirikiano wako na amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:06, 18 Februari 2020 (UTC)[jibu]
Sawa basi ngoja ibakie jumapili kama ilivyo kwa sasa, mwanzo nilidhani kuwa kuna siku nyingine katikati ya wiki ya Wikipedia. Asante! MagoTech Tanzania 23:08, 18 Februari 2020 (UTC)

Habari za siku ndugu. Samahani sana nilipata dharura nikaondoka Morogoro. Sitokuwepo kwa mda kwa maana hiyo sitoweza kuhudhuria katika mikutano ya klabu ya Wikipedia kwa shuleni Alfagems. Samahani sana kwa usumbufu ulio na unaoweza kujitokeza. Nitawatembelea pindi ntakapo rejea tena. Asante MagoTech Tanzania 12:59, 16 Machi 2020 (UTC)

Masahihisho[hariri chanzo]

Ndugu unasahisha haraka mno. Meitneri sijamaliza. Sasa nilikuwa na masahihisho katika dirisha langu, nasi sehemu ya kazi yako imepotea, nahofia. TAfadhali nipe masaa kadhaa! Kipala (majadiliano) 15:10, 16 Machi 2020 (UTC)[jibu]

Pictures from Wiki Loves Africa 2020[hariri chanzo]

Hello. I am sure you are right, but we can only use what is available. So do not hesitate to take different pictures, more relevant, I will be glad to insert them. Actually we had the same problem. In the beginning we had only 19th-century engravings. But this is changing rapidly now. And Wiki Loves Africa helps. Have a nice day, Ji-Elle (majadiliano) 14:47, 21 Machi 2020 (UTC)[jibu]

Good news, here came some more contemporary pictures uploaded this morning ([2]). If you want to add something you can send me an email. -- Ji-Elle (majadiliano) 06:09, 22 Machi 2020 (UTC), from France[jibu]

Kumbukumbu[hariri chanzo]

Habari, nimeona ni vyema nikupatie picha yako ya kumbukumbu katika mradi wa Astronomia.
Riccardo Riccioni akitazama anga wakati wa mradi wa Astronomia.

. Czeus25 Masele (majadiliano)

Makala kwa ufutaji[hariri chanzo]

Naona umependekezwa makala Tarekh ya mitume:Ibrahim ifutwe, ni sahihi maana amenakili yote. Ila usipoandikisha makala katika Wikipedia:Makala kwa ufutaji inaweza kusahauliwa na kubaki. Naomba ukumbuke! Kipala (majadiliano) 11:54, 23 Aprili 2020 (UTC)[jibu]

Ma lei è di Grosseto. Perchè ci siamo già incrociati, ma non mi ricordo dove? Io sono di Castel del Piano. A parte la mia curiosità spero non inopportuna mentre venivo a sbirciare ho notato che ci sono tre link nella colonna a sinistra non tradotti:

  • email this user
  • mute preferences (in italiano abbiamo tradotto "preferenze sul silenzio")
  • view user groups

se mi scrive la traduzione ve li sistemo su translatewiki. Grazie--Pierpao (majadiliano) 13:12, 26 Aprili 2020 (UTC)[jibu]

No, non sono di Grosseto, ma mia sorella si è sposata a Orbetello e vive a Capalbio. Ha 4 figli in giro per il mondo... Poi ho due amici sacerdoti di Castell'Azzara. Può darsi che ci siamo visti nella maremma! Scusa, ma non capisco bene quello che dici riguardo ai tre link. Pace a te! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 13:16, 26 Aprili 2020 (UTC)[jibu]

Makala kwa ufutaji[hariri chanzo]

Naona umependekeza tena makala 2 zifutwe. Ila usipoandikisha makala katika Wikipedia:Makala kwa ufutaji inaweza kusahauliwa na kubaki. Nimeona kwa kubahatika tu! Kipala (majadiliano) 11:54, 23 Aprili 2020 (UTC)[jibu]

Usaidizi wa upangiliaji wa makala[hariri chanzo]

Ndugu ricardo mimi ni mgeni hapa sina muda mrefu, ila mara kadhaa nimekua nikiona makala nyngi sana hasa za lugha ya Kiswahili zikiwa zime haririwa na wewe, una mchango mkubwa sana kwenye makala nyingi za Kiswahili Hongera kwako. Nina makala ambayo nimeaianzisha hapa, kwenye swwiki na ningependa uipitie kwa maboresho zaidi, Nafurahi sana kura miongoni mwa watumiaji wa swwiki na ninatazamia kutoa mchango mkubwa kwenye swwiki. Ahsante Na makala hiyo inaitwa Counsellorsalah.

Ndugu, nimeshapitia na kurekebisha makala hiyo mara mbili, ila mwenyewe sijui kurekebisha vizuri sanduku la infobox mwanzoni. Kwa mengine namna ya kujifunza ni kuangalia kila mara marekebisho tunayofanya ili ufanye vizuri zaidi na zaidi. Unapoona katika "Mabadiliko ya karibuni" kwamba ukurasa wako umehaririwa na mwingine, bonyeza "tofauti" ili kuona wapi na wapi yamefanyika hayo mabadiliko. Polepole ndiyo mwendo. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:44, 9 Mei 2020 (UTC)[jibu]

Kanisa la Mwenyezi Mungu[hariri chanzo]

I figured, that I could spread the word about The Church of Almighty God (or "Kanisa la Mwenyezi Mungu" as it's officially called in Swahili), which is also known as Eastern Lightning (or Umeme wa Mashariki).

Here are some links to be shared:

Do you mind if I make a personal userpage for an English mock-up of a Swahili article on The Church of Almighty God?

Thanks for reading. --Apisite (majadiliano) 23:09, 3 Agosti 2020 (UTC)[jibu]

Please, ask [[Mtumiaji:Kipala|Kipala]]. Thank you. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:39, 4 Agosti 2020 (UTC)[jibu]

Nimechanganyikiwa katika Wilaya ya Lindi[hariri chanzo]

Labda utaona nimeanzisha makala za wilaya mpya "Mtama" pale Lindi. Basi nilikosea, kesho nitafanya usafi tena (chanzo ni swali lako kuhusu kata lile kama ni mjini au vijijini, nikaangalia orodha ya wakazi wa 2016, nikachanganya wilaya na jimbo....) Nivumilie kidogo, sasa nalala. Kipala (majadiliano) 22:35, 17 Agosti 2020 (UTC)[jibu]

Hongera Ndugu Riccardo ya kutupeleka kwa 60,000[hariri chanzo]

Nyota ya Ujenzi wa Wikipedia

Ndugu Riccardo, umetupeleka kwa makala 60,000. Hongera na Asante! Kipala (majadiliano)

Hongera Ndugu Riccardo. Czeus25 Masele (majadiliano) 13:05, 20 Agosti 2020 (UTC)[jibu]
Asante kwenu kwa kutambua mchango wangu. Mimi pia natambua mchango wenu na wa wenzetu wengine. Tuongeze bidii tukilenga makala ya 100,000. Lakini pia namkumbusha Kipala suala la kupunguza viongozi waliopumzika muda mrefu na kuongeza wakabidhi wapya, mmojawapo Czeus25 Masele... Amani kwa wote! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:54, 21 Agosti 2020 (UTC)[jibu]

Wakabidhi[hariri chanzo]

naomba uangalie tangazo kwenye ukurasa wa Mwanzo (juu) na ukurasa wa Wakabidhi. Kipala (majadiliano) 10:39, 4 Septemba 2020 (UTC)[jibu]

Maswali[hariri chanzo]

Nimeangalia makala za Rutamba, Malunde na Madume bora; Malunde najaribu kufuatilia, Rutamba nimesahihisha, Madume bora ningeacha kwa sasa au kufuta, sjui. Tafadhali angalia swali langu kuhusu Taniaba. Kipala (majadiliano) 14:13, 6 Septemba 2020 (UTC)[jibu]

Kata mpya[hariri chanzo]

Ombi tu: tafadhali usianze bado kuhariri kata mpya nilizoingiza katika vigezo vya masanduku ya kata. Kazi hii ni maandalizi ya mafundisho kwa ajili ya wachangiaji wapya, wapate nafasi ya kuhariri kwa njia nyepesi. Kipala (majadiliano) 08:55, 28 Septemba 2020 (UTC)[jibu]

Habari, ukiwa na nafasi nashukuru ukiangalia baruapepe zako. Kipala (majadiliano) 04:09, 20 Oktoba 2020 (UTC)[jibu]

Mambo ya ukabidhi, baruapepe[hariri chanzo]

Tafadhali angalia baruapepe. Kipala (majadiliano) 14:49, 6 Novemba 2020 (UTC)[jibu]


Gunter Pauli[hariri chanzo]

Hello Riccardo, could you please kindly clarify the reason why you have deleted this page ? https://sw.wikipedia.org/wiki/Gunter_Pauli Thank you Freemanbat (majadiliano) 13:13, 24 Novemba 2020 (UTC)[jibu]

Yes, I deleted it because this is Swahili Wikipedia and your text was not in Swahili. I think it was in a South Asian language. Peace to you! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:32, 24 Novemba 2020 (UTC)[jibu]
Just to chip in: you uploaded some gibberish. Did you take it from Google Translate? Please read the welcome notice on your user page, and be reminded that this is considered unwanted here. Generally not a good idea if you have no clue of the language you try to contribute to, because the results usually are so bad that we delete it anyway (so even if you had picked the right language at google translate). Kipala (majadiliano) 19:17, 24 Novemba 2020 (UTC)[jibu]

Hello,

is it possible to flag the name of the train station Hamburg Dammtor in this map thats shown in the article:

Ramani ya mtandao wa kituo cha Hamburg S-Bahn na Dammtor

All the names of the stations in this map are flagged in black language, but because this map is also shown in the WP page of Kituo cha Hamburg Dammtor, could you flag the name Hamburg Dammtor in the map of this article in a different colour?

Reg, Alex Owah 84.174.183.93 13:43, 17 Desemba 2020 (UTC)[jibu]

Hi, the map is as it is. it is not flexible. You would have to make a new map. Maybe there is a different one, you better look for it at commons. Kipala (majadiliano) 20:37, 18 Desemba 2020 (UTC)[jibu]

Hello, I was patrolling recent changes and noticed this article and upon some investigation I found out that it's Google translation of English Wikipedia article, which is a copyright violation, so I am requesting you to delete it. --1997kB (majadiliano) 17:15, 16 Januari 2021 (UTC)[jibu]

Majadiliano:Frozen 1[hariri chanzo]

If you'll see the discussion at this page, the article is marked as needing improvement. I already signed up so it can be moved, but I'm not confirmed yet. I don't know what else to do with the article just yet as I'm not fluent in Swahili. But this page and other Disney articles have some problems due to vandalism. One of the other pages with these kinds of problems would be The Fox and the Hound. Bambi and Dumbo are two more. I also saw Teletubbies deleted, but can it be recreated with better content? I like peace and quiet (majadiliano) 21:57, 27 Februari 2021 (UTC)[jibu]

At Thumbelina (filamu ya 1994), the English text added that was reverted would have helped the article if it had been translated. So, who could translate it? I also wanted to add that Dove Cameron plays the twins in Liv and Maddie. As usual, the English text would have helped the article. For those other pages like The Fox and the Hound, Dumbo, and Bambi, they often have machine translation in them, and the machine translations came from either English or Simple English Wikipedias (or both). The Dumbo page seemed to have the worst translation. Meanwhile, other Disney pages don't exist yet (like Fantasia, Cinderella, Lady and the Tramp, The Aristocats, Oliver & Company, The Little Mermaid, The Rescuers Down Under, and many more. I don't know if it'd be worth it to just create stubs about them. Even if it is, I wouldn't know who could improve them all. Do you? I like peace and quiet (majadiliano) 20:13, 6 Machi 2021 (UTC)[jibu]

I appreciate your intention but I think at this stage our little Wikipedia has more urgent tasks. Peace to you! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 05:10, 7 Machi 2021 (UTC)[jibu]
Can the machine translation on The Fox and the Hound be removed? That, and on pages like Liv and Maddie, The Simpsons, and Hannah Montana, Jamii:Televisheni za Marekani was replaced with Jamii:vipindi vya televisheni. The problem with that is, they are American television shows, but the other category says genres of television. They aren't television genres. The genre of Liv and Maddie is a situation comedy for teenagers (teen sitcom). Hannah Montana is also that. The Simpsons, however, is an animated adult situation comedy. So, how does this get corrected? Finally, there's the fact that I would just fix everything myself if I knew Swahili well. Is there a way to learn it? I like peace and quiet (majadiliano) 17:59, 12 Machi 2021 (UTC)[jibu]
I think there are many ways to learn Swahili, especially through internet. About television, I don't understand your point. If something is presented in TV it is called kipindi, without examining what is its genre. Peace to you! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:26, 13 Machi 2021 (UTC)[jibu]
Jamii:vipindi vya televisheni is linked to Category:Television genres at the Wikidata page. Is that wrong? Meanwhile, Jamii:Televisheni za Marekani was supposed to say Category:Television of the United States. However, should it be Jamii:Vipindi vya televisheni za Marekani for Category:Television series of the United States? Finally, do you know the best ways I can learn Swahili? I've already been blocked in another Wikipedia (diqwiki) because I was too disruptive. Right now, they are working on cleaning up pages after vandalism by the Disney vandals. There are many Disney vandals, but the worst ones do things like adding the machine translations, content in the wrong language, or pages with no content. The diq articles were made very badly, where the content was short and unwikified. That has happened here before. However, there hasn't been disruption to The Fox and the Hound since 2011 (10 years ago), so can the protection be removed? However, it's at least much better now with the machine translated content. I like peace and quiet (majadiliano) 19:32, 14 Machi 2021 (UTC)[jibu]
Riccardo asked me to look at this. As for the naming of the categories, we have to consult a little. May take a bit of time, depends who has time for that. For learning Swahili? If you find a course that is best. If you cannot find one, do not try to translate long texts. You can possibly help by doing short stubs if you are wise enough to know your limits. Disney ntries are no priority here. Kipala (majadiliano) 06:13, 16 Machi 2021 (UTC)[jibu]

nakala ya arthur schopenhauer[hariri chanzo]

je unaeza fafanua sababu za kutoa sehemu nilioandika kuhusu mwanafalsafa huyu? Sinatrasona (majadiliano) 19:37, 10 Machi 2021 (UTC)[jibu]

Grazie mille!!![hariri chanzo]

Sì, preghiamo gli uni per gli altri, e anche perchè il signor Corona se ne torni da dov'è venuto al più presto!!!

Scusami per il primo messaggio, me lo sono scritto direttamente nella mia pagoina pensando di scrivere nella tua. Pace a te!

Rei Momo (majadiliano) 23:52, 13 Machi 2021 (UTC)[jibu]

Request for adding an article[hariri chanzo]

Hello sir Riccardo Riccioni Could you please write a stub about the Tachelhit language in this wiki ? its an african language in Morocco – just a few sentences based on https://en.wikipedia.org/wiki/Shilha_language ? Thank you very much -- Ayour2002 (majadiliano) 15:03, 17 Machi 2021 (UTC)[jibu]

Hello Sir!!! Samahani kwa usumbuu, baruapepe ya Ijumaa (matembezi ya anga) ilifika kwako? Kipala (majadiliano) 07:25, 22 Machi 2021 (UTC)[jibu]

Caro padre Riccardo, Pace!!!

Come stai? Io, mia mamma, la mia morosa e tutte le nostre famiglie stanno bene: tutti negativi al Covid-19!!! Ma in Italia la situazione è molto brutta, anzi, fa schifo, 15 regioni in zona rossa. le nostre mamme hanno fatto le due dosi del vaccino Pfeizer, e hanno avuto solo un po' di male al braccio e un po' di stanchezza nei giorni successivi.

Ieri, il presdiente del Consiglio dei ministri e sua moglie si sono fatti vaccinare pubblicamente con Astra Zeneca.

La Pasqua sarà comunque a casa, tutti confinati, eccetto i ricongiungimenti familiari, ma anche quì ci saranno molte restirizioni.

Per favore, ti chiedo qualche minuto per vedere se vada tutto bene in questa pagina. Secondo me, potresti aggiungere che, attualmente (al momento della sua elezione) è il vescovo cattolico italiano più giovane. Grazie molte per il tuo prezioso aiuto!!!

Una Buona e Santa Pasqua, in comunione

Rei Momo (majadiliano) 08:24, 31 Machi 2021 (UTC)[jibu]

Buon Lunedì dell'Angelo[hariri chanzo]

carissimo padre Riccardo, pace!!! Grazie per le tue preghiere!!! Completerò con piacere le diocesi mancanti della Lombardia. Poi, per le correzioni, ci penserai tu. Grazie ancora, un caro saluto Rei Momo (majadiliano) 09:28, 5 Aprili 2021 (UTC)[jibu]

Ciao, ho cominciato ad aprire la diocesi di Crema. Quando riesci a trovare qualche minuto, per favore, dovresti sistemare le poche cose che ho lasciato in italiano dove ci sono i nomi dei vescovi, soprattutto i due vescovi appartenenti agli ordini religiosi.
Grazie ancora, a presto
Rei Momo (majadiliano) 09:43, 5 Aprili 2021 (UTC)[jibu]

Kuzuia mtumiaji[hariri chanzo]

Habari, Kuna mtumiaji ambaye ametumia IP address na kufuta makala kwa kuandika maneno ya kingereza. Nimejaribu kumzuia je nimefanya kitu sahihi? Na je ambavyo nimefanya ndo inavyotakiwa kuwa? Asante sana --CaliBen (majadiliano) 08:50, 19 Aprili 2021 (UTC)[jibu]

Makala Yenye Mashaka[hariri chanzo]

Habari Mr Riccardo. Kuna hii makala (https://sw.wikipedia.org/wiki/Josephs_Quartzy) nimejaribu kupitia vyanzo vyake ila nimekuwa na mashaka navyo kama ni vyanzo vya kuaminika moja kwa moja kutumika na kamusi elezo, nimeona vinatoka katika mitandao ambayo mtu anaweza kutengeneza account na kuweka taarifa zake binafsi, unaweza kuitazama zaidi, Amani sana Idd ninga (majadiliano) 22:15, 27 Aprili 2021 (UTC)Idd ninga[jibu]

Asante kwa kunishirikisha. Mimi pia naona shaka, ila sina utaalamu zaidi. Kwa mambo kama hayo ni afadhali kumuuliza Kipala. Amani kwako pia. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 08:26, 28 Aprili 2021 (UTC)[jibu]

Kigezo cha Redirect[hariri chanzo]

Habari, Naomba kuuliza ni kwa namna gani unaweza kuweka redirect. Kuna jamii ya waigizaji filamu wa India nataka niiwekee redirect kuelekea jamii ya waigizaji filamu wa uhindi. Nimejaribu ila sikufanikiwa, naomba mwongozo. Asante! --CaliBen (majadiliano) 05:45, 29 Aprili 2021 (UTC)[jibu]

Kwanza hongera kwa juhudi zako. Pili suala la majina ya nchi linatakiwa bado kujadiliwa. Mfano mmojawapo ni: India au Uhindi? Tatu: kuweka redirect ni rahisi, ila ukielekeza upya jamii, makala za jamii iliyoelekezwa upya hazionekani katika jamii mpya. Inabidi ubadilishe jina la jamii katika kila ukurasa. Labda kuna template maalumu, lakini mimi siijui. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:25, 29 Aprili 2021 (UTC)[jibu]

Hongera[hariri chanzo]

Hongera, nikitazama massview analysis hiyo https://pageviews.toolforge.org/massviews/?platform=all-access&agent=user&source=category&range=latest-20&subjectpage=0&subcategories=1&sort=views&direction=1&view=list&target=https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamii:Watakatifu_Wakristo

Jamii:Watakatifu Wakristo 2021-04-10 - 2021-04-30
Daily average Totals 3.385 pages 30.090/total 1.433/day
1 Orodha ya Watakatifu Wakristo 1.482 71 / day

Ingawa naona jamii inajumlisha kurasa nyingi ambazo si watakatifu wenyewe (kama vile watu wengi wa Biblia kwa jumla, mahali kama Roma), hata hivyo kuna wasomaji wengi wanaotafuta huduma hiyo! Ubarikiwe! Kipala (majadiliano) 14:21, 1 Mei 2021 (UTC)[jibu]

Asante kwa pongezi. Hata hivyo kuna mengi ambayo siyaelewi katika majedwali hayo... --Riccardo Riccioni (majadiliano) 05:39, 2 Mei 2021 (UTC)[jibu]

Matumizi ya wikimedia special:content translation[hariri chanzo]

Habari Riccardo Riccioni, Naomba kuuliza kuhusu matumizi ya wikimedia special:content translation, nilishauriwa kufundisha watu namna ya kuitumia kutoka kwa mtu ambaye anashiriki kikamilifu kuhakikisha kwamba wikimedia special:content translation inatumika. Juzi nilijaribu kuitumia mwenyewe kuona kama itakua na manufaa kwetu nikaona ni kifaa ambacho kingeweza kutufaa sana kama watu watakaokua wanakitumia watakua makini. Naomba kupata mtazamo wako juu ya kifaa hichi kifaa. Na je ni sahihi nikiwafundisha watu kutoka Arusha kutumia? Asante, --CaliBen (majadiliano) 10:33, 17 Mei 2021 (UTC)[jibu]

Makala juu ya umaarufu![hariri chanzo]

Salaam tele. Unisamehe kwa ukimya wangu, kuna mambo mengi yanaingiliana kwa wakati mmoja. Nimeusoma ujumbe wako na ninakubaliana nao kwa asilimia mia moja. Nilidhani nimeiandika mimi kumbe kumbukumbu zangu zimeyonzwa na msukumo wa maisha!--Muddyb Mwanaharakati Longa 08:28, 30 Mei 2021 (UTC) [jibu]

Kuhusu marekebisho ya nakala ya Arthur Schopenhauer[hariri chanzo]

Bado sijatosheka na sababu ulizopeana za kufuta aya nyingi nilizowakilisha tawasifu ya mwanafalsafa Arthur Schopenhauer. Mimi ni mzaliwa wa Kenya na nimeongea kiswahili tangu utotoni na nimekua nikisoma Kazi za Schopenhauer kwa miaka zaidi ya saba sasa. Nilikua na nia ya kuandika nakala zaidi nikifafanua nadharia muhimu za mwanafalsafa huyu lakini katisha tamaa na tabia hii yako ya kufutafuta mawakilisho yangu kiholelaholela.. kama kuna kitu yauelewi niambie kwanza tujadili ama urudishe ujinga yako Italia!! Sinatrasona (majadiliano) 11:19, 14 Juni 2021 (UTC)[jibu]

Asante kwa tusi lako, ila si utamaduni wetu. Pia ulivyoandika ni uthibitisho kwamba Kiswahili chako si sanifu. Kwa mfano "ujinga yako" si sahihi. Kama ukiona nimefuta kiholela, uwasiliane na mkabidhi mwingine aweke mambo sawa. Amani tele kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:32, 16 Juni 2021 (UTC)[jibu]

Can you help me correct an article? Thank you![hariri chanzo]

Hello, @Riccardo Riccioni:! I wrote an article on Andrea Benetti, a well-known Italian artist https://en.wikipedia.org/wiki/Andrea_Benetti_(artist). I used the automatic translator to make a draft https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtumiaji:BarbaraLuciano13 . Could you help me correct the text and add the infobox with the photo at the beginning and the categories at the bottom? Unfortunately I don't know the language and I am not able to do it ... Thanks for what you can do, see you soon, --BarbaraLuciano13 (majadiliano) 09:05, 19 Juni 2021 (UTC)[jibu]

Hello, please save the Qaem Shahr article and link it to the wiki data item. Thank Viera iran (majadiliano) 22:45, 24 Julai 2021 (UTC)[jibu]

Kukarabisha wageni[hariri chanzo]

Salamu,Katika ukurasa huu hapa https://sw.wikipedia.org/wiki/Mtumiaji:Ultracounter_nitrogenius wakati namkaribisha nilijikuta nimechapisha sehemu ya kurasa ya mtumiaji bila kugundua, ila baada ya kushtuka nikafuta alama na maneno ya ukaribisho na kwenda kuandika upya tena katika ukurasa wa majadiliano, nisaidie kutazama kama itakuwa sawa na msaada zaidi wa maelekezo iwapo ikitokea nimerudia makosa kama hayo, Amani sana Idd ninga (majadiliano)

Translation request[hariri chanzo]

Hello.

Can you translate and upload the article en:Flag of Azerbaijan in Swahili Wikipedia? It does not need to be long.

Yours sincerely, Multituberculata (majadiliano) 14:06, 4 Agosti 2021 (UTC)[jibu]

Kuzuia mtumiaji[hariri chanzo]

Habari ndugu,
Naona umemzuia mtumiaji Awadhi awampo bila kumpa sababu. Naomba kama hautojali kumwandikia sababu ya kumzuia katika kurasa yake ya majadiliano. Asante.
Amani kwako MagoTech Tanzania (majadiliano) 10:58, 5 Agosti 2021 (UTC)[jibu]

Ndugu, hongera kwa kumtetea mhariri mpya, lakini sijakuelewa. Mbona nilimpa maelekezo tarehe 25 Juni asiyafanyie kazi? Sababu ya kumzuia ni hiyo: kutafsiri kwa kutumia progamu bila kurekebisha matini hata yaeleweke! Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:28, 6 Agosti 2021 (UTC)[jibu]

Kigezo ya uzuio[hariri chanzo]

Naomba uangalie Kigezo:Zuia tafsiri. Itumiwe kwa kunakili {{Zuia tafsiri}} ~~~~ na kuweka kwenye ukurasa wa majadiliano wa mhusika, baada ya kumzuia.

Unadhani inafaa? Kesho nataka kufanya zoom meeting saa 2 usiku kuhusu hiyo. Ungeweza kungia? (najua ni saa mbaya kwako...)

Taarifa ya kukuzuia!

Ndugu, imenibidi kukuzuia kwa sababu zinazotajwa chini. Wakati unapokuwa umezuiwa huwezi kuhariri isipokuwa penye huu ukurasa wako wa majadiliano. Unaweza kunijibu kwa kutumia “Email this user”.

Sababu ni kuwa umeingiza matini iliyopatikana kwa njia ya tafsiri ya kompyuta ikiwa na kasoro nzito ya lugha. Umearifiwa kwamba ni marufuku kumwaga matokeo ya google translate katika makala zetu. Wachangiaji wanaopuuza utaratibu huu wanasababisha hasara kubwa kwa Wikipedia yetu na kuwapa wengine kazi kubwa mno ya kusafisha makosa yao.

Bila shaka una nia nzuri kuchangia katika Wikipedia. Tutafurahi kushirikiana nawe lakini ni lazima ufuate utaratibu. Kazi yetu kama wakabidhi ni kulinda mradi huu.

Ukiwa tayari kufuata utaratibu pamoja na kupitia upya matini ulizozileta tayari, naomba uwasiliane nami kwa kufungua ukurasa wangu (bofya jina langu chini) na kuniandikia baruapepe kwa kubofya “Email this user” upande wa kushoto. Hapo nitaweza kukuruhusu tena. Hapo lazima uwezeshe njia kwa kufuata maelezo katika Wikipedia:Email.

Kipala (majadiliano) 12:00, 11 Agosti 2021 (UTC) [jibu]


Msaada Tafsiri[hariri chanzo]

Habari, nimetunga Msaada:Tafsiri. Tafadhalia angalia kama inafaa, inaeleweka n.k. Naona wako wachache watakaoisoma maana wako wanaojitahidi. -- Nimeona nitaje pia ContentTranslation. Hadi sasa nimejaribu kuificha. Lakini hao wote wanatumia google, na google haina msaada kutunza fomati. ContentTranslation angalau inasaidia kupata fomati (interwiki, jamii). Ushauri wako? Kipala (majadiliano) 12:31, 12 Agosti 2021 (UTC)[jibu]

Kweli, ni afadhali kuliko Google. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:36, 12 Agosti 2021 (UTC)[jibu]

Habari naona umemzuia Praygood Mwanga, sawa kabisa. Ila naona ni vema kuongeza chini ya kigezo nusu sentensi tunapotaja makala tunayorejelea. Kama ningeelewa vigezo vizuri zaidi, ningeingiza nafasi ndani ya kifupi cha kigezo lakini sijui. Kwa mtu kama yule kijana anayeazisha makala mengi, ni vema kutaja makala husika chini ya kigezo, kabla ya sahihi. Unaonaje? Kipala (majadiliano) 21:19, 19 Agosti 2021 (UTC)[jibu]

Location za Kenya - vijiji au kata?[hariri chanzo]

NAona unahariri locations za Kenya ukiziita "kijiji". Nisipokosei hizo ni zaidi kata kuliko "vijiji". Nimekutumia faili ambako nimeorodhesha majina kutoka faili ya sensa; nadhani nimefaulu kutenganisha ngazi mbalimbali jinsi ilivyoandikwa kule. Nisipokosei, kuna
County - subcounty - division - location - sublocation
ambazo zinalingana na
Mkoa - wilaya - tarafa - kata - kijiji.

Au unaonaje? Kipala (majadiliano) 15:28, 10 Septemba 2021 (UTC)[jibu]

Ndugu, nimeshamaliza kuandika makala kwa kata (wards) zote za Kenya kupitia vitabu vya sensa. Vijiji ambavyo mpaka sasa havina ukurasa, maana yake si kata au kata imeanzishwa baada ya sensa. Nadhani msamiati wa hapo juu una tofauti kati ya Kiingereza na Kiswahili, labda ni kwa ajili ya utekelezaji wa sensa. Nimeona umebadilisha ukurasa juu ya kijiji cha Suam, lakini ungesoma kwanza ukurasa juu ya maana mbalimbali za jina hilo ungeona kuna kijiji cha Suam katika kaunti moja na kata ya Suam katika kaunti nyingine. Kwa vyovyote kata nyingi zina jina la kijiji chake kimojawapo. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:28, 12 Septemba 2021 (UTC)[jibu]

Upitiaji wa makala[hariri chanzo]

pitia makala hii https://sw.wikipedia.org/wiki/Dougaj pamoja na https://sw.wikipedia.org/wiki/Shule_ya_Sekondari_ya_FPCT_Tumaini nimerekebisha kidogo Justine Msechu (majadiliano) 08:16, 11 Septemba 2021 (UTC)[jibu]

Sawa, lakini sasa angalia mimi nilivyorekebishwa zaidi ili ujifunze kufanya vizuri zaidi. Amani kwako| --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:28, 12 Septemba 2021 (UTC)[jibu]

Vimo vya vilele vya Mlima Kenya[hariri chanzo]

Riccardo salaam. Wakati ulipoandika vimo vya vilele vya Mlima Kenya, labda ulikuwa umekosea? Ukarasa wa Mlima Kenya una vimo vingine. Amani kwako. ChriKo (majadiliano) 14:11, 16 Septemba 2021 (UTC)[jibu]

Ni kweli, nimeona hicho, ila nimefuata Wikipedia ya Kisebuano. Kama unaweza kusahihisha, nitashukuru sana. Kinachonifurahisha ni kwamba sasa Wakenya wengi wanasoma Wiki ya Kiswahili! Amani kwako pia! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:34, 16 Septemba 2021 (UTC)[jibu]

Apology[hariri chanzo]

Hello Riccardo Riccioni I hope you're doing well. I'm C1K98V from India. I don't know the language, nor was aware of the sw wikipedia. However, I'm familiar with the policy of wikipedia. I apologize to begin with the wrong step. But my intention was not violate the policy. Please help with expanding the stub subject, creating article associated with India. I upload creative commons license files on wikimedia commons. I assure, I won't create any problem to the community. Please guide me. Thanks for your consideration, stay safe. --C1K98V (💬 ✒️ 📂) 11:39, 25 Septemba 2021 (UTC)[jibu]

Grazie per il tuo benvenuto :-) La mia utenza qui è stata creata in conseguenza di una rinomina effettuata, non conosco lo swahili ma fa comunque sempre piacere essere "benvenutati", poter ringraziare in italiano è poi davvero una sorpresa! Grazie e buon lavoro! --Civvì (majadiliano) 19:56, 9 Oktoba 2021 (UTC)[jibu]

Makala za ufutaji[hariri chanzo]

Mzee mwenzangu, nisipokosei ulipendekeza makala kadhaa zifutwe, Ila usipopeleka makala hizo kwenye ukurasa wake Wikipedia:Makala kwa ufutaji zitasahauliwa! Kipala (majadiliano) 21:38, 28 Novemba 2021 (UTC)[jibu]

Ndiyo, najua, lakini siku hizi tunafanya kazi kwa wasiwasi: umeme unakatika muda wowote kwa saa nyingi! Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 06:03, 29 Novemba 2021 (UTC)[jibu]

BwanaHeri[hariri chanzo]

Asante kwa salamu, nimeiunda kama akaunti mbadala; niliihitaji leo nilitaka kutunga maelezo jinsi ya kujiandikisha kwa matumizi ya barua pepe, na hapo nilihitaji kutumia akaunti mpya ili niweza kuona hatua. Ukiangalia Wikipedia:Mwongozo (Kujisajili) naomba ukague maelezo chini na. 4) kama ni sahihi. Kipala (majadiliano) 09:27, 29 Novemba 2021 (UTC)[jibu]

Request translate article about Isabelle de Charrière (Q123386)[hariri chanzo]

Hello Riccardo Riccioni, Would you like to translate the article en:Isabelle de Charrière (Q123386) for the SW Wikipedia? That would be appreciated. Boss-well63 (majadiliano) 08:27, 20 Desemba 2021 (UTC)[jibu]

Marejeo[hariri chanzo]

Kama kuna kosa umeliona kwenye tasfiri, rekebisha na ujadili kwenye majadilano ya page husika, na utumie lugha ya upole. Asante. --Halidtz (majadiliano) 13:20, 25 Desemba 2021 (UTC)[jibu]

Interlingue[hariri chanzo]

Grazie per il benvenuto. Potresti aiutarmi ad aggiungere qualche informazione in più all'articolo su Interlingue, per favore? --Caro de Segeda (majadiliano) 12:34, 31 Desemba 2021 (UTC)[jibu]

How we will see unregistered users[hariri chanzo]

Hi!

You get this message because you are an admin on a Wikimedia wiki.

When someone edits a Wikimedia wiki without being logged in today, we show their IP address. As you may already know, we will not be able to do this in the future. This is a decision by the Wikimedia Foundation Legal department, because norms and regulations for privacy online have changed.

Instead of the IP we will show a masked identity. You as an admin will still be able to access the IP. There will also be a new user right for those who need to see the full IPs of unregistered users to fight vandalism, harassment and spam without being admins. Patrollers will also see part of the IP even without this user right. We are also working on better tools to help.

If you have not seen it before, you can read more on Meta. If you want to make sure you don’t miss technical changes on the Wikimedia wikis, you can subscribe to the weekly technical newsletter.

We have two suggested ways this identity could work. We would appreciate your feedback on which way you think would work best for you and your wiki, now and in the future. You can let us know on the talk page. You can write in your language. The suggestions were posted in October and we will decide after 17 January.

Thank you. /Johan (WMF)

18:19, 4 Januari 2022 (UTC)

Looking for French speakers[hariri chanzo]

Hello, Riccardo. I am looking for French speakers, especially French speakers from Africa who use mobile devices for editing. Do you know of anyone here at the Kiswahili Wikipedia who might be interested in talking to me? The goal is to make it easier for people using a smartphone to post on a talk page. You can see the current status on this page by clicking on this link: https://sw.wikipedia.org/wiki/Majadiliano_ya_mtumiaji:Riccardo_Riccioni?dtenable=1 – but it's still too hard, and it isn't available on the mobile site yet. Please let me know if you could recommend any editors who might be affected. Whatamidoing (WMF) (majadiliano) 20:28, 1 Februari 2022 (UTC)[jibu]

@SJ, @Kipala, @ChriKo, @Asterlegorch367, perhaps one of you knows an editor who might edit the French or Arabic Wikipedias from a smartphone. Whatamidoing (WMF) (majadiliano) 20:48, 1 Februari 2022 (UTC)[jibu]
No I don't know anyone.
Asterlegorch367 (majadiliano) 12:33, 11 Machi 2022 (UTC)[jibu]

Come stai?[hariri chanzo]

Carissimo Riccardo, Pace!

Come stai? Quì sembra che stiamo migliorando, da ieri non abbiamo più l'obbligo di mascherine all'aperto, anche se l'attenzione è sempre alta. Io e la mia famiglia stiamo bene.

Volevo chiederti un piccolo favore, quando avessi due minuti di tempo: potresti tradurmi in Swahili la didascalia della mia foto nella mia pagina personale? Grazie mille di tutto e buon fine settimana, a presto. Rei Momo (majadiliano) 23:20, 11 Februari 2022 (UTC)[jibu]

Grazie infinite, sempre (come diceva il mio amico trappista brasiliano frei Manù) em comunhão!!! Rei Momo (majadiliano) 13:57, 12 Februari 2022 (UTC)[jibu]

Global IP block exemption[hariri chanzo]

Hello, I saw your request o er at Kipala's talk page and I think there's one way to fix your problem. Since your IP has been blocked as an Open Proxy, it cannot be unblocked rather you can request Global IP block exemption. Email stewards@wikimedia.org . Include:

  • the IP mentioned in the error message you got
  • the username you use
  • why you need to use Tor or the Open Proxy

Hope this helps. Cheers --Synoman Barris (majadiliano) 18:53, 12 Februari 2022 (UTC)[jibu]

Incorrect block[hariri chanzo]

Hello. User:EthanGaming7640 undo vandalism. Please see his contributions. Thank you! AlPaD (majadiliano) 15:29, 17 Februari 2022 (UTC)[jibu]

Hiki ni kizuizi kisicho sahihi. Mtumiaji alikuwa akifanya uhariri mzuri. Tafadhali kagua. Asante. Griffinofwales (majadiliano) 15:41, 17 Februari 2022 (UTC)[jibu]
He has 1 edit only on this wikipedia which was absolutely destructive, inserting gibberish. Here we block indefinitely for such behaviour. Are you sockpuppets? Complain to Meta. Kipala (majadiliano) 20:05, 17 Februari 2022 (UTC)[jibu]
I am a former administrator with over 30,000 edits on multiple projects. If you look at the change, he was removing the gibberish. You can also see extensive work cross-wiki for his account. Griffinofwales (majadiliano) 18:56, 18 Februari 2022 (UTC)[jibu]
That seems to have been a mixup. He is unblocked, thanks for pointing to it. Kipala (majadiliano) 20:58, 18 Februari 2022 (UTC)[jibu]

Have you voted in the UCoC enforcement guidelines ratification?[hariri chanzo]

Hi! @Riccardo Riccioni:

The ratification voting process for the revised enforcement guidelines of the Universal Code of Conduct (UCoC) is now open! Voting commenced on SecurePoll on 7 March 2022 and will conclude on 21 March 2022. Please read more on the voter information and eligibility details.

Please vote and encourage other editors of Swahili Wikipedia to also vote.

Regards, Zuz (WMF) (majadiliano) 11:24, 11 Machi 2022 (UTC)[jibu]

asante @Riccardo Riccioni sana kwa Marekebisho yako kwenye makala ninazo edit maan mimi bado ni mwanafunzi mchanga kabsa bashukuru sana najifunza kila unapo nirekebisha tuwasiliane kwa barua pepe Ceasar255 (majadiliano) 18:52, 2 Aprili 2022 (UTC)[jibu]

Msaada wa utengenezaji wa (infobox:football biografy)[hariri chanzo]

Salaam nimeona wewe ni mtaalamu naomba unisaidie kutengeneza (kigezo:infobox) kwaajili ya makala za wachezaji nimeona kwenye wikipedia ya kingereza kwakweli inapendeza mfano kama hii (, https://en.wikipedia.org/wiki/Template:Infobox_football_biography ) amani,sana Hussein m mmbaga (majadiliano) 07:38, 22 Machi 2022 (UTC)[jibu]

Ndugu, ni kweli masanduku yanapendeza, ila mimi siyatengenezi kwa kuwa si mtaalamu zaidi. Umuulize Muddyb. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:41, 22 Machi 2022 (UTC)[jibu]
sawa sawa Hussein m mmbaga (majadiliano) 07:45, 22 Machi 2022 (UTC)[jibu]

Goodbye[hariri chanzo]

Hi Riccardo Riccioni, I'm going to block globally because I made the bad translations.--Martorellpedro (majadiliano) 19:18, 15 Mei 2022 (UTC)[jibu]

Riccardo sijui kuhariri (kuchangis) Kwa kutumia smartphone he nifanyeje??[hariri chanzo]

Learning Jr 10:51, 2 Juni 2022 (UTC)

Samahani, mimi hata simu sina... Sijui ufanyeje. Umuulize mkabidhi mwingine yeyote. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 07:23, 3 Juni 2022 (UTC)[jibu]
Naona kuhariri kwa simu itakuwa changamoto kwa wengi, pia kwake Tomson G Wiston. Nikiangalia swali lake, tayari ameshakosea mara 2 tahajia ("kuchangis" badala ya "kuchangia"; "he" badala ya "je"). Si rahisi kuharir vema ukiwa na simu tu. Hakika asijaribu matini ndefu. Menginevyo anahitaji tu nafasi ya kujiunga na intaneti, simu janja halafu aingie sw.m.wikipedia.org na kuhariri. Kipala (majadiliano) 18:37, 3 Juni 2022 (UTC)[jibu]

Unda ukurasa Parvej Husen Talukder. Parvej Husen Talukder ni mshairi na mwandishi wa Bangladeshi. Rnwiki-global (majadiliano) 00:48, 16 Juni 2022 (UTC)[jibu]

Manii na shahawa[hariri chanzo]

Riccardo salaam. Umeshasoma toleo la mwisho la makala kuhusu shahawa? Nilitaka kupea shahawa ufafanuzi tofauti kwa manii. ChriKo (majadiliano) 13:36, 21 Juni 2022 (UTC)[jibu]

Salamu nyingi kwako! Natumaini unazidi kupona. Ndiyo, nimeona jaribio lako, lakini sijaelewa tofauti iko wapi. Nimeangalia kamusi mbalimbali, zinaonyesha ni visawe. Amani kwa wote! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 08:38, 22 Juni 2022 (UTC)[jibu]
Asante. Ninaendelea kupona. Shida tatu zimeisha, lakini moja inabaki. Ni kweli kama kamusi nyingi zinasema kwamba maneno haya ni visawe. Lakini Kamusi sanifu ya Biolojia, Fizikia na Kemia inapendelea manii kwa sperm na shahawa kwa semen. Sperm na semen ni tofauti. Amani kwako! ChriKo (majadiliano) 11:21, 22 Juni 2022 (UTC)[jibu]
ni kwanini nikiweka biography yangu @Riccardo Riccioni anai futa? wakati sijakosea chochote Jamespromax (majadiliano) 14:52, 14 Julai 2022 (UTC)[jibu]

Ukurasa wa Sigebert III[hariri chanzo]

Habari ndugu,

Nimejaribu kupitia makala ya Sigebert na kuona makala iliyoandikwa haikuwa na uwiano na makala ya kiingereza. Nimejaribu kuirekebisha waweza kuipitia na kuona ilivyo sasa. Katika jina la makala pia naona ulikosea (au ndo ilivyo?).

Amani kwako. MagoTech Tanzania (majadiliano) 15:52, 25 Julai 2022 (UTC)[jibu]

Ukarasa wa majadiliano wa "Katimawan2005"[hariri chanzo]

Habari ndugu Riccardo,

Samahani ninaomba msaada kwenye ukurasa wa mtumiaji "Katimawan2005" uweze kuupitia na kufuta kili nilichochapisha kimakosa wakati ninamtumia salaam ya ukaribisho kwenye wikipedia ya kiswahili, kama ndugu "Kipala" alivyosema kule kwenye group la telegram kuwa hata sisi ambao sio wakabidhi tutoe msaada kwenye kutuma salaam ya ukaribisho kwa kila mtumiaji aliejiunga na Wikipedia ya kiswahili ambaye alikua bado hajapokea salam hiyo.

Asante. Anuary Rajabu (majadiliano) 07:38, 7 Agosti 2022 (UTC)[jibu]

Sioni shida yoyote kwa sasa. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:05, 7 Agosti 2022 (UTC)[jibu]
Asante sana naona umeshakuwa sawa ndio. Anuary Rajabu (majadiliano) 08:12, 8 Agosti 2022 (UTC)[jibu]

Msaada wa kuandika Makala ya Mtandao wa jamiiTalk na Mwanzilishi wake[hariri chanzo]

Habari Wana Wikia kama kuna yeyote wa kuwekeza kuandika makala ya Mtandao wa jamiiTalk na Mwanzilishi wake asaidie. Kwa Maswali zaidi nashauri kumuulize Mwanzilishi wake kwenye Akaunti yake ya JamiiTalk

Seronera[hariri chanzo]

Riccardo Hi!
I would like to ask you the following: Could [[3]] it be by any chance the same with Seronera (under a different name)? My guess is, that it is most likely the same place (Serengeti National Park cannot have many populated areas within the park).
Asante sana - With kindest regards! --Aristo Class (majadiliano) 20:24, 18 Agosti 2022 (UTC)[jibu]

Nyegere[hariri chanzo]

Riccardo, habari yako? Je, ungependa kuangalia makala ya Nyegere? Mtu fulani amechangia maandishi ambayo yanaonekana kwangu kama hadithi za kitamaduni. Kwa hivyo nimeweka hii kama kichwa. Kitu kingine ni kwamba siwezi kupata maneno kadhaa katika kanusi yoyote, ingawa Google Translate inaleta tafsiri inayokubalika. Kwa mfano, maana ya kulina na kujambia ni nini? Google inatafsiri ile ya kwanza kwa kuwa na/kumiliki na ile nyingine kwa kuambia. Maandishi hayo yana maana kamili kwako? ChriKo (majadiliano) 07:31, 19 Agosti 2022 (UTC)[jibu]

Hayo maneno mawili si ya kawaida, labda kwenu Kenya... Kuhusu nyegere naenda kupitia makala hiyo. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:08, 22 Agosti 2022 (UTC)[jibu]
Asante sana. Nilipaswa kufikiria kubadilisha l kwa r ili kupata "rina". Lakini uliacha "jambia". Maanake ni nini? Alitumia nomino kama kitenzi? Amani kwako pia. ChriKo (majadiliano) 18:27, 22 Agosti 2022 (UTC)[jibu]
Wameniambia kwamba kujambia linatumika mitaani kwa maana ya kudakia, kukamata, kushika. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 05:55, 23 Agosti 2022 (UTC)[jibu]

Habari, ulimkaribisha. Nahisi ni yeye yule Mtumiaji:Justin yav sony0 uliyemwahi kuzuia tarehe 28.07. Ana na akaunti nyingine mtumiaji:Justin yav sony (sony). Kipala (majadiliano) 16:11, 4 Septemba 2022 (UTC)[jibu]

Tufanye jaribio[hariri chanzo]

Habari

naomba tufanye jaribio la mawasiliano kabla ya Jumamosi. Ninapenda kutumia programu ya Zoom. Hapa natuma link na wewe unabofya tu. Tutaona kama mikrofoni kwenye kompyuta yako itafanya kazi ipasavyo.

Napanga sasa mikutano mawili, maana sijui wewe utakuwa na nafasi leo au kesho na saa ngapi. Napanga leo saa 10 na kesho saa 4. Tafadhali unijibu utakuwepo tayari saa ngapi.

LEO Jumatatu saa 10

Thema: jaribio 1 Uhrzeit: 5.Sept. 2022 04:00 PM Nairobi Zoom-Meeting beitreten https://us05web.zoom.us/j/82223084212?pwd=MEJpdmdGTjgvS2Nvd2U0S1ZwUzJ1dz09 Meeting-ID: 822 2308 4212 Kenncode: u7fvxz

(Sijui kama unahitaji msimbo wa Kenncode...)

Kesho Jumanne saa 4 asubuhi Thema: Mein Meeting Uhrzeit: 6.Sept. 2022 10:00 AM Nairobi

Zoom-Meeting beitreten https://us05web.zoom.us/j/87027674202?pwd=T1o2NlBJQTdxVDRobmpLNmw5Lys4UT09

Meeting-ID: 870 2767 4202 Kenncode: v1tsZM

Kipala (majadiliano) 10:40, 5 Septemba 2022 (UTC)[jibu]

Mito Volta[hariri chanzo]

Habari yako, Riccardo? Niliona ulihamisha makala kuhusu mito Volta ili yapate majina kwa Kishahili. Lakini nafikiri ni bora kuiita Volta Mweupe na Volta Mweusi, kwa sababu hiyo inalingana na ngeli ya neno mto. Vile vile, tunasema: Ujerumani inapakana na Uholanzi, kwa sababu nchi ni ngeli ya n-. Unasemaje? ChriKo (majadiliano) 20:27, 14 Septemba 2022 (UTC)[jibu]

Salaam, ChriKo! Nilifurahi kukuona Jumamosi... Kuhusu majina hayo, nadhani inawezekana kufuata ngeli ya mto na nchi au kufuata jina la mto au nchi husika. Mpaka nimekuta katika kamusi fulani "Ulaya wa Magharibi". Nimeshaambiwa na mwingine nisiandike "Urusi una...", lakini nakuta sehemu nyingine matumizi ya namna hiyo, kwa mfano "Yerusalemu ya mbinguni". Kwa vyovyote, tukibadilisha kuhusu Volta, lazima tufanye vilevile kwa Nile n.k. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 06:54, 15 Septemba 2022 (UTC)[jibu]

Asante kwa kuchangia kuhusu Mateso ya Wakristo. Tatizo ukichangia haraka wakati makala bado inaandikwa, sijui tufanye nini . . . Maana mimi huhifadhi mara kwa mara , naogopa kukatwa umeme na kupoteza maudhui. Hivyo nahifadhi, naendelea kujisomea naendelea kuhariri na kuongeza. Nakupongeza kuchangia haraka, ila haraka2 = baraka-3 . Samahani, nachoka sasa, hivyo nitahifadhi hali yangu kwangu, tafadhali uangalie na kuunganisha. Ona hapa Mtumiaji:Kipala/Mateso_ya_Wakristo#Mateso_chini_ya_Decius_na_Valerian

(napanga kuendelea, lakini kwanza naomba uunganishe) Kipala (majadiliano) 18:52, 19 Oktoba 2022 (UTC)[jibu]

Pole sana. Nimeunganisha. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 06:43, 20 Oktoba 2022 (UTC)[jibu]

Tafadhali nisaidie[hariri chanzo]

Tafadhali zuia aina ya IP 147.158.0.0/16 kwa sababu ilitumika kuongeza taarifa ghushi kwenye miradi ya Wikimedia kama imeonyeshwa kama hii..... asante....... 36.76.6.84 11:10, 21 Novemba 2022 (UTC)[jibu]

Simodmart (mwanamuziki)[hariri chanzo]

Simodmart (mwanamuziki) Habari, ninataka kuibadilisha iwe Kifaransa na Kiingereza @Riccardo Riccioni MHMD DM1 (majadiliano) 01:28, 27 Novemba 2022 (UTC)[jibu]

Majira ya joto[hariri chanzo]

Riccardo salaam. Ulianzia makala Majira ya joto, lakini Muddyb aliandika makala kuhusu mada hiyo hiyo yenye kichwa Kipindi cha Kiangazi. Kwa maoni yangu kiangazi haiwezi kutumiwa kurejezea "summer". Unakubali? Misimu katika kando za wastani ni tofauti na ile ya ukanda wa tropiki, kwa hivyo inapaswa kuwa na majina tofauti. Kwa kanda za wastani, tunaweza kutumia majina uliyopendekeza. Kwa ukanda wa tropiki, napendekeza kiangazi kwa msimu wa ukame na masika kwa msimu wa mvua. Ambapo kuna misimu miwili ya mvua kwa mwaka, tutatumia mvuli kwa msimu mfupi wa mvua na kifuku kwa msimu mrefu wa mvua. Unaonaje? ChriKo (majadiliano) 07:32, 19 Desemba 2022 (UTC)[jibu]

Ndugu, kweli majira 4 ya Ulaya hayalingani na majira ya Afrika Mashariki. Ndiyo sababu tulitunga makala juu ya summer ya Wazungu na na juu ya kiangazi kwa Waafrika. Kuhusu mapendekezo yako mapya, sioni tofauti kati ya masika na kifuku: kwangu ni kitu kimoja ambacho pamoja na vuli vinaunda msimu wa mvua. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:06, 19 Desemba 2022 (UTC)[jibu]
Sawasawa ndugu, lakini hii makala juu ya kiangazi ni gani? Ile ya Muddyb inaelezea majira ya joto ya kanda za wastani. Sioni makala ingine kuhusu kiangazi. Hata masika, kifuku na mvuli sioni. ChriKo (majadiliano) 14:04, 19 Desemba 2022 (UTC)[jibu]
Kweli. Naona tubadilishe ukurasa wa Muddyb uhusu tu mazingira yetu, halafu tuongeze nyingine kuhusu misimu hiyo (ila jina ni vuli, si mvuli). --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:34, 19 Desemba 2022 (UTC).[jibu]

About Recently deleted articles[hariri chanzo]

kwa nini ulifuta nakala zangu zote mbili kutoka kwa Wikipedia naweza kujua sababu na ikiwa ninafanya chochote kibaya unaweza kunielekeza nawezaje kurekebisha makosa yangu HAAN BHAI ABHI (majadiliano) 11:21, 6 Februari 2023 (UTC)[jibu]

Jibu kutoka Ingo Koll, [07/02/2023 11:33] tahadhari: Nimetambua majaribio kadhaa za kuanzisha makala za wajasiriamali kutoka nchi mbalimbali zinazopewa makala kwenye swwiki. Ninahisi kuna mtu / kampuni inayolipwa ikijaribu kuingiza watu wasio na umaarufu katika wikipedia kupitia swwiki. Kama mtu kutoka nchi ya mbali anapata makala kwenye swwwiki lakini hakuna makala enwiki au penginepo, ni dalili yule si maarufu. Nimeona vyanzo ukichungulia ni tovuti za wenyewe au taarifa katika blogu zinazoonekana zinatoa taarifa kwa malipo kwa watu kujipromote. naona sawa tukifuta. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:10, 7 Februari 2023 (UTC)[jibu]

Asante! Chalcedon[hariri chanzo]

Shikamoo, Riccardo Riccioni.

Asante kwa kusahihisha makosa yangu kwenye Chalcedon. Sasa ninaanza kufundisha theolojia katika Kiswahili katika Tanzania, kwa hiyo natumaini - Mungu akipenda - nitaweza kuendelea kuandika zaidi katika sw.wikipedia.org

Nina swali. Unafikiri nafsi ni tafsiri nzuri ya hypostasis? Kama unavyojua, Wakristo wanaamini kwamba Yesu alikuwa mwanadamu kamili, kutia ndani nafsi ya kibinadamu. Kwa hivyo nina wasiwasi kwamba kwa kusema kwamba kwa kutafsiri 'Yesu ni hypostasis moja na umungu na ubinadamu' kuwa 'Yesu ni nafsi moja yenye umungu na ubinadamu' itamaanisha kwamba watu wanafikiri kwamba Yesu ana nafsi ya kimungu inayokaa ndani ya mwili wa mwanadamu. Hili ni tatizo katika kila lugha! TeolojiayaKiswahili (majadiliano) 08:42, 15 Februari 2023 (UTC)[jibu]

Ndugu, sijajua lugha mama yako ni ipi, na unatumia Kiswahili tangu lini. Kwa jumla nakushauri usijaribu kubadilisha haraka msamiati wa teolojia. Umefanya vizuri kuniuliza mimi ninayefundisha teolojia kwa Kiswahili tangu miaka mingi, kwa sauti na kwa maandishi kama hayo ya Wikipedia. Nimejitahidi kuwa sahihi kadiri iwezekanavyo kwa kulinganisha lugha asili na lugha ya taifa. Kuhusu swali lako, nafsi ni neno sahihi zaidi. Kweli Yesu ni mmoja tu, ni nafsi moja, ile ya Kimungu ya Mwanapekee wa milele, iliyotwaa mwili kwa maana ya utu kamili, ukiwa pamoja na roho (akili na utashi), si mwili tu, lakini haikutwaa nafsi ya kibinadamu la sivyo wangekuwa wawili kama alivyodhani Nestori. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:13, 15 Februari 2023 (UTC)[jibu]
Asante, Baba! Nitafanya kama unavyosema, na nitatumia 'nafsi'. Kwa hati za kanisa, ninajaribu kutumia tafsiri za watu wengine. Kwa mfano, Kitabu cha Sala (Mimi ni Padre wa Anglikana) kina Imani ya Nicene, Imani ya Athanasio Mtakatifu, n.k. Lakini sikuweza kupata tafsiri ya kitu chochote kutoka kwa Chalcedon, hivyo niliitafsiri mwenyewe na kuiweka mtandaoni ili itumike. . Ikiwa sikuwa na uhakika juu ya neno moja, niliandika Kigiriki na Kiingereza pia. Ninafurahi sana kwamba umeboresha tafsiri ili kuifanya ipatikane kwangu na kwa wengine. Nina mengi ya kujifunza. Nilianza tu kujifunza Kiswahili mwezi wa tisa mwaka jana, na lugha mama yangu ni Kiingereza. Mungu akubariki! TeolojiayaKiswahili (majadiliano) 11:29, 15 Februari 2023 (UTC)[jibu]

Konstantinos Tsimikas[hariri chanzo]

Nmeona kwenye makala hii https://sw.wikipedia.org/wiki/Konstantinos_Tsimikas nliyoiandika uliondoa Jamii ya Liverpool ningependa kujua ni kwanini? Ilinisirudie makosa hayo hayo katika makala nyingine Husseyn Issa (majadiliano) 12:17, 15 Machi 2023 (UTC)[jibu]

Kwanza hongera kwa juhudi zako. Pia kwa kupenda kujua zaidi ili kufanya vizuri. Nimeondoa jamii hiyo katika wachezaji wa timu hiyo kwa sababu [[Jamii:Liverpool]] inahusu mji huo, si timu. Labda uanzishe jamii mpya kama zile za timu za Manchester: [[Jamii:Wachezaji mpira wa Liverpool F.C.]]. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:23, 15 Machi 2023 (UTC)[jibu]
Ahsante sana,nitajaribu hivyo.

Husseyn Issa (majadiliano) 00:06, 18 Machi 2023 (UTC)[jibu]

Pamoko LGBTQ[hariri chanzo]

Hello, ningependa kufahamu kwanini ukurasa wetu sisi wanachama wa LGBT umefutwa. Je, pengine inaweza kuwa ni unyanyasaji kwetu sisi wanachama wa LGBT? Au tunakandamizwa kwa namna moja ama nyingine? Mister Way (majadiliano) 14:10, 6 Aprili 2023 (UTC)[jibu]

Nilivyoandika tayari, sababu ya kufuta ukurasa wako ni kwamba ulikuwa tangazo binafsi. Si ajabu kwamba ni mchango wako wa kwanza na kwamba ukurasa kama huo haupo katika Wikipedia ya lugha nyingine. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:32, 7 Aprili 2023 (UTC)[jibu]
Asante sana kwa ufafanuzi wako wa kina, nime elewa vyema. Ni kweli kuwa ukurasa ulikuwa mbegu. Asante sana. Mister Way (majadiliano) 17:45, 8 Aprili 2023 (UTC)[jibu]

Programu ya unasaji wa makala mpya[hariri chanzo]

Shikamoo ndugu Riccardo, ningependa kujua kama kuna programu inayotumika kujua makala zilizo anzishwa ama kuhaririwa hivi karibuni? Nimeona mara nyingi ukurasa wa mabadiliko ya karibuni mara nyingi unaweza usione vizuri kwakuwa kunakuwepo na matukio mengi. Kwa maarifa yangu nimeona kuna programu ya kuona waandishi wapya waliofungua akaunti zao punde na hata muda kidogo uliopita ambapo tumekuwa tukitumia programu hii https://sw.wikipedia.org/wiki/Maalum:Kumbukumbu/newusers pia kama njia rahisi ya kuona na kuwakaribisha ndugu zetu wageni katika uandishi wa makala,hivyo ningependa kujua kama kuna programu katika kupata makala mpya zilizo zanzishwa hivi karibuni na muda mrefu uliopita pia? Husseyn Issa (majadiliano) 09:39, 20 Mei 2023 (UTC)[jibu]

Naona list of abbreviations upande wa juu wa ukurasa wa mabadiliko ya karibuni. Kati yake kuna link na orodha ya kurasa mpya. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:40, 20 Mei 2023 (UTC)[jibu]
Ahsante sana bwana @Riccardo Riccioni Husseyn Issa (majadiliano) 18:36, 21 Mei 2023 (UTC)[jibu]

Namna ya kutengeneza vigezo na infobox[hariri chanzo]

Habari ndugu @Riccardo Riccioni natumaini uko salama, Ninaomba kujua kama unaweza kunifundisha namna ya kutengeneza infobox na vigezo kadhaa kwasababu nimeona watu wengi wanapata changamoto ya kuweka infobox na wamekua wakitumia Databox ambayo inaleta taarifa ambazo sio sahihi. Asante Justine Msechu (majadiliano) 08:01, 2 Julai 2023 (UTC)[jibu]

Ndugu, kwa kweli mimi mwenyewe sielewi, ndiyo sababu situmii hizo infobox. Anayeelewa zaidi ni Mtumiaji:Muddyb. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:54, 2 Julai 2023 (UTC)[jibu]
Naona imeanza editathon nyingine, na kama kawaida makosa ni yaleyale... Wote wanaoshughulikia viumbehai wanapangwa katika jamii:Mazingira!!! Hao ni watu, wawekwe kwenye jamii za watu, kwa mfano Jamii:wanaharakati wa Kanada. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:58, 2 Julai 2023 (UTC)[jibu]

UFUTAJI WA MAKALA[hariri chanzo]

kwa nini makala niliyochangia ya "shule ya sekondari ya Minaki " imefutwa na RICCARDO RICCION? Jr 13:41, 11 Julai 2023 (UTC)

Ndugu, kwanza salamu zako! Kuhusu kufuta ukurasa huo ni kwa sababu hujaweza kueleza shule hiyo ina upekee gani hata ikapata makala katika kamusi elezo. Kwa sababu hiyohiyo ilifutwa makala juu ya shule yako ya zamani Alfagems. Usikate tamaa kuchangia Wikipedia yetu! Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:23, 12 Julai 2023 (UTC)[jibu]

You have been a medical translators within Wikipedia. We have recently relaunched our efforts and invite you to join the new process. Let me know if you have questions. Best Doc James (talk · contribs · email) 12:34, 13 August 2023 (UTC)

Richiesta di sblocco dell'utente LR0725[hariri chanzo]

Ciao. Riccardo Riccioni

Sono Lee Kang-cheol, l'amministratore della Wikipedia in coreano.

Si è verificato un errore nel bloccare LR0725. LR0725 è l'amministratore della Wikipedia in coreano. Inoltre, detiene i diritti su molti altri progetti.

Condivido di seguito l'elenco degli account globali per la versione italiana.


It:Speciale:UtenzaGlobale/LR0725


hello. Riccardo Riccioni

I am Lee Kang-cheol, the administrator of the Korean Wikipedia.

There was an error in blocking LR0725. LR0725 is the admin of the Korean Wikipedia. Additionally, he holds rights to several other projects.

I share the global account list for the Italian version above.

--이강철 (majadiliano) 16:04, 8 Septemba 2023 (UTC)[jibu]

I came here to say the exact same thing. Please unblock LR0725; the block seems to be in error. They are a trusted crosswiki vandalfighter who is a sysop on kowiki and a global rollbacker. Prodraxis (majadiliano) 16:10, 8 Septemba 2023 (UTC)[jibu]

Salamu Riccardo Riccioni! Tafadhali ondoa Utawala, IA, Haki za Mtayarishaji Akaunti na Urasimi.

Ndugu yetu, Kipala, alifariki miezi michache iliyopita na kifo chake kimekuwa hasara kubwa kwa kikundi chetu cha Jumuiya ya Wikipedia ya Kiswahili. Asante. -- Tumbuka Arch 08:07, 19 Septemba 2023 (UTC)[jibu]

Akaunti yake imefungwa kwa matumizi yoyote yale. Ni global lock. Hivyo haina madhara. Hata hivyo, nitafikisha salamu hizi kule Meta. Asante sana!--Muddyb Mwanaharakati Longa 14:04, 19 Septemba 2023 (UTC)[jibu]

Adhabu kali kwa DigitalTanzania[hariri chanzo]

Wakati nikifikiria kutoa adhabu kali kwa mtajwa hapo juu, nimekuta amepigwa spana mbili mfululizo. Ya wiki, baada ya kutambua usumbufu wake, ukapiga ya milele. Nimefurahi mno. Huwezi kutoka huko ukaja kuchukua credit za watu waliofanya kazi miaka tele kwa maneno mawili. Hongera sana. Hapa si mahali pa kujipaia sifa za kijinga. Akitaka hizo sifa aende kwao. Asifunguliwe kabisa. Muddyb Mwanaharakati Longa 19:37, 21 Septemba 2023 (UTC) [jibu]

Tool that condenses references[hariri chanzo]

We have this tool that condenses references. But it takes a few hours before it runs. Pertaining to this article Kukosa usingizi Best Doc James (talk · contribs · email) 00:23, 24 Oktoba 2023 (UTC)[jibu]

Thanks for the information. Your infobox, however, is English only. What to do? Peace to you! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:22, 24 Oktoba 2023 (UTC)[jibu]

Carissimo pe Riccardo, Pace!

Per favore, daresti un'occhiata a questa nuova pagina che ho appena aperto quì? Ci sarebbero un paio di parole che ho lasciato in Inglese, per favore potresti tradurle tu? Quando avessi bisogno per il Francese o il Portoghese, ci sono!

Buona domenica Rei Momo (majadiliano) 15:56, 2 Desemba 2023 (UTC)[jibu]

Bravissimo, grazie mille!!! A presto Rei Momo (majadiliano) 13:36, 3 Desemba 2023 (UTC)[jibu]

Mvutano au uvutano?[hariri chanzo]

Mambo, nadhania tubadilishe jina la makala ya "mvutano" kuwa "uvutano". Nikitafuta maneno haya mawili katika google, inaonekana kuwa "mvutano" hutumiwa ili kumaanisha vita, harakati, n.k. Lakini, "uvutano" hutumiwa kama "gravity" kwa kawaida zaidi (makala za BBC ni mfano mzuri wa hivyo). Kwa hiyo, nadhania "uvutano" ni jina bora la makala hii. Siwezi kuhamisha ukurasa kwenye "Uvutano" (tayari kuna ukurasa wenye jina hili). Ungweza kufanya hiyo? Asante sana Kisare (majadiliano) 06:27, 10 Desemba 2023 (UTC)[jibu]

GuyanI ya Kifaransa au GuyanA ya Kifaransa[hariri chanzo]

Habari !

Ninatoka Guyani ya Kifaransa, ninazungumza lugha ya Kifaransa, Kiingereza na Kikrioli ya Guyani ya Kifaransa.

Nilitaka kukuambia tu kwamba nadhani ni muhimu kuashiria tofauti katika jina la Guyana ya Kifaransa na nchi ya Guyana katika lugha ya Kiswahili kwa sababu tofauti hii ipo katika lugha nyingine zinazozungumzwa katika eneo kama vile Kifaransa, Kiingereza na Kihispania...

kwa mfano:

Kwa hivyo, nadhani "i" badala ya "a", mwishoni mwa neno: GuyanA (ya Kifaransa) ni bora kutofautisha Guyana na nyingine...! PouLagwiyann (majadiliano) 16:19, 4 Januari 2024 (UTC)[jibu]

Ndugu, baada ya kutoa pendekezo hilo ulitakiwa kusubiri jibu, kumbe umebadilisha makala na jamii kadhaa... Si utaratibu mzuri katika Wikipedia. Ni kama kulazimisha. Tena sijui kama unamudu Kiswahili. Kwa mfano, hakuna neno Kikrioli, ila Krioli. Inawezekana pia kusema Kiguyani cha Kifaransa. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 10:32, 5 Januari 2024 (UTC)[jibu]

Unaogopa nini?[hariri chanzo]

Ikiwa neno halipo katika Kiswahili, tutengeneze au turekebishe neno kutoka lugha nyingine, kama Kiswahili na lugha zote za dunia tayari zimefanya...

Kukaa hapa, kutofanya lolote na kulia kwa kukosa neno uswahilini kunatufanya turudi nyuma hatua mbili tatu na kutoendelea. kinachofanya lugha kuwa hai ni kwamba anabadilika kwa kuunda au kuazima baadhi ya maneno kutoka lugha nyingine. Kiswahili ni lugha hai sio mfu ambayo inaogopa sana wawili kukopa wengine dunia mbili inabadilika... Kwa hivyo sioni ni nini kigumu kwako hapa.

Na katika Guyani ya Kifaransa, tuna njia yetu wenyewe ya kuzungumza Kifaransa, sio sawa na Paris na kikrioli yetu pia kwa hivyo hatuwezi kuiita Krioli yetu "guyani cha kifaransa" kama ulivyosema kwa sababu inawakilisha lugha yetu ya Kifaransa tunayozungumza hivyo sisi. Unahitaji jina lingine la krioli ya guyani ya kifaransa.

Na nazungumza Kiswahili lakini si 100% bali zaidi kama 50/60%. Lakini Kiingereza changu, Kifaransa na Kikrioli cha Guyani ya Kifaransa ziko kwenye uhakika. PouLagwiyann (majadiliano) 14:31, 5 Januari 2024 (UTC)[jibu]