Samsoni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Samson akipigana na simba kadiri ya Lucas Cranach the Elder, 1525.
Samsoni kipofu kadiri ya Lovis Corinth, 1912.

Samsoni (kwa Kiebrania שִׁמְשׁוֹן, Shimshon, Šimšôn, "Mtu wa jua"[1]) alikuwa mmojawapo kati ya Waamuzi wa Biblia.

Kadiri ya Waamuzi 13-16 alikuwa wa kabila la Dan, alizaliwa na mwanamke tasa, akawa mnadhiri tangu achukuliwe mimba, akapewa nguvu ya ajabu kutokana na nadhiri hiyo, akapigana na Wafilisti hadi kifo chake alipowaua kwa pamoja wengi kuliko maisha yake yote[2].

Hadithi zake zinaonyesha kwamba alikuwa jitu lakini mwenye akili ya kitoto na tamaa nyingi ambazo hatimaye zilimponza.

Hata hivyo Waraka kwa Waebrania 11:32-34 unamsifu kwa imani yake iliyompa nguvu.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Van der Toorn, Karel; Pecking, Tom; van der Horst, Peter Willem (1999). Dictionary of Deities and Demons in the Bible. Wm. B. Eerdmans. p. 404. ISBN 9780802824912. 
  2. "The "Minor Judges"- A Re-evaluation". Alan J. Hauser. 1975. Retrieved 2015-03-27. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Samsoni kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.