Escherichia coli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Escherichia coli
Scientific classification
Domain: Bacteria
Phylum: Proteobacteria
Class: Gammaproteobacteria
Order: Enterobacteriales
Family: Enterobacteriaceae
Genus: Escherichia
Species: E. coli
Binomial name
Escherichia coli
(Migula 1895)
Castellani and Chalmers 1919
Synonyms

Bacillus coli communis Escherich 1885

Escherichia coli (kwa kawaida hufupisha kama E. coli, tamka: ɛʃɘˈrɪɣiɑ ˈkoʊli), ilipewa jina baada ya Theodor Escherich) ni bakteria yaGramu hasi yenye umbo la fimbo ambayo kwa kawaida hupatikana katika utumbowa chini wa viumbe damu moto (endothamu). Aina nyingi zaE. koli si hatari, lakini nyingine, kama vile serotaipu O157: H7, zinaweza kusababisha madhara makubwa ya sumu ya chakula katika binadamu, na mara kwa mara husababisha bidhaa kurejeshwa kwa watengenezaji.[1][2] Zile zisizo hatari ni sehemu ya kawaida ya viumbe vya utumbo, na zinaweza kufaidi wenyeji kwa kuzalisha vitamini K2,[3] na kwa kuzuia kuanzishwa kwa bakteria ya kusababisha magonjwa ndani ya utumbo.[4][5]

E. koli hazikai tu kwenye utumbo, na uwezo wao wa kuishi kwa muda mfupi nje ya mwili inazifanya viumbe viashiria halisi kupima sampuli za mazingira kwa ukolezi wa kinyesi.[6][7] Bakteria hii inaweza kukuzwa kwa urahisi na jeni yake ni rahisi na inaweza kufanywa kwa urahisi au kurudiwa kwa kupitia mchakato wa metajeni, na kuifanya moja ya viumbe vya prokarioti ambavyo mifano yao imetafitiwa sana, na aina muhimu katika teknolojia ya mimea na mikrobiolojia.

E. koli iligunduliwa na daktari wa watoto na mtafiti wa bakteria Mjerumani Theodor Escherich katika 1885,[6] na kwa sasa imeainishwa kama sehemu ya familia ya Enterobacteriaceae ya gamma proteobacteria[[.]][8]

Aina[hariri | hariri chanzo]

Mfano wa mfululizo wa mpasuko jozi katika E. koli

Aina ya E. koli ni kikundi kidogo ndani ya jamii hiyo ambacho kina sifa za kipekee ambazo zinaitofautisha kutokana aina nyingine za E. koli. Tofauti hizi mara nyingi huweza kuonekana tu katika ngazi ya Masi, hata hivyo, zinaweza kuleta mabadiliko katika fiziolojia au maisha ya bakteria hii. Kwa mfano, aina inaweza kupata uwezo kusababisha magonjwa, uwezo wa matumizi ya chanzo cha kipekee cha kaboni , uwezo wa kupambana na shubaka fulani ya kimazingira au uwezo wa kupinga mawakala wa kumaliza mikrobu. Aina mbalimbali za E. koli mara nyingi hutegemea kimelea, na kuifanya rahisi kujua chanzo cha Ukolezi wa kinyesi katika sampuli ya mazingira.[6][7] Kwa mfano, kujua aina ya E. koli iliopo katika sampuli ya maji inaruhusu kufanya uamuzi kuhusu asili ya ukolezi kama umetoka kutoka kwa binadamu, mamalia mwingine au ndege.

Aina mpya za E. koli hufuka kwa njia ya mchakato wa asili wa kibiolojia na kupitia mabadiliko ya jeni na kupitia uhamisho wa upande[9]. Baadhi ya aina huendeleza sifa ambazo zinaweza kudhuru mnyama kimelea. Aina hizi zenye madhara kawaida husababisha wimbi la kuhara ambayo ni kero katika watu wazima na mara nyingi ni hatari kwa afya ya watoto katika nchi zinazoendelea duniani. [10] Aina hatari zaidi, kama vile O157: H7 husababisha ugonjwa mkubwa ugonjwa au kifo kwa wazee, wachanga sana au wenye kinga dhoofu.[4][10]

Biolojia na biokemia[hariri | hariri chanzo]

E. koli ni Gramu-hasi, enerobu zinazozalisha ATP na zisizozalisha vijimbegu. Seli kwa kawaida huwa na umbo la fimbo na zina ukubwa wa karibu 2 Mikromita2 (μm) na kipenyo cha 0.5 μm , kwa kiasi cha kiini cha 0.6-0.7 μm 3.[11] Inaweza kuishi kwa aina mbalimbali ya nyenzo. E. koli inatumia kugandisha mchanganyiko-asidi katika hali anaerobiki, inayozalisha lakteti, susineti, ethanoli, asetati na kaboni dioksidi. Kwa vile njia nyingi katika kugandisha asidi-mchanganyiko huzalisha gesi ya hidrojeni, hizi njia uhitaji viwango vya hidrojeni kuwa chini, kama ilivyo wakati E. koli inapoishi pamoja naviumbe vinavyotumnia hidrojeni kama vile methanojeni au bakteria zinazopunguza salfeti.[12]

Ukuaji wa juu wa E. koli hutokea katika kiwango cha joto cha 37 ° C (98.6 ° F) lakini aina nyingine za maabara zinaweza kuongezeka kwa joto la juu ya 49 ° C (120.2 ° F).[13] Ukuaji inaweza kuendeshwa na kupumua anaerobiki au aerobiki, kwa kutumia aina kubwa ya jozi redoksi, ikiwa ni pamoja na uoksidisha wa asidi piruvati, asidi fomi, hidrojeni na asidi amino, na kupunguza nyenzo kama vile oksijeni, nitrati, dimethili salfoksidi na trimethilamini oksidi-N.[14]

Aina ambazo zina flajela zinaweza kuogelea na ni sogezi. flajela zina utaratibu wa viungo vya pembeni.[15]

E. koli na bacteria zinazohusiana humiliki uwezo wa kuhamisha DNA kupitia bakteria za muungano, uhamisho wa DNA kutoka kwa seli ya bakteria hadi nyingine au mabadiliko, ambayo inaruhusu nyenzo za kijenetiki kueneza kiupande kwa jamii iliyopo. Utaratibu huu ulisababisha kuenea kwa mwandiko wa jeni wa sumu shiga kutoka Shigella hadi E. coli O157:H7 , inayoenezwa kwa kilabakteria.[16]

Wajibu kama mikrobiota ya kawaida[hariri | hariri chanzo]

E. koli kwa kawaida humiliki njia ya utumbo wa mtoto mchanga ndani ya masaa 40 baada ya kuzaliwa, huwasili kwa chakula au maji au kupitia kwa watu wanaombeba mtoto. Katika utumbo, hushikamana na kamasi ya utumbo mkubwa. Ni enerobu ya msingi ya kutengeneza ATP katika njia ya utumbo [17]wa binadamu. (Enerobu za kuzalisha ATP ni viumbe ambavyo vinaweza kukua katika uwepo au bila uwepo wa oksijeni.) Bora tu bakteria zisipate vipengele vya kijenetiki vya kusababisha madhara, hizo hazisababishi madhara.[18]

