Gideoni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Gideoni alivyochorwa na Maarten van Heemskerck (1550 hivi).

Gideoni (kwa Kiebrania גדעון - Ghide'on) alikuwa mwana wa Yoas, wa kabila la Manase.

Mungu alimuita awe mwamuzi wa Israeli kwa miaka 40, kisha kukomboa sehemu kubwa ya nchi kutoka mikono ya Wamidiani kama kitabu cha Waamuzi (6-8) kinavyosimulia.

Kwa jinsi anavyosifiwa na Waraka kwa Waebrania, anaheshimiwa katika imani ya Wakristo wote ulimwenguni kama mtakatifu kulingana na ushuhuda wake katika kipindi chake cha kuwa mwamuzi wa Israeli.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 26 Septemba[1].

Maisha yake[hariri | hariri chanzo]

Alipoitwa na Mungu alijitetea kwa kusisitiza udogo na ufukara wake, lakini akajaliwa ishara zote alizoziomba ili kuhakikishiwa msaada (Amu 6:11-24,36-40).

Sura ya 7 inasimulia Mungu alivyopunguza askari wake ili ionekane wazi kuwa ushindi ni wa Mungu mwenyewe, hautegemei uhodari na wingi wa watu au silaha zao. Ni kawaida ya kazi ya Mungu kuonyesha uweza wake katika udhaifu wa binadamu.

Waisraeli walipotaka Gideoni awe mfalme wao, akakataa katakata ili Bwana tu aendelee kuwatawala (Amu 8:22-23), lakini wazo hilo likaendelea kuenea, ingawa wengine walilipinga (Amu 9:1-21).

Sala yake (Amu 6:15)[hariri | hariri chanzo]

"Ee Bwana, nitawaokoa Israeli kwa jinsi gani? Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu".

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Gideoni kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.