Kitabu cha Mika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Pitio kulingana na tarehe 21:34, 22 Aprili 2015 na Magioladitis (majadiliano | michango) (→‎Viungo vya nje: All info is kept in Wikidata, removed: {{Link FA|he}} using AWB (10903))

Kitabu cha Mika ni kimoja kati ya vitabu 12 vya Manabii wadogo ambavyo, pamoja na vingine vingi, vinaunda Tanakh.

Hivyo ni pia sehemu ya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo.

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Mwandishi na muda

Jina la nabii huyo, aliyefanya kazi wakati uleule wa nabii Isaya, mwishoni mwa karne ya 8 K.K., lina maana ya "Nani kama Mungu?".

Muhtasari

Kitabu kinaweza kuwaganyika sehemu nne ambamo vitisho na ahadi vinapokezana:

  • hukumu dhidi ya Israeli (Mik 1:2-3,12)
  • ahadi kwa Siyoni (Mik 4:1-5,14)
  • hukumu ya pili dhidi ya Israeli (Mik 6:1-7,7)
  • matumaini (Mik 7:8-20)

Dondoo maarufu

Tunavyosoma katika Injili ya Mathayo (2:1-6), dondoo la Mik 5:2 lilitumiwa na Wayahudi kutarajia ujio wa Masiya wa ukoo wa Mfalme Daudi kutoka Bethlehemu.

Dondoo lenyewe lilibainisha miaka 700 kabla ya Yesu kuzaliwa kwamba Bethlehemu hiyo ni ile ya Efrata, si nyingine yenye jina hilohilo: "Bali wewe, Betlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele".

Marejeo

  • Ben Zvi, Ehud (2000). Micah. Eerdmans. 
  • Coogan, Michael (2009). A Brief Introduction to the Old Testament. Oxford University Press. 
  • King, Phillip J (2006). HarperCollins Study Bible: Micah. Harper Collins Publishers. 
  • Limburg, James (1988). Hosea-Micah. Westminster John Knox Press. 
  • Mays, James L (1976). Micah. Westminster John Knox Press. 

Marejeo mengine

  • “Book of Micah.” The Anchor Bible Dictionary. Vol. 4, Editor-in-Chief: Freedman, David N. Doubleday; New York, NY. 1992.
  • “Book of Micah.” International Standard Bible Encyclopedia. General Editor: Bromley, G.W. William B. Erdmans Publishing Co.; Grand Rapids, MI. 1986.
  • Holy Bible: The New Oxford Annotated Bible. Coogan; Oxford University Press, 2007.
  • LaSor, William Sanford et al. Old Testament Survey: the Message, Form, and Background of the Old Testament. Grand Rapids: William B. Eerdmans, 1996.
  • Hailey, Homer. (1973). A Commentary on the Minor Prophets. Grand Rapids: Baker Book House.
  • Maxey, Al. THE MINOR PROPHETS: Micah. (n.d.). 20 Paragraphs. Retrieved 4 Oktoba 2005, from http://www.zianet.com/maxey/Proph11.htm
  • McKeating, Henry. (1971). The Books of AMOS, HOSEA, AND MICAH. New York: the Syndics of the Cambridge University Press.
  • Pusey, E. B. (1963). The Minor Prophets: A Commentary (Vol. II). Grand Rapids: Baker Book House.
  • Wood, Joyce Rilett. (2000). Speech and action in Micah’s prophecy. Catholic Biblical Quarterly, no. 4(62), 49 paragraphs. Retrieved 30 Septemba 2005, from OCLC (FirstSearch) database http://newfirstsearch.oclc.org

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.