Matumizi ya kimatibabu ya E. koli isiyosababisha magonjwa[hariri | hariri chanzo]

Aina ya Esicherichia koli ya Nissle 1917 pia ijulikanayo kama Mutaflor hutumika kama hamira katika dawa, hasa kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali ya njia ya utumbo, [19] ikiwa ni pamoja na ugonjwa wa uvimbe wa tumbo.[20]

Wajibu katika ugonjwa[hariri | hariri chanzo]

Aina zenye madhara za E. koli zinaweza kusababisha gastroenteritisi, maambukizi ya njia ya mkojo, na ugonjwa wa uvimbe wa tando za uti wa mgongo na ubongo katika mwezi wa kwanza wa utotoni. Katika kesi adimu, aina zenye madhara husababisha ugonjwa wa haemoliti uremiki (HUS), peritonitisi, mastitisi, septikemia na kichomi cha Gramu-hasi.[17]

Maambukizi ya Utumbo[hariri | hariri chanzo]

Mikrografu ya kielektroni ya joto la chini ya nguzo za bakteria za E. koli, akasifiwa mara 10,000. Bakteria moja ni silinda ya mviringo.

Baadhi ya aina za E. koli, kama vile O157: H7, O121 na O104: H21, huzalisha sumu zinazoweza kuwa hatari. Sumu ya chakula inayotokana na E. koli husababishwa na kula mboga amabzo hazikuoshwa au nyama ambayo haikupikwa vizuri. O157: H7 pia ina sifa mbaya ya kusababisha athari kubwa na hata kusababisha matatizo yenye kutishia maisha kama vile ugonjwa wa hemoliti-uremiki (HUS). Aina hii inahusishwa na mkurupuko wa 2006 wa E. coli huko Marekani kutokana na mchicha mbichi. Ukali wa ugonjwa unatofautiana mno, hivyo unaweza kuwa mbaya, hasa kwa watoto wadogo, wazee au walio na upungufu wa kinga, lakini ni mara nyingi si kali. Awali, njia zisizozingatia usafi katika kuandaa nyama nchini Uskoti kuliwaua watu saba mwaka 1996 kutokana na sumu ya E. koli , na kuacha mamia zaidi wakiwa wameambukizwa. E. koli inaweza kuhifadhi enterotoksini zisizoathiriwa na joto na zinazoathiriwa na joto. Hiyo ya mwisho, huitwa LT, ina sehemu moja A na tano za B zilizopangwa katika holotoksini moja, na ni sawa sana katika umbo na utendajikazi na sumu ya kipindupindu. Sehemu za B husaidia katika kushikilia na kuingia kwa sumu ndani ya seli za matumbo ya kimelea, wakati sehemu ya A hupasuliwa na kuzuia seli kufonyonza maji, na kusababisha kuhara. LT ni huzalishwa na njia ya uzalisha ya Aina ya 2.[21]

Iwapo bakteria za E. koli zitatoka kwenye njia ya utumbo kupitia utoboaji (kwa mfano kutoka kwa kidonda, na kiambatanisho kilichopasuka, au kutokana na makosa ya upasuaji a) na kuingia katika tumbo, kawaida husababisha peritonitisi ambayo inaweza kuwa hatari isipotibiwa haraka. Hata hivyo, E. koli ni nyeti sana kwa Antibiotiki kama vile streptomisini au gentamisini. Hii inaweza kubadilika kwani, kama ilivyobainishwa awali, E. koli hupata upinzani kwa dawa haraka.[22] Utafiti wa karibuni unaonyesha kwamba matibabu ya antibiotiki hayaboreshi matokeo ya ugonjwa huo, na yanaweza kuongeza pakubwa uwezekano wa kuugua ugonjwa wa haemolitiki uraemiki.[23]

Mukosa ya matumbo inayohusishwa na E. koli huonekana kwa idadi iliongezeka katika uvimbe wa tumbo ugonjwa, na ugonjwa wa Crohn na colitis ya vidonda.[24] Aina za kuingilia za E. koli huwepo kwa idadi kubwa katika tishu zilizovimba, na idadi ya bakteria katika sehemu zilizofura zinawiana na ukali wa kuvimba tumbo.[25]

Sifa hatari[hariri | hariri chanzo]

E. koli za matumbo (EC) huanishwa kwa misingi ya sifa za majimaji ya damu na tabia za uhatari.[17] Virotaipu ni pamoja na:

Jina Vimelea Maelezo
E. koli Enterotoksijeniki (ETEC) chanzo cha kuhara (bila homa) kwa binadamu, nguruwe, kondoo, mbuzi, ng'ombe, mbwa, farasi ETEC hutumia vinato vya fimbriali (vichomozi kutoka eneo la kiini cha bakteria ) kufunga seli za enterosaiti katika utumbo mdogo. ETEC unaweza kuzalisha enterotoksini mbili zenye protini:aina za ETEC haziingilii, na hazitoki kwenye lumeni ya matumbo. ETEC ni sababu ya bakteria inayoongoza ya kuhara kwa watoto katika nchi zinazoendelea duniani, na pia ni chanzo kikuu cha kuharisha kwa msafiri. Kila mwaka, ETEC husababisha milioni 200 kesi zaidi ya kuhara na vifo 380,000, wengi wao wakiwa watoto katika nchi zinazoendelea. [26]
  • protini kubwa kwa hizi mbili, enterotoksini ya LT, ni sawa na sumu ya kipindupindu kimuundo na utendajikazi.
E. koli Enteropathojeniki (EPEC) Sababu ya kuhara kwa binadamu, sungura, mbwa, paka na farasi Kama ETEC, EPEC pia husababisha kuhara, lakini utaratibu wa Masi wa ukoloni na etiolojia ni tofauti. EPEC hukosa fimbriae, na sumu ya ST na LT, lakini hutumia kinatisha kinachojulikana kama intimini kufunga seli za matumbo. Virotaipu hii ina mpangilio wa vipengele hatari ambazo ni sawa na zile zinazopatikana katika Shigela, na zinazweza kuwa na sumu shiga. Kunata kwa mukosa ya matumbo husababisha ya kupangwa tena kwa aktini katika seli kimelea, inayosababisha kulemaa sana. Seli za EPEC huvamia kwa kiasi (yaani hizo huingia katika seli kimelea) na kusababisha athari ya uvimbe Mabadiliko katika muundo wa msingi wa seli za matumbo kutokana na "kunatisha na kufutilia mbali" kunaweza kuwa sababu kuu ya kuhara kwa wale walioathiriwa na EPEC.
E. koli Vamizi (EIEC) hupatikana tu kwa binadamu maambukizi ya EIEC husababisha ugonjwa unaofanana na Shigelosisi, na kuhara sana na homa kali.
E. koli ya Kuharisha damu (EHEC) hupatikana kwa binadamu, mifugo, na mbuzi Mwanachama maarufu sana kwa virotaipu hii ni aina ya O157:H7 , ambayo husababisha kuhara damu na haina homa. EHEC inaweza kusababisha ugonjwa hemolaiti-uremiki na kufeli ghafla kwa figo. Inatumia fimbriae ya kibakteria kwa kunata (pilusi ya kawaida ya E. koli , ECP), [27] huvamia kwa kiasi na ina sumu ya shiga ambayo inaweza kusababisha uvimbe wenye uchungu mwingi.
E. koli Ya kukusanya (EAEC) hupatikana tu kwa binadamu Imeitwa hivyo kwa sababu ina fimbriae ambazo hukusanya seli za tishu, EAEC hunata kwenye mukosa ya matumbo na kusababisha kuhara majimaji bila homa. EAEC si vamizi. Hizo huzalisha hemolaisini na enterotoksini ya ST sawa na ile ya ETEC.

Epidemolojia ya maambukizi ya utumbo[hariri | hariri chanzo]

Kusambaa kwa E. koli inayosababisha magonjwa mara nyingi hutokea kwa kinyesi kuingia mdomoni.[18][28][29] Njia za kawaida za kusambaa ni pamoja na: maandalizi ya chakula yasiyozingatia usafi,[28]Ukolezi wa shamba kutokana na kuwekwa mbolea,[30] umwagiliaji maji wa mazao kwa maji taka kutoka bafu au jikoni yaliyosibikwa au maji taka yenye kinyesi, nguruwe mwitu katika nchi za kilimo,[31] au matumizi ya moja kwa moja ya maji-taka yaliyosibikwa.[32] Ng'ombe wa maziwa na nyama ni hifadhi ya msingi ya E. koli O157: H7,[33] na wanaweza kuibeba bila dalili na kuimwaga katika vinyesi vyao. Bidhaa za chakula zinazohusiana na kuzuka kwa E. koli ni pamoja na nyama mbichi,[34] mbegu ghafi zinazootesha au mchicha,[30] maziwa ghafi, juisi ambayo haijaondolewa vijidudu, siagi ambayo haijaondolewa vijidudu na vyakula vilivyosibikwa na wafanyakazi wa chakula kupitia njia ya kinyesi na mdomo.[28]

Kwa mujibu wa Tawala za Marekani za Chakula na Dawa ,mzunguko wa njia ya kinyesi na mdomo wa usambazaji unaweza kukatizwa kwa kupika vyakula vizuri, kuzuia kusabikiwa, kuanzisha vikwazo kama vile glavu za mipira kwa wafanyakazi wa vyakula, kuanzisha sera za huduma ya afya ili wafanyakazi wa sekta ya chakula kutafuta matibabu wakati wao ni wagonjwa, kuondoa vijidudu kwa maziwa au juisi na mahitaji halisi ya kuosha mkono.[28]

E. koli zinazozalisha sumu ya Shiga (STEC), hasa serotaipu O157: H7, pia husambazwa na nzi,[35][36][37] na pia kugusana moja kwa moja na wanyama wa shambani,[38][39] kuwagusa wanyama wa pori waliofugwa,[40] na chembechembe zinazopeperuka hewani zinazopatikana katika mazingira ya ufugaji wanyama.[41]

Maambukizi ya njia ya mkojo[hariri | hariri chanzo]

Bakteria ya E. koli, viumbe wenye gramu-hasi wanaopatikana kwa wingi sana katika utumbo [42].

E. koli ya Uropathojeniki (UPEC) huwa chanzo cha takriban 90% ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) kuonekanako katika watu wenye maumbile ya kawaida.[17] Katika maambukizi yanayoongezeka, bakteria ya kinyesi hutawala yurethra na kuenea kwenda juu kwa njia ya mkojo na kibofu cha mkojo na vilevile mafigo (kusababisha athari ya kuvimba kwa mafigo na fupanyonga lake),[43] au tezi kibofu katika wanaume. Kwa sababu wanawake wana yurethra fupi kuliko wanaume, wao wana uwezekano mara 14 zaidi kuugua kutokana na kupanda kwa UTI.[17]

Uropathojeniki za E. koli hutumia fimbriae P (kuvimba kwa mafigo na fupanyonga lake inayohusiana na pili) ili kufunga seli za endotheli za njia ya mkojo na kutawala kibofu cha mkojo. Vinata hivi hufunga D-galaktosi-D-galaktosi ya kundi tendakazi la molekuli kwenye kundi P la antijeni ya damu ya erythrosaiti na seli uroepitheli.[17] Takriban 1% ya binadamu hawana hukosa vipokezi hivi, na uwepo au ukosefu wake huamua uwezekano wa mtu kuathiriwa na E. koli ya njia ya mkojo. Uropathojeniki za E. koli huzalisha hemolaisini za alpha na beta, hiyo husababisha lisisi ya seli za njia ya mkojo.

UPEC inaweza kuepuka kinga ya ndani ya mwili (kwa mfano mfumo wa kusaidia) kwa kuvamia mwavuli wa juu juu wa seli na kuunda jamii ya bakteria ndani ya seli(IBC s).[44] Hizo pia zina uwezo wa kuunda antijeni K, polisakaraidi zenye umbo la kapsuli ambazo huchangia ukuaji wa viumbe vinavyokuwa vimeshikamana. E. koli zinazozalisha viumbe vinavyokuwa vimeshikamana ni kinzani kwa vipengele vya kinga na tiba ya antibiotiki na mara nyingi huwa chanzo cha maambukizi sugu ya njia ya mkojo.[45] Maambukizi ya E. koli yanayozalisha antijeni-K kwa kawaida hupatikana katika sehemu ya juu ya njia ya mkojo.[17]

Maambukizi yanayoshuka, ingawa kwa kiasi ni nadra, hutokea wakati seli za E. koli huingia katika viungo vya juu vya njia ya mkojo (figo, kibofu cha mkojo au ureta) kutoka mkondo wa damu.

Ugonjwa wa uvimbe wa tando za uti wa mgongo na ubongo wa utotoni[hariri | hariri chanzo]

Huzalishwa na serotaipu ya Esicherichia koli ambayo ina antijeni ya kikapsuli iitwayo K1. Ukoloni wa matumbo ya mtoto mchanga kwa mashina haya, ambayo yako katika uke wa mama, husababisha bakteriemia, ambayo inapelekea kwa ugonjwa uvimbe wa tando za uti wa mgongo na ubongo. Na kwa sababu ya kukosekana kwa kingamwili ya IgM kutoka kwa mama (hizi hazivuki kondo kwa sababu FcRn husimamia uhamisho wa IgG), pamoja na kuwa mwili hutambua antijeni K1 kama yake, kwa kuwa inafanana na serebali ya glikopeptidi, hii husababisha ugonjwa mkali wa uvimbe wa tando za uti wa mgongo na ubongo katika watoto wachanga.

Uaguzi wa kimaabara[hariri | hariri chanzo]

Katika sampuli za kinyesi masomo ya hadumini huonyesha fimbo za Gramu hasi, bila mpango maalum wa seli. Kisha, aidha agari MacConkey au agari EMB (au zote) inachanjwa kwa kinyesi. Katika agari MacConkey, makoloni nyekundu ya kina huzalishwa kwa kiumbe kina laktosi, na kuchachishwa kwa sukari hii husababisha pH ya chombo kushuka, na hivyo kusababisha chombo kuwa giza. Ukuaji katika agari Levini EMB hutoa koloni nyeusi na mngaro wa kimetali wa rangi ya nyeusi-kijani. Huu niutambuzi wa E. koli. Kiumbe pia kina laisini, na hukua kwa TSI iliyopinda kwa mtazamo wa (A / A / g + / H 2 S-). Pia, IMViC ni + + - kwa E. koli, kama ni 2}indoli yake chanya (pete nyekundu) na methili nyekundu chanya (nyekundu angavu), lakini VP hasi (hakuna mabadiliko-haina rangi) na sitreti hasi (rangi ya kijani-hakuna mabadiliko). Vipimo vya uzalishaji wa sumu viaweza kutumia seli za mamalia katika tishu, ambazo huuawa haraka kwa sumu shiga. Ingawa inaathirika kwa urahisi sana na ni maalum sana, utaratibu huu ni wa polepole na wa gharama kubwa.[46]

Utambuzi wa kawaida umefanyika kwa kukuza viini kwa chombo cha sobitoli cha MacConkey kisha kutumia antiserumu ya kuandika. Hata hivyo, mipira ya kuchanganua kiasi cha dutu na baadhi antiserumu za kuandika umeonyesha athari za kuvuka na koloni zisizo za E koli O157. Aidha, si aina zote za E. coli O157 zinazohusiana na HUS ni vichachishaji vya sobitoli.

Baraza la Jimbo na Wanaepidemiolojia wa Wamaeneo walipendekeza kwamba maabara ya kliniki angalau yapime vinyesi vyote vyenye damu kwa uwepo wa pathojeni hii. Chama cha Marekani cha Msingi wa Magonjwa ya Njia ya Tumbo(AGAF) kilipendekeza katika Julai 1994 kuwa sampuli zote za kinyesi zipimwe mara kwa mara kwa uwepo wa E. koli O157: H7.[onesha uthibitisho] Inapendekezwa kwamba Tabibu awasiliane na idara ya hali ya afya zao au na Kituo cha Kudhibiti Ugonjwa na Kuzuia kuamua sampuli ambazo ni lazima zipimwe na kama matokeo yanafaa kuripotiwa.

Njia nyingine za kuchunguza E. koli O157 kwenye kinyesi ni pamoja na vipimo vya ELISA, koloni ya vipimo vya kupima protini, masomo ya moja kwa moja ya hadumini ya imunofloresensi ya vichungi, pamoja na mbinu za kutenga viumbe maalum kwa kutumia shanga za kisumaku.[47] Changanuzi hizi zimekusudiwa kama chombo kuruhusu uchunguzi wa haraka kwa ajili ya kupima uwepo wa E. koli O157 bila ya kukuza viini kwanza kwa sampuli hiyo ya kinyesi.

Tiba ya Antibiotiki na upinzani[hariri | hariri chanzo]

Maambukizi ya bakteria kwa kawaida hutibiwa kwa antibiotiki Hata hivyo kiwango cha kuathiriwa na antibiotiki cha aina mbalimbali za E. koli kinatofautiana sana. Kama viumbe vya Gramu-hasi, E. koli ni stahimilivu kwa antibiotiki nyingi ambazo hufanyakazi dhidi ya Gramu-chanya. Antibiotiki ambazo zinaweza kutumika kutibu maambukizi ya E. koli ni pamoja na amoksilini pamoja na penisilini nyingine zilizosanisiwa nusu, sefalosporini nyingi, kabapenemi, aztreonami, trimethoprim-sulfamethoksazoli, ciprofloksasini, nitrofurantoini na aminoglaikosidi.

Kustahimili Antibiotiki ni tatizo linalokua. Baadhi ya hii inatokana na kutumika sana kwa antibiotiki na binadamu, lakini baadhi yake pengine ni kutokana na matumizi ya antibiotiki kama viendelezi ukuaji wa chakula cha wanyama.[48] Utafiti uliochapishwa katika jarida la Sayansi katika Agosti 2007 ulipata kuwa kiwango cha mabadiliko katika E. koli ni "juu ya mara 10 -5 kwa kila jenomu kwa kizazi, ambayo ni mara 1000 zaidi ya makadirio ya awali," matokeo ambayo yanaweza kuwa na maana kwa ajili ya utafiti na uthibiti wa ustahimilivu kwa antibiotiki wa bakteria.[49]

E. koli inayostahimili Antibiotiki pia inaweza kupitisha jeni zinazosababisha ustahimilivu kwa antibiotiki kwenda kwa aina nyingine ya bakteria, kama vile Stafilokokasi aureasi, kupitia mchakato uitwao uhamisho wa upande wa jeni . E. koli mara nyingi hubeba plasmidi zinazostahimili madawa mengi na uzihamisha kwa urahisi iwapo ina shinikizo kwenda kwa aina nyingine. Hakika, E. koli ni mwanachama wa mara kwa mara wa jamii ya viumbe ambapo aina nyingi za bakteria huishi kwa karibu karibu. Mchanganyiko huu wa aina unaruhusu aina za E. koli ambazo zimefunikwa na pili ili kukubali na kuhamisha plasmidi kutoka na kwenda kwa bakteria zingine. Hivyo E. koli na enterobakteria nyingine ni hifadhi muhimu ya ustahimilivu wa antibiotiki unaoweza kuhamishwa.[50]

Aina ya laktamisi beta[hariri | hariri chanzo]

Ustahimilivu kwa antibiotiki laktamu beta umekuwa tatizo hasa katika miongo ya hivi karibuni, kama aina ya bakteria ambazo huzalisha laktamasi beta zimekuwa za kawaida zaidi.[51] Vimeng'enya hivi vya laktamsi beta hufanya penisilini sefalosporini nyingi, kuwa tiba isiyofanya kazi. Laktamasi beta za wigo uliopanuliwa zinazozalisha E. koli ni stahimilivu sana kwa aina nyingi ya antibiotiki na maambukizi ya aina hizi ni magumu kutibu. Katika matukio mengi, mbili tu ya antibiotiki simulizi na kiasi kidogo sana cha antibiotiki za ndani ya mishipa bado zina ufanisi. Katika 2009, jeni iitwayo New Delhi metallo-beta-lactamasi (kwa kifupi NDM-1) ambayo inatoa ustahimilivu kwa antibiotiki kabapenemu ya ndani ya mifupa, ziligunduliwa katika India na Pakistan katika bakteria za E. koli .

Kuongezeka kwa wasiwasi kuhusu maambukizi ya aina hii ya "bakteria hatari" nchini Uingereza kumesababisha wito wa ufuatiliaji zaidi na mkakati wa Uingereza nzima wa kukabiliana na maambukizi na vifo.[52] Vipimo vya uwezekano wa kuathiriwa vinafaa kuongoza tiba katika magonjwa yote ambayo viumbe vinaweza kutengwa kwa ajili ya kukuza viini.

Tiba ya feji[hariri | hariri chanzo]

Tiba ya bakteriafeji virusi ambavyo hasa vinalenga baketria ya kipathojeni imekuwa ikiendelezwa kwa zaidi ya miaka 80 iliyopita, hasa katika Urusi ya zamani, ambapo ilitumika kuzuia kuhara kulikosababishwa na E. koli. [53] Hivi sasa, tiba ya kilabakteria kwa binadamu inapatikana tu katika Kituo cha Tiba ya kilabakteria katika Jamhuri ya Jeojia na Poland.[54] Hata hivyo, tarehe 2 Januari 2007, shirika la Marekani la FDA lilitoa kibali kwa Omnilytics kutumia Tiba yake ya kilabakteria ya kuuaE. koli O157: H7 katika ukungu, kinyunyizio au safisha ya wanyama hai watakaochinjwa kwa ajili ya matumizi ya binadamu.[55] Bakteriafeji T4 ni feji iliyotafitiwa sana kwa malengo ya kuambukiza E. koli.

Chanjo[hariri | hariri chanzo]

Watafiti wamefanya juhudi kuendeleza chanjo yenye usalama, na ufanisi wa kupunguza matukio ya maambukizi duniani kote ya E. koli .[56] Katika Machi 2006, chanjo iliyosababisha jibu la kinga dhidi ya E. koli O157: H7 O-maalum polisakaraidi ilo unganishwa tena kwa eksotoksini Pseudomonas aeruginosa (O157-rEPA) iliripotiwa kuwa salama kwa watoto wa umri wa miaka miwili hadi mitano. Kazi ya awali ilikuwa tayari imeonyesha kuwa ni salama kwa watu wazima.[57] Awamu ya III ya majaribio ya kimatibabu ya kuthibitisha ufanisi kwa kiwango kikubwa wa matibabu imepangwa.[57]

Katika 2006 Afya ya Wanyama ya Fort Dodge (Wyeth) ilianzisha chanjo madhubuti ya virusi visoukali ili kudhibiti aisakulitisi na peritonitisi katika kuku. Chanjo hii ni chanjo nasaba isosumu ambayo imethibitisha kinga dhidi ya O78 na aina zisizoweza kupigwa chapa .[58]

Katika Januari 2007 kampuni ya Kanada Madawa, Bioniche ilitangaza kuwa imetengeneza chanjo ya mifugo ambayo inapunguza idadi ya O157: H7 inayomwaga katika mbolea kwa mara 1000, hadi karibu bakteria pathojeni 1000 kwa kila gramu ya mbolea.[59][60][61]

Katika Aprili 2009 mtafiti wa Chuo Kikuu cha Jimbo la Michigan alitangaza kwamba ameanzisha chanjo inayofanya kazi kwa aina ya E. koli. Mahdi Saeed, profesa wa Epidemolojia na maradhi ya kuambukiza katika vyuo vya MSU vya Tiba Wanyama na Dawa za Binadamu, ametuma maombi kwa ajili ya hataza kwa ugunduzi wake na amefanya mawasiliano na makampuni ya dawa kwa ajili ya uzalishaji wa kibiashara.[62]

Wajibu katika bioteknolojia[hariri | hariri chanzo]

Kwa sababu ya historia yake ndefu ya utamaduni wa maabara na urahisi wa kushughulikiwa, E. koli pia ina jukumu muhimu katika uhandisi wa kibiolojia wa kisasa na mikrobiolojia ya kiviwanda.[63] Kazi ya Stanley Cohen Norman na Herbert Boyer katika E. koli, kwa kutumia plasmidi na vimeng'enya vya kuzuia kuunda DNA inayoshikana tena, ikawa msingi wa bioteknolojia.[64]

Hufikiriwa kuwa kimelea chenye uwezo mkubwa sana kwa ajili ya uzalishaji wa protini heterologu,[65] watafiti wanaweza kujumuisha jeni katika vijiumbe maradhi kwa kutumia plasmidi, kuruhusu uzalishaji kwa wingi wa protini katika mchakato uchachishaji wa kiviwanda. Mifumo ya maumbile pia imeendelezwa ambayo inaruhusu uzalishaji wa protini inayoweza kuunganishwa tena kwa kutumia E. koli. Moja ya matumizi muhimu ya kwanza ya teknolojia ya DNA inayoweza kuungana tena ilikuwa kughilibiwa kwa E. koli kuzalisha insulini binadamu.[66] E. koli zilizobadilishwa zimetumika katika maendelezo ya chanjo, kutumia viumbe kurejesha mazingira ya awali, na uzalishaji wa vimeng'enya visivyoweza kusonga.[65] Hata hivyo,E. koli haiwezi, kutumika kuzalisha baadhi ya protini tata kubwa zaidi, ambazo zina bondi za disulfidi nyingi na, hasa, thiol zisizopacha, au protini zinazohitaji pia kubadilishwa baada ya kutafsiriwa kimuundo kwa ajili ya utendajikazi.[63]

Tafiti pia zinafanywa katika kuweka programu katika E. koli ili labda iweze kutatua matatizo ya hisabati magumu kama vile tatizo la njia la Hamilton.

Ubora wa Mazingira[hariri | hariri chanzo]

Bakteria za E. koli kwa kawaida zimekuwa zikipatikana katika maji ya burudani na uwepo wao hutumika kuashiria uwepo wa kuhasibika kwa kinyesi kwa hivi karibuni, lakini uwepo wa E. koli inaweza kosa kuwa dalili ya kinyesi cha binadamu. E. koli ni mkadhania katika wanyama wote wasioathiriwa na joto: ndege na mamalia. Bakteria ya E. koli pia zimepatikana katika samaki na kasa. Mchanga na udongo pia huifadhi bakteria ya E. koli na baadhi ya aina za E. koli ambazo asilishwa . Baadhi ya maeneo ya kijiografia yanaweza kusaidia aina za kipekee za E. koli na kinyume, baadhi aina za E. koli zina asili tofauti[1].

Viumbe Mifano[hariri | hariri chanzo]

E. koli mara nyingi hutumika kama viumbe mfano katika masomo ya mikrobiolojia. Aina zilizokuzwa (km E. koli K12) zinaishi vizuri katika mazingira ya maabara, na, tofauti na aina zisizokuzwa, zimepoteza uwezo wao wa kustawi katika utumbo. Aina nyingi za maabara hupoteza uwezo wao wa kuunda muungano wa seli tofauti.[67][68] Maumbile haya hulinda aina zisizokuzwa kutokana na kingamwili na mashambulizi mengine ya kemikali, lakini uhitaji matumizi makubwa ya nishati na rasilimali.

Katika 1946, Joshua Lederberg na Edward Tatum kwanza walielezea jambo lililojulikana kama kuunganisha bakteria kwa kutumia bakteria ya E. koli kama mfano,[69] na inabakia kuwa mfano wa msingi wa kutafiti muungano.[onesha uthibitisho] E. koli ilikuwa ni sehemu muhimu ya majaribio ya kwanza ya kuelewa jenetiki za kilabakteria,[70] na watafiti mapema, kama vile Seymour Benzer, alitumia E. koli na kilabakteria ya T4 kuelewa topografia ya muundo wa jeni.[71] Kabla ya utafiti wa Benzer, haikuwa inayojulikana kama jeni ilikuwa na utaratibu kimstari, au kama ulikuwa na muundo wa kimatawi.

