Filomena wa Roma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Filomena katika kanisa kuu la Montauban.
Sanamu ya Mt. Filomena, kazi ya Johann Dominik Mahlknecht, Museum Gherdëina, huko Urtijëi, Italia.

Filomena wa Roma (10 Januari 291 - 10 Agosti 304) alikuwa bikira wa ukoo tawala wa Corfu (Ugiriki) ambaye alianza kuheshimika kama mtakatifu mfiadini baada ya masalia kupatikana mnamo Mei 1802 katika katakombu ya Priscilla, Roma, Italia. Paliandikwa Pax Tecum Filumena (yaani "Amani kwako, Filomena"). Kabla ya hapo hakujulikana, lakini baadaye heshima ya Wakatoliki na Waorthodoksi wengi kwake imestawi sana hadi leo sehemu nyingi za dunia ikisaidiwa na njozi na miujiza iliyotokea kwa kuomba sala zake.

Kati ya miaka 1837 na 1961 Kanisa Katoliki liliruhusu heshima hiyo katika liturujia pia.[1] Lakini wasiwasi wa wanahistoria umefanya jina lake liondolewe katika kalenda zote za watakatifu.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. 1920 typical edition of the Roman Missal, with feasts updated to the late 1920s Archived 1 Machi 2020 at the Wayback Machine., p. [214]: "11 August. St Philomena. Virgin and Martyr. Mass: Loquebar from the Common of Virgins, 1."

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.