Bomas of Kenya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kijiji cha Waluo kwenye Bomas of Kenya.

Bomas of Kenya ni makumbusho ya utamaduni wa makabila ya Kenya yanayoonyesha nyumba na vijiji vya kimila kutoka pande nyingi za nchi.

Kuna makumi ya nyumba zilizopangwa pamoja kufuatana na maeneo asilia; kwa mfano Waembu, Wakalenjin, Wakamba, Wakikuyu, Wakisii, Wakuria, Waluhya, Waluo, Wamaasai, Wamijikenda au Wataita.

Getini kuna ukumbi mkubwa wenye nafasi 3,500 uliojengwa kwa namna ya kufanana na nyumba za kimila na katika ukumbi huo kuna maonyesho ya ngoma za makabila ya Kenya. Maonyesho hayo hutembelewa na wananchi na pia watalii.

Ukumbi mkubwa ulikuwa pia mahali pa mikutano ya pekee. Mkutano wa kutunga katiba mpya ulifanyika hapo baada ya uchaguzi wa rais Mwai Kibaki lakini katiba hii haikukubaliwa baadaye na serikali.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bomas of Kenya kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.