Hidrojeni
| Hidrojeni (Hydrogenium) | |
|---|---|
| Jina la Elementi | Hidrojeni (Hydrogenium) |
| Alama | H |
| Namba atomia | 1 |
| Mfululizo safu | Simetali |
| Uzani atomia | 1.00794 |
| Valensi | 1 |
| Densiti | 2700 kg/m3 |
| Ugumu (Mohs) | {{{ugumu}}} |
| Kiwango cha kuyeyuka | 14.02 K (−259.12°C) |
| Kiwango cha kuchemka | 20.27 K (−252,88 °C) |
| Asilimia za ganda la dunia | 0.88 |
Hidrojeni (kwa Kiingereza: hydrogen) ni elementi ya kikemia yenye namba atomia 1 na uzani wa atomi 1.00794. Alama yake ni H. Ni atomi nyepesi zaidi kati ya elementi zote, hivyo ina nafasi ya kwanza katika mfumo radidia.
Hidrojeni ni elementi inayopatikana kwa wingi kabisa ulimwenguni lakini si duniani. Iko ndani ya maji na katika molekuli zote za maada hai.
Muundo wa atomi
[hariri | hariri chanzo]Atomi za H zina elektroni moja tu inayozunguka kiini cha atomi. Hidrojeni ya kawaida ina protoni moja tu. Hii ni zaidi ya asilimia 98 ya isotopi zote za hidrojeni. Kuna pia isotopi yenye nyutroni moja au mbili katika kiini lakini zinatokea mara chache tu.
Kuna isotopi mbili zinazoitwa Duteri (deuterium) na Triti (tritium).
Kupatikana kwake ulimwenguni
[hariri | hariri chanzo]Duniani kwa kawaida hakuna hidrojeni ya atomi mojamoja hutokea kama gesi yenye molekuli za H2.
Masi ya jua letu ni hasa hidrojeni lakini pia sehemu kubwa ya masi za sayari kubwa yaani Mshtarii, Zohali, Uranus na Neptun. Kwa jumla asilimia 93 za atomi zote na asilimia ya masi katika mfumo wa jua letu ni H.
- Muundo wa atomi ya hidrojeni. Elektroni yenye chaji ya hasi yazunguka kiini chenye chaji ya chanja. Kiini cha kawaida kina protoni moja to; ni isotopi ya kudumu ya pekee kati ya elementi zote isiyo na nyutroni.
Matumizi
[hariri | hariri chanzo]Kiasi kikubwa cha hidrojeni hutumika katika:
- viwanda vya kusafisha mafuta kwa ajili ya hidrodesulfurinaztion[1][2], hidrodealkylation,hidroisomerization
- usanisi wa methanoli na amonia
- hidrojeni ya michanganyiko ya kikaboni isiyoshiba
Hidrojeni kwa ajili ya michakato hii hutengenezwa kila wakati mahali hapo, kwa kupasuka kwa mvuke na gesi asilia. Hidrojeni mbadala inaweza kutengenezwa kwa kutumia maji kwa kutumia nishati ya jua na upepo. Kwa sababu ya eneo lake la kijiografia, Afrika ina uwezo mzuri wa kuzalisha hidrojeni mbadala na amonia ili kupunguza utegemezi wake kwa uagizaji wa mbolea;[3][4].
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Gheorghe, Catalina Gabriela; Dragomir, Raluca-Elena (2025-10-01). "Optimization of diesel fuel quality and production by hydrotreated gasoil mixtures using Co-Mo/γAl2O3 catalysts". Reaction Kinetics, Mechanisms and Catalysis (kwa Kiingereza). 138 (5): 2759–2776. doi:10.1007/s11144-025-02913-0. ISSN 1878-5204.
- ↑ Linares, Carlos F.; Brunet, Sylvette (2023-02). "Hydrodesulfurization of dibenzothiophene on Ni–Co alloy boride catalysts supported on alumina". Reaction Kinetics, Mechanisms and Catalysis (kwa Kiingereza). 136 (1): 47–68. doi:10.1007/s11144-023-02356-5. ISSN 1878-5190.
{{cite journal}}: Check date values in:|date=(help) - ↑ Skills development workshop for hydrogen and ammonia https://www.igb.fraunhofer.de/en/reference-projects/ptx-skills-development-in-tunisia.html;
- ↑ Green Ammonia – Production of green ammonia in Morocco https://www.igb.fraunhofer.de/en/reference-projects/green-ammonia.html
| Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Hidrojeni kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |