Komba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Komba
Komba magharibi (Galago senegalensis)
Komba magharibi (Galago senegalensis)
Uainishaji wa kisayansi
Domeni: Eukaryota (Viumbe walio na seli zenye kiini)
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Primates (Wanyama wanaofanana kiasi na binadamu)
Nusuoda: Strepsirrhini (Wanyama wanaofanana zaidi na lemuri)
Oda ya chini: Lorisiformes (Wanyama kama poto)
Familia: Galagidae (Wanyama walio na mnasaba na komba)
Gray, 1825
Ngazi za chini

Jenasi 5:

Komba ni wanyama wadogo wa familia Galagidae. Wamo miongoni mwa wanyama wa asili wa jamaa ya binadamu. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara.

Hukiakia usiku na hulala mchana katika matundu ya miti. Kwa ajili hiyo wana macho makubwa ili kuona vizuri kwenye giza. Hata masikio yao ni makubwa ili kusikia mawindo yao na hata maadui wao. Mkia mrefu wao huzuia wasiyumbe wakitembea juu ya matawi. Wanaweza kuruka sana, hadi mita 2 kwa wima. Wana makucha kama yale ya watu, isipokuwa lile la kidole cha pili cha miguu ambao ni mrefu wenye ncha kali na hutumika kwa kusafisha manyoya. Hula wadudu, wanyama wadogo, matunda na sandarusi.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.