Soko la Hisa la Nairobi(NSE) ndilo soko kuu la kuuza na kununua Hisa nchini Kenya. Lilianza mwaka wa 1954 kama Soko la Hisa la Ng'ambo wakati Kenya ilikuwa bado chini ya Ukoloni wa Uingereza kwa ruhusa ya Soko la Hisa la London. NSE ni mwanachama wa Shirikisho la Masoko ya Hisa ya Afrika.
Soko la Hisa la Nairobi ndilo la nne kwa ukubwa Afrika katika mtazamo wa idadi ya hisa zinazouzwa, na la tano katika Thamani ya Hisa zote kama asilimia ya Pato la Taifa.[1] Soko hili hufanya kazi kwa ushirikiano na Soko la Hisa la Uganda na Soko la Hisa la Dar-es-Salaam, pamoja na kusajili hisa mbalimbali katika masoko yote matatu.
Soko hili lina vikao vya kabla kati ya 09:00-09:30 na vikao vya biashara ya kawaida kati ya 09:30-03:00 siku zote za wiki isipokuwa Jumamosi, Jumapili na sikukuu zinazotangazwa na Soko mapema.[2]
Ofisi na sakafu ya biashara za NSE ziko katika jumba la Nation Centre katika baraste ya Kimathi. Biashara hufanywa kupitia Electronic Trading System (ETS) ambayo ilikamilika mwaka wa 2006. Mtandao wa Wide Area Network (WAN) uliwekwa mwaka wa 2007 na hili lilitupilia mbali haja ya Kampuni za kuuza na kununlia Hisa kuwapeleka mawakala wao (wafanyabiashara) kwenye ukumbi wa biashara ili kuuza au kununua hisa. Kwa sasa, shughuli za kununua na kuuza hufanywa kutoka ofisi zao kupitia mtandao wa WAN. Hata hivyo, baadhi ya mawakala bado wanaweza kufanya biashara kutoka sakafu ya NSE.
Fahirisi mbili hutumiwa kwa kawaida kupima utendaji. Ile ya NSE 20-Share Index imetumiwa tangu mwaka wa 1964 na hupima utendaji wa kampuni 20 bora zilizo na msimamo mzuri kifedha na ambazo zimezidi kurejesha matokeo mazuri ya kifedha mfululizo. Zilizojumuishwa katika fahirisi hii ni Kampuni ya Sukari ya Mumias, Express Kenya, Rea Vipingo, Sasini Tea, CMC Holdings, Kenya Airways, Safaricom, Nation Media Group, Barclays Bank Kenya, Equity Bank, Kenya Commercial Bank, Standard Chartered Bank, Bamburi Cement, British American Tobacco, Kengen, Centum Investment Company, East African Breweries, EA Cables, Kenya Power & Lighting Company Ltd na Athi River Mining. Fahirisi hii haswa hulenga mabadiliko ya bei ya makampuni haya 20.
Mwaka wa 2008, NSE All Share Index (NASI) ilianzishwa kama fahirisi mbadala. Kipimo chake ni kiashiria cha utendaji wa soko kwa jumla. Fahirisi hii hujumuisha hisa zote zilizouzwa au kununuliwa kila siku. Hivyo basi mtazamo wake ni utendaji kwa ujumla wa thamani ya hisa zote katika soko badala ya mabadiliko ya bei ya Hisa chache teule.
Hata hivyo kuna fahirisi nyingine ya tatu; AIG 27 Index ambayo hulinganishwa mabadiliko ya bei ya hisa za makampuni 27 ambazo zimetambuliwa kama zilizo imara kiasi. Wazo la msingi la fahirisi hii inalingana na ile ya NSE 20-Share Index. Lakini ilhali ile ya AIG imebainishwa na kampuni ya AIG (kampuni ya huduma za kifedha na sehemu ya AIG Group), ile ya NSE 20-share Index ni ya Soko la Hisa la Nairobi.
Magazeti, majarida,stesheni za redio na televisheni. Shirika la Safari za ndege la Kenya; limesajiliwa pia katika masoko ya Hisa ya Uganda, Rwanda na Dar es Salaam
SCAN
Scangroup
Utangazaji na utafutaji masoko
SGL
Standard Group Limited
Magazeti, majarida,stesheni za redio na televisheni
TPSE
TPS Serena
Huduma ya kuchangia Utalii; Hoteli na Maeneo ya Starehe
UCHM
Maduka ya Uchumi
Maduka; Uchumi limesajiliwa pia katika masoko ya Hisa ya Uganda, Rwanda na Dar es Salaam
Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Soko la Hisa la Nairobi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Makala African corporation or company bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari.