Altare

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Altare iliyotengenezwa huko Poland kwa ajili ya ziara ya Papa Yohane Paulo II.
Altare ya Kibizanti huko Valaam.

Altare au madhabahu ni mahali patakatifu inapotolewa sadaka au ibada.

Mara nyingi altare inapatikana ndani ya hekalu au kanisa.

Katika dini nyingi kuna madhehebu ya kafara, dhabihu au matoleo kwa Mungu au mizimu. Ndiyo sababu panahitajika mahali pa kufaa.

Katika Ukristo altare inatiwa maanani kwa kiasi tofauti kulingana na imani ya madhehebu husika juu ya Ekaristi, iliyo ukumbusho wa sadaka pekee ya Yesu Kristo iliyotolewa msalabani.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.