Tulia Ackson
| Mheshimiwa Tulia Ackson Mbunge | |
Ackson mwaka 2024 | |
Rais wa 31 wa IPU na Spika wa 7 wa Bunge la Taifa la Tanzania | |
| Aliingia ofisini 1 Februari 2022 | |
| Rais | Samia Suluhu |
|---|---|
| mtangulizi | Job Ndugai |
Makamu wa Spika wa Bunge la Taifa la Tanzania | |
| Muda wa Utawala Novemba 2015 – 31 Januari 2022 | |
| Rais | John Magufuli |
| mtangulizi | Job Ndugai |
| aliyemfuata | Iddi Azzan |
Mbunge wa Bunge la Taifa la Tanzania | |
| Aliingia ofisini 19 Novemba 2015 | |
| mtangulizi | Anna Makinda |
Makamu wa 16 wa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania | |
| Muda wa Utawala 9 Septemba 2015 – 15 Novemba 2015 | |
| Rais | Jakaya Kikwete |
| mtangulizi | George Masaju |
Mbunge wa Bunge la Kwanza la Katiba la Tanzania | |
| Muda wa Utawala 18 Februari 2014 – 2 Oktoba 2014 | |
| Rais | Jakaya Kikwete |
| Appointed by | Jakaya Kikwete |
| tarehe ya kuzaliwa | 23 Novemba 1976 Bulyaga, Tukuyu, Rungwe, Mbeya, Tanzania |
| mhitimu wa | University of Dar es Salaam (LL.B) University of Dar es Salaam (LL.M) University of Cape Town (PhD) |
| Fani yake | Wakili |
| tovuti | https://www.agctz.go.tz/ |
Tulia Ackson (alizaliwa 23 Novemba 1976) ni mwanasheria na mwanasiasa Mtanzania mwanachama wa Chama cha kisiasa cha Chama cha Mapinduzi (CCM).
Tarehe 1 Februari 2022 alichaguliwa na wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa spika wa Bunge hilo. [1]
Historia na Elimu
[hariri | hariri chanzo]Ackson alizaliwa kwenye kata ya Bulyaga, Tukuyu, kwenye wilaya ya Rungwe. Alisoma shule huko Tukuyu Mbeya kuanzia mwaka 1984 hadi 1990, ambapo alipata Cheti cha Elimu ya Msingi. Baadaye alichaguliwa kujiunga na Shule ya Sekondari ya Wasichana Loleza huko Mbeya, ambapo alipata Cheti cha Elimu ya Sekondari mwaka 1994, na baadaye alipata Cheti cha Juu cha Elimu ya Sekondari katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Zanaki. Kisha alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1998, ambapo alipata shahada ya kwanza ya Sheria mwaka 2001. Ackson alihitimu na kupata shahada ya uzamili ya Sheria mwaka 2003. Mwaka 2004 alifanya mtihani wa upatikanaji wa leseni ya utetezi wa sheria (bar examinations) na kupata Cheti cha Mazoea ya Sheria nchini Tanzania. Mwaka 2005 alikubaliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Cape Town kwa masomo ya shahada ya uzamivu (PhD) na alipata shahada ya uzamivu katika Falsafa mwaka 2007.[2]
Kazi na Siasa
[hariri | hariri chanzo]Alirudi Dar es Salaam alipofundisha sheria kwenye chuo kikuu hadi mwaka 2014 alipoteuliwa na rais Jakaya Kikwete kuwa mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Mwaka 2015 alikuwa kati ya wabunge 10 walioteuliwa na rais John Magufuli kuingia bungeni kwa miaka 2015 – 2020.
Tulia Ackson kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amechaguliwa kuwa Rais wa 31 wa Umoja wa Mabaraza ya Kitaifa Duniani (IPU) na Baraza la Uongozi la IPU, chombo chake kikuu cha kufanya maamuzi kinachojumuisha wabunge kutoka duniani kote.
Anachukua nafasi hiyo kutoka kwa Duarte Pacheco, mbunge kutoka Ureno, ambaye alimaiza muda wake wa miaka mitatu mwishoni mwa Mkutano wa 147 wa IPU huko Luanda, Angola.
Baada ya kuchaguliwa, Ackson alisema: “Asanteni kwa imani mliyonipa kwa kunichagua. Ninasikiliza nafasi hii kwa unyenyekevu huku nikifahamu majukumu yote inayokuja nayo. Nawathibitishia azma yangu ya kufanya kazi pamoja nanyi kufanya IPU iwe taasisi yenye ufanisi zaidi, inayowajibika na inayoeleweka.”
Wabunge walipiga kura kwa siri. Kukiwa na wagombea wanne kwenye kura, Rais mpya wa IPU alichaguliwa kwa 57% ya kura baada ya duru moja ya upigaji kura.
Wabunge kutoka Mabaraza 130 ya IPU wanachama walishiriki katika uchaguzi huo. Kwa lengo la kukuza usawa wa jinsia, kila Baraza la IPU lilistahili kupiga kura tatu ikiwa na uwiano sawa wa jinsia. Vikundi vyenye wajumbe wa jinsia moja walistahili kura moja tu.
Kwa mara ya kwanza katika historia, wagombea wote wengine watatu kwenye kura – Adji Diarra Mergane Kanouté wa Senegal, Catherine Gotani Hara wa Malawi na Marwa Abdibashir Hagi wa Somalia – walikuwa wabunge wanawake kutoka Afrika.
Tulia Ackson ni mwanamke wa tatu tu kuwa Rais wa IPU baada ya Najma Heptulla wa India (1999–2002) na Gabriela Cuevas wa Mexico (2017–2020). Pia, yeye ni mwanamke wa kwanza kutoka Afrika kushikilia nafasi hiyo.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2022-02-01. Iliwekwa mnamo 2022-02-01.
- ↑ "task documents download". sheria.go.tz. Iliwekwa mnamo 2015-10-18.
| Makala hii kuhusu kuhusu mwanasiasa wa Tanzania bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Tulia Ackson kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |