Jumapili ya Utatu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Utatu Mtakatifu ulivyodokezwa katika mchoro wa Mt. Andrei Rublev.
Mwaka wa liturujia
Magharibi
Mashariki

Jumapili ya Utatu Mtakatifu ni sikukuu ya Ukristo inayoadhimishwa na madhehebu kadhaa, kama vile Kanisa Katoliki, ili kutukuza fumbo la Mungu aliye mmoja tu katika nafsi tatu kadiri ya imani iliyofafanuliwa na mitaguso ya kiekumene.

Kwa kawaida Wakristo wa magharibi huwa wanaadhimisha fumbo hilo Jumapili inayofuata Pentekoste, wakati wale wa mashariki wanaliadhimisha siku hiyohiyo ya Pentekoste, Roho Mtakatifu kulishukia Kanisa huko Yerusalemu ili kulihuisha na kuliongoza hadi ujio wa pili wa Yesu Kristo kutoka utukufu wa Mungu Baba.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jumapili ya Utatu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.