Martin de Porres

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha hii ya Martin des Porres iko katika monasteri ya Mt. Ann mjini Lima.

Martin de Porres (15793 Novemba 1639) alikuwa bradha wa Shirika la Wahubiri katika nchi ya Peru.

Akiwa mtoto chotara wa kabaila Mhispania Juan de Porres na binti mwenye asili ya Afrika Anna Velasquez hakutambuliwa na baba yake akalelewa na mama na kuwa msaidizi wa daktari akijifunza hivyo elimu ya matibabu.

Mwaka 1594 alijiunga na watawa Wadominiko akaendelea kuwaangalia wagonjwa wa matabaka na rangi zote.

Alikuwa na kipaji cha uponyaji ambacho kiliwasaida watu wengi. Kutokana na upendo aliowaonyesha watu wote aliheshimiwa sana na taarifa za uponyaji wa ajabu zilianza kuenea.

Mwaka 1837 alitangazwa mwenye heri na Papa Gregori XVI, halafu tarehe 6 Mei 1962 akatangazwa na Papa Yohane XXIII kuwa mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 3 Novemba kila mwaka[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • BENEDICTINE FATHERS – Rafiki Martin, Habari za Maisha ya Mtakatifu Martin De Porres O.P. – Kipigo Chapa cha Tano ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Peramiho 1990 – ISBN 9976-63-057-3

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.