Kariakoo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Kata ya Kariakoo
Kata ya Kariakoo is located in Tanzania
Kata ya Kariakoo
Kata ya Kariakoo

Mahali pa Kariakoo katika Tanzania

Majiranukta: 6°49′26″S 39°14′56″E / 6.82389°S 39.24889°E / -6.82389; 39.24889
Nchi Tanzania
Mkoa Dar es Salaam
Wilaya Ilala
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 10,246
Soko la Kariakoo

Kariakoo ni kata ya wilaya ya Ilala katika Mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania, yenye postikodi namba 11106.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 10,246 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 13,780 waishio humo.[2]

Kariakoo inajulikana kutokana na soko kubwa.

Asili ya jina[hariri | hariri chanzo]

Jina la eneo hili ni la kihistoria: linatokana na neno la Kiingereza "carrier corps", yaani kikosi cha wapagazi waliobeba mizigo ya jeshi wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.

Pande zote vitani walitumia malakhi ya wapagazi waliokodishwa au kulazimishwa kufanya huduma hii.

Baada ya vita wapagazi kadhaa walipewa maeneo ya kujenga nyumba kwenye miji mbalimbali na hivyo majina kama "Kariakoo" au "Kariokor" (Nairobi) yanapatikana katika miji mbalimbali ya Afrika ya Mashariki.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Kata za Wilaya ya Ilala - Tanzania

Bonyokwa | Buguruni | Buyuni | Chanika | Gerezani | Gongolamboto | Ilala | Jangwani | Kariakoo | Kimanga | Kinyerezi | Kipawa | Kipunguni | Kisukuru | Kisutu | Kitunda | Kivukoni | Kivule | Kiwalani | Liwiti | Majohe | Mchafukoge | Mchikichini | Minazi Mirefu | Mnyamani | Msongola | Mzinga | Pugu | Pugu Station | Segerea | Tabata | Ukonga | Upanga Magharibi | Upanga Mashariki | Vingunguti | Zingiziwa