E. koli ilikuwa moja ya viumbe vya kwanza kuwa na jenomu iliyotaratibiwa; jenomu kamili ya E. koli K12 ilichapishwa na Sayansi katika 1997.[72]

Majaribio ya muda mrefu ya mabadiliko kwa kutumia E. koli, yalianzishwa na Richard Lenski mwaka 1988, yameruhusu kushuhudiwa moja kwa moja kwa mabadiliko makubwa katika maabara.[73] Katika jaribio hili, moja ya idadi ya E. koli bila kutarajia ilitoa uwezo wa kumetaboli siterati kwa kutumia oksijeni. Uwezo huu ni nadra sana katika E. koli. Kwa kuwa kukosa uwezo na kukua kukiwepo oksijeni kwa kawaida hutumika kama njia ya kutofautisha E. koli kutokana nyingine, zinazohusiana kwa karibu sana kibakteria kama vile Salmonella, uvumbuzi huu unaweza kuashiria tukio la kipekee kuonekana katika maabara.

Kwa kuchanganya nanoteknolojia na ikolojia ya kimazingira Mandhari ya mazingira magumu yanaweza kutolewa na maaelezo katika skeli ya nano.[74] Kwa mazingira sanisi kama haya majaribio ya mabadiliko kwa kutumia E. koli yamefanywa ili kutafiti biofizikia ya kukabiliana na hali katika kisiwa cha biojiografia kwenye .

Tazama Pia[hariri | hariri chanzo]

  • Escherichia coli O157:H7
  • Majaribio ya mageuzi ya muda mrefu ya E. koli
  • Kanuni za Kimataifa za majina ya Bakteria
  • Mfumo wa T4 rII
  • uchambuzi wa bakteria ya maji
  • Bakteria kolifomu
  • Kudhibiti ukolezi
  • Sumu ya chakula
  • Kolifomu ya kinyesi
  • uzalishaji wa gesi kutoka glukosi na E. koli maonyesho ya video Archived 24 Novemba 2012 at the Wayback Machine.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Escherichia coli O157:H7. CDC Division of Bacterial and Mycotic Diseases. Iliwekwa mnamo 2007-01-25.
  2. Vogt RL, Dippold L (2005). "Escherichia coli O157:H7 outbreak associated with consumption of ground beef, June-July 2002". Public Health Rep 120 (2): 174–8. PMC 1497708. PMID 15842119. 
  3. Bentley R, Meganathan R (1 Septemba 1982). "Biosynthesis of vitamin K (menaquinone) in bacteria". Microbiol. Rev. 46 (3): 241–80. PMC 281544. PMID 6127606.  Check date values in: |date= (help)
  4. 4.0 4.1 Hudault S, Guignot J, Servin AL (Julai 2001). "Escherichia coli strains colonising the gastrointestinal tract protect germfree mice against Salmonella typhimurium infection". Gut 49 (1): 47–55. PMC 1728375. PMID 11413110. doi:10.1136/gut.49.1.47.  Check date values in: |date= (help)
  5. Reid G, Howard J, Gan BS (Septemba 2001). "Can bacterial interference prevent infection?". Trends Microbiol. 9 (9): 424–8. PMID 11553454. doi:10.1016/S0966-842X(01)02132-1.  Check date values in: |date= (help)
  6. 6.0 6.1 6.2 Feng P, Weagant S, Grant, M (2002-09-01). Enumeration of Escherichia coli and the Coliform Bacteria. Bacteriological Analytical Manual (8th ed.). FDA/Center for Food Safety & Applied Nutrition. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-05-19. Iliwekwa mnamo 2007-01-25.
  7. 7.0 7.1 Thompson, Andrea. "E. coli Thrives in Beach Sands", Live Science, 2007-06-04. Retrieved on 2007-12-03. 
  8. Escherichia. Taxonomy Browser. NCBI. Iliwekwa mnamo 2007-11-30.
  9. Lawrence, JG na Ochman, H. (1998) Akiolojia ya Masi ya jenomu ya Esicherichia koli Proc. Natl. Acad. Sci. USA 95:9413-9417 PMC21352
  10. 10.0 10.1 Nataro JP, Kaper JB (Januari 1998). "Diarrheagenic Escherichia coli". Clin. Microbiol. Rev. 11 (1): 142–201. PMC 121379. PMID 9457432.  Check date values in: |date= (help)
  11. Kubitschek HE (1 Januari 1990). "Cell volume increase in Escherichia coli after shifts to richer media". J. Bacteriol. 172 (1): 94–101. PMC 208405. PMID 2403552.  Check date values in: |date= (help)
  12. Madigan MT, Martinko JM (2006). Brock Biology of microorganisms (11th ed.). Pearson. ISBN 0-13-196893-9. 
  13. Fotadar U, Zaveloff P, Terracio L (2005). "Growth of Escherichia coli at elevated temperatures". J. Basic Microbiol. 45 (5): 403–4. PMID 16187264. doi:10.1002/jobm.200410542. 
  14. Ingledew WJ, Poole RK (1984). "The respiratory chains of Escherichia coli". Microbiol. Rev. 48 (3): 222–71. PMC 373010. PMID 6387427. 
  15. [36] ^ Darnton NC, Turner L, Rojevsky S, Berg HC, Kuhusu msongonyo katika Esicherichia koli ya kuogelea. J Bacteriol. 2007 Machi, 189 (5) :1756-64. Epub 2006 22 Desemba.
  16. Brüssow H, Canchaya C, Hardt WD (Septemba 2004). "Phages and the evolution of bacterial pathogens: from genomic rearrangements to lysogenic conversion". Microbiol. Mol. Biol. Rev. 68 (3): 560–602. PMC 515249. PMID 15353570. doi:10.1128/MMBR.68.3.560-602.2004.  Unknown parameter |pagesteuhqw89-ty389q= ignored (help); Check date values in: |date= (help)
  17. 17.0 17.1 17.2 17.3 17.4 17.5 17.6 Todar, K.. Pathogenic E. coli. Online Textbook of Bacteriology. University of Wisconsin–Madison Department of Bacteriology. Iliwekwa mnamo 2007-11-30.
  18. 18.0 18.1 Evans Jr., Doyle J.; Dolores G. Evans. Escherichia Coli. Medical Microbiology, 4th edition. The University of Texas Medical Branch at Galveston. Iliwekwa mnamo 2007-12-02.
  19. Grozdanov, L; Raasch, C; Schulze, J; Sonnenborn, U; Gottschalk, G; Hacker, J; Dobrindt, U (Agosti 2004). "Analysis of the genome structure of the nonpathogenic probiotic Escherichia coli strain Nissle 1917.". J Bacteriol 186 (16): 5432–41. PMC 490877. PMID 15292145. doi:10.1128/JB.186.16.5432-5441.2004.  More than one of |author2= and |last2= specified (help); More than one of |author3= and |last3= specified (help); More than one of |author4= and |last4= specified (help); More than one of |author5= and |last5= specified (help); More than one of |author6= and |last6= specified (help); More than one of |author7= and |last7= specified (help); Check date values in: |date= (help)
  20. Kamada, N; Inoue, N; Hisamatsu, T; Okamoto, S; Matsuoka, K; Sato, T; Chinen, H; Hong, KS; Yamada, T (Mei 2005). "Nonpathogenic Escherichia coli strain Nissle1917 prevents murine acute and chronic colitis.". Inflamm Bowel Dis 11 (5): 455–63. PMID 15867585. doi:10.1097/01.MIB.0000158158.55955.de.  More than one of |author2= and |last2= specified (help); More than one of |author3= and |last3= specified (help); More than one of |author4= and |last4= specified (help); More than one of |author5= and |last5= specified (help); More than one of |author6= and |last6= specified (help); More than one of |author7= and |last7= specified (help); More than one of |author8= and |last8= specified (help); More than one of |author9= and |last9= specified (help); Check date values in: |date= (help)
  21. Tauschek M, Gorrell R, Robins-Browne RM,. "Identification of a protein secretory pathway for the secretion of heat-labile enterotoxin by an enterotoxigenic strain of Escherichia coli". PNAS 99: 7066–71. PMID 12011463. doi:10.1073/pnas.092152899. 
  22. Gene Sequence Of Deadly E. Coli Reveals Surprisingly Dynamic Genome. Science Daily (2001-01-25). Iliwekwa mnamo 2007-02-08.
  23. Wong CS, Jelacic S, Habeeb RL, et al. (29 Juni 2000). "The risk of the hemolytic-uremic syndrome after antibiotic treatment of Escherichia coli O157:H7 infections.". N Engl J Med 342 (26): 1930–6. PMID 10874060.  Check date values in: |date= (help)
  24. Rolhion N, Darfeuille-Michaud A (2007). "Adherent-invasive Escherichia coli in inflammatory bowel disease". Inflamm. Bowel Dis. 13 (10): 1277–83. PMID 17476674. doi:10.1002/ibd.20176. 
  25. Baumgart M, Dogan B, Rishniw M, et al. (2007). "Culture independent analysis of ileal mucosa reveals a selective increase in invasive Escherichia coli of novel phylogeny relative to depletion of Clostridiales in Crohn's disease involving the ileum". ISME J 1 (5): 403–18. PMID 18043660. doi:10.1038/ismej.2007.52. 
  26. Shirika la Afya Duniani. Archived 15 Mei 2012 at the Wayback Machine.Enterotoksijeniki Esicherichia koli (ETEC). Archived 15 Mei 2012 at the Wayback Machine.
  27. Rendón, M. A.; et al. (2007). "Commensal and pathogenic Escherichia coli use a common pilus adherence factor for epithelial cell colonization". PNAS 104 (25): 10637–42. PMC 1890562. PMID 17563352. doi:10.1073/pnas.0704104104. 
  28. 28.0 28.1 28.2 28.3 Retail Establishments; Annex 3 - Hazard Analysis. Managing Food Safety: A Manual for the Voluntary Use of HACCP Principles for Operators of Food Service and Retail Establishments. U.S. Department of Health and Human Services Food and Drug Administration Center for Food Safety and Applied Nutrition (Aprili 2006). Jalada kutoka ya awali juu ya 2007-06-07. Iliwekwa mnamo 2007-12-02.
  29. Gehlbach, S.H.; J.N. MacCormack, B.M. Drake, W.V. Thompson (Aprili 1973). "Spread of disease by fecal-oral route in day nurseries". Health Service Reports 88 (4): 320–322. PMC 1616047. PMID 4574421.  Check date values in: |date= (help)
  30. 30.0 30.1 Sabin Russell. "Spinach E. coli linked to cattle; Manure on pasture had same strain as bacteria in outbreak", San Francisco Chronicle, 13 Oktoba 2006. Retrieved on 2007-12-02. 
  31. Thomas R. DeGregori (2007-08-17). CGFI: Maddening Media Misinformation on Biotech and Industrial Agriculture. Jalada kutoka ya awali juu ya 2007-10-13. Iliwekwa mnamo 2007-12-08.
  32. Chalmers, R.M.; H. Aird, F.J. Bolton (2000). "Waterborne Escherichia coli O157". Society for Applied Microbiology Symposium Series (29): 124S–132S. PMID 10880187. 
  33. Hitilafu ya kutaja: Invalid <ref> tag; no text was provided for refs named bach
  34. Institute of Medicine of the National Academies (2002). Escherichia coli O157:H7 in Ground Beef: Review of a Draft Risk Assessment. Washington, D.C.: The National Academies Press. ISBN 0-309-08627-2.  More than one of |author= and |last= specified (help)
  35. Szalanski A, Owens C, McKay T, Steelman C (2004). "Detection of Campylobacter and Escherichia coli O157:H7 from filth flies by polymerase chain reaction". Med Vet Entomol 18 (3): 241–6. PMID 15347391. doi:10.1111/j.0269-283X.2004.00502.x. 
  36. Sela S, Nestel D, Pinto R, Nemny-Lavy E, Bar-Joseph M (2005). "Mediterranean fruit fly as a potential vector of bacterial pathogens". Appl Environ Microbiol 71 (7): 4052–6. PMID 16000820. doi:10.1128/AEM.71.7.4052-4056.2005. 
  37. Alam M, Zurek L (2004). "Association of Escherichia coli O157:H7 with houseflies on a cattle farm". Appl Environ Microbiol 70 (12): 7578–80. PMID 15574966. doi:10.1128/AEM.70.12.7578-7580.2004. 
  38. Rahn, K.; S.A. Renwick, R.P. Johnson, J.B. Wilson, R.C. Clarke, D. Alves, S.A. McEwen, H. Lior, J. Spika (Aprili 1998). "Follow-up study of verocytotoxigenic Escherichia coli infection in dairy farm families". Journal of Infectious Disease 177 (4): 1139–1140. PMID 9535003. doi:10.1086/517394.  Check date values in: |date= (help)
  39. Trevena, W.B.; G.A Willshaw, T. Cheasty, G. Domingue, C. Wray (Desemba 1999). "Transmission of Vero cytotoxin producing Escherichia coli O157 infection from farm animals to humans in Cornwall and west Devon". Community Disease and Public Health 2 (4): 263–268. PMID 10598383.  Check date values in: |date= (help)
  40. Heuvelink, A.E.; C. van Heerwaarden, J.T. Zwartkruis-Nahuis, R. van Oosterom, K. Edink, Y.T. van Duynhoven and E. de Boer (Oktoba 2002). "Escherichia coli O157 infection associated with a petting zoo". Epidemiology and Infection 129 (2): 295–302. PMID 12403105. doi:10.1017/S095026880200732X.  Check date values in: |date= (help)
  41. Varma, J.K.; K.D. Greene, M.E. Reller, S.M. DeLong, J. Trottier, S.F. Nowicki, M. DiOrio, E.M. Koch, T.L. Bannerman, S.T. York, M.A. Lambert-Fair, J.G. Wells, P.S. Mead (26 Novemba 2003). "An outbreak of Escherichia coli O157 infection following exposure to a contaminated building". JAMA 290 (20): 2709–2712. PMID 14645313. doi:10.1001/jama.290.20.2709.  Check date values in: |date= (help)
  42. [100]
  43. Nicolle LE (Februari 2008). "Uncomplicated urinary tract infection in adults including uncomplicated pyelonephritis". Urol. Clin. North Am. 35 (1): 1–12, v. PMID 18061019. doi:10.1016/j.ucl.2007.09.004.  Check date values in: |date= (help)
  44. Justice S, Hunstad D, Seed P, Hultgren S (2006). "Filamentation by Escherichia coli subverts innate defenses during urinary tract infection". Proc Natl Acad Sci U S A 103 (52): 19884–9. PMID 17172451. doi:10.1073/pnas.0606329104. 
  45. Ehrlich G, Hu F, Shen K, Stoodley P, Post J (Agosti 2005). "Bacterial plurality as a general mechanism driving persistence in chronic infections". Clin Orthop Relat Res (437): 20–4. PMC 1351326. PMID 16056021. doi:10.1073/pnas.0606329104.  Check date values in: |date= (help)
  46. Paton JC, Paton AW (1 Julai 1998). "Pathogenesis and diagnosis of Shiga toxin-producing Escherichia coli infections". Clin. Microbiol. Rev. 11 (3): 450–79. PMC 88891. PMID 9665978.  Check date values in: |date= (help)[dead link]
  47. De Boer E, Heuvelink AE (2000). "Methods for the detection and isolation of Shiga toxin-producing Escherichia coli". Symp Ser Soc Appl Microbiol (29): 133S–143S. PMID 10880188. 
  48. Johnson J, Kuskowski M, Menard M, Gajewski A, Xercavins M, Garau J (2006). "Similarity between human and chicken Escherichia coli isolates in relation to ciprofloxacin resistance status". J Infect Dis 194 (1): 71–8. PMID 16741884. doi:10.1086/504921. 
  49. Adaptive Mutations in Bacteria: High Rate and Small Effects. Science Magazine (10 Agosti 2007). Iliwekwa mnamo 10 Septemba 2007.
  50. Salyers AA, Gupta A, Wang Y (2004). "Human intestinal bacteria as reservoirs for antibiotic resistance genes". Trends Microbiol. 12 (9): 412–6. PMID 15337162. doi:10.1016/j.tim.2004.07.004. 
  51. Paterson DL, Bonomo RA (2005). "Extended-spectrum beta-lactamases: a clinical update". Clin. Microbiol. Rev. 18 (4): 657–86. PMC 1265908. PMID 16223952. doi:10.1128/CMR.18.4.657-686.2005. 
  52. HPA Press Statement: Infections caused by ESBL-producing E. coli. Jalada kutoka ya awali juu ya 2011-07-17. Iliwekwa mnamo 2010-11-30.
  53. Therapeutic use of bacteriophages in bacterial infections. Polish Academy of Sciences. Jalada kutoka ya awali juu ya 2006-02-08. Iliwekwa mnamo 2010-11-30.
  54. Medical conditions treated with phage therapy. Phage Therapy Center.
  55. OmniLytics Announces USDA/FSIS Approval for Bacteriophage Treatment of E. coli O157:H7 on Livestock. OmniLytics. Jalada kutoka ya awali juu ya 2007-09-30. Iliwekwa mnamo 2010-11-30.
  56. Girard M, Steele D, Chaignat C, Kieny M (2006). "A review of vaccine research and development: human enteric infections". Vaccine 24 (15): 2732–50. PMID 16483695. doi:10.1016/j.vaccine.2005.10.014. 
  57. 57.0 57.1 Ahmed A, Li J, Shiloach Y, Robbins J, Szu S (2006). "Safety and immunogenicity of Escherichia coli O157 O-specific polysaccharide conjugate vaccine in 2-5-year-old children". J Infect Dis 193 (4): 515–21. PMID 16425130. doi:10.1086/499821. 
  58. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-01-08. Iliwekwa mnamo 2021-01-16.
  59. Pearson H (2007). "The dark side of E. coli". Nature 445 (7123): 8–9. PMID 17203031. doi:10.1038/445008a. 
  60. New cattle vaccine controls E. coli infections. Canada AM (2007-01-11). Jalada kutoka ya awali juu ya 2007-01-13. Iliwekwa mnamo 2007-02-08. Archived 13 Januari 2007 at the Wayback Machine.
  61. Canadian Research Collaboration Produces World's First Food Safety Vaccine: Against E. coli O157:H7 (Press release). Bioniche Life Sciences Inc.. 2007-01-10. Archived from the original on 2007-10-11. https://web.archive.org/web/20071011103738/http://cnxmarketlink.com/en/releases/archive/January2007/10/c4698.html. Retrieved 2007-02-08.
  62. http://www.physorg.com/news158951048.html
  63. 63.0 63.1 Lee SY (1996). "High cell-density culture of Escherichia coli". Trends Biotechnol. 14 (3): 98–105. PMID 8867291. doi:10.1016/0167-7799(96)80930-9. 
  64. Russo E (Januari 2003). "The birth of biotechnology". Nature 421 (6921): 456–7. PMID 12540923. doi:10.1038/nj6921-456a.  Check date values in: |date= (help)
  65. 65.0 65.1 Cornelis P (2000). "Expressing genes in different Escherichia coli compartments". Curr. Opin. Biotechnol. 11 (5): 450–4. PMID 11024362. doi:10.1016/S0958-1669(00)00131-2. 
  66. Tof, Ilanit (1994). Recombinant DNA Technology in the Synthesis of Human Insulin. Little Tree Pty. Ltd.. Iliwekwa mnamo 2007-11-30.
  67. Fux CA, Shirtliff M, Stoodley P, Costerton JW (2005). "Can laboratory reference strains mirror "real-world" pathogenesis?". Trends Microbiol. 13 (2): 58–63. PMID 15680764. doi:10.1016/j.tim.2004.11.001. 
  68. Vidal O, Longin R, Prigent-Combaret C, Dorel C, Hooreman M, Lejeune P (1998). "Isolation of an Escherichia coli K-12 mutant strain able to form biofilms on inert surfaces: involvement of a new ompR allele that increases curli expression". J. Bacteriol. 180 (9): 2442–9. PMC 107187. PMID 9573197. 
  69. [164] ^ Lederberg, Joshua; E.L. Tatum (19 Oktoba 1946). "Gene recombination in E. coli" (PDF). Nature 158: 558. doi:10.1038/158558a0.  Check date values in: |date= (help) Chanzo: Maktaba ya Kitaifa ya Tiba - Machapisho ya Joshua Lederberg
  70. The Phage Course - Origins. Cold Spring Harbor Laboratory (2006). Jalada kutoka ya awali juu ya 2002-07-20. Iliwekwa mnamo 2007-12-03.
  71. Benzer, Seymour (Machi 1961). "On the topography of the genetic fine structure". PNAS 47 (3): 403–15. PMC 221592. doi:10.1073/pnas.47.3.403.  Check date values in: |date= (help)
  72. Frederick R. Blattner, Guy Plunkett III, Craig Bloch, Nicole Perna, Valerie Burland, Monica Riley, Julio Collado-Vides, Jeremy Glasner, Christopher Rode, George Mayhew, Jason Gregor, Nelson Davis, Heather Kirkpatrick, Michael Goeden, Debra Rose, Bob Mau, Ying Shao (5 Septemba 1997). "The complete genome sequence of Escherichia coli K-12". Science 277 (5331): 1453–1462. PMC 9278503 Check |pmc= value (help). doi:10.1126/science.277.5331.1453.  Check date values in: |date= (help)
  73. [172] ^ Bakteria zafanya mabadiliko makubwa katika maabara Mwanasayansi Mpya
  74. Keymer J.E., P. Galajda, C. Muldoon R., and R. Austin (Novemba 2006). "Bacterial metapopulations in nanofabricated landscapes". PNAS 103 (46): 17290–295. doi:10.1073/pnas.0607971103.  Check date values in: |date= (help)

Sehemu nyingine[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Jumla
Hifadhidata