Berbera

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru



Jiji la Berbera

Nembo
Mahali paJiji la Berbera
Mahali paJiji la Berbera
Jiji la Berbera is located in Somaliland
Jiji la Berbera
Jiji la Berbera

Mahali pa mji wa Berbera katika Somaliland

Majiranukta: 10°26′08″N 045°00′59″E / 10.43556°N 45.01639°E / 10.43556; 45.01639
Nchi Somaliland
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 60,753

Berbera ni bandari na mji wa Somalia ya Kaskazini wenye wakazi 260,000. Iko katika sehemu ya Somalia iliyojitenga kwa jina la Somaliland. Ni mji mkuu wa mkoa wa Sahil wa Somaliland na ndio bandari kuu ya bahari ya nchi hiyo. Berbera ni mji wa pwani na ulikuwa mji mkuu wa zamani wa mlinzi wa Somalia ya Kiingereza kabla ya Hargeisa.

Mawasiliano na bandari[hariri | hariri chanzo]

Kuna kiwanja cha ndege na barabara za kuunganisha mji na Hargeisa na Burao.

Biashara ya bandari ilikuwa hasa ya kondoo, uvumba na mazao mengine ya Somaliland. Ethiopia imeanza kutumia bandari kwa biashara yake ya nje baada ya kutokea kwa mafarakano kati ya Ethiopia na Eritrea. Biashara ya Ethiopia inaleta mapato makubwa zaidi kwa bandari.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Bandari ya Berbera ni bandari bora upande wa kusini wa Ghuba ya Aden. Hali ya hewa ni joto sana na halijoto inaweza kupita sentigredi 50. Mazingira yake ni jangwa au nusujangwa.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Habari za kwanza za mji zimo katika Periplus ya Bahari ya Eritrea, kitabu kilichoandikwa mnamo 200 BK. Wakati ule mji uliitwa "Malao".

Historia yake ilifuata historia ya pwani kwa jumla; mara watawala wenyeji walikuwa na madola yao madogo, mara majirani makubwa yaliingia.

Tangu mwaka 1546 Dola la Osmani lilivamia eneo lote na kumpeleka wali wake Berbera. Wakati wa udhaifu wa Waturuki athira hii ilipotea tena. Baada ya vita vya Mahdi katika Sudani Waosmani walipaswa kuondoa wanajeshi wao tena na Waingereza waliingia wakaitawala Berbera kama sehemu ya eneo lindwa la "British Somaliland Protectorate" au Somalia ya Kiingereza.

Berbera ilikuwa bandari kuu ya Waingereza na pia makao makuu ya serikali yao wakati wa miezi isiyo na joto mno.

Baada ya uhuru wa Somalia bandari ya Berbera ilikuwa na umuhimu fulani katika vita baridi kati ya Marekani na Umoja wa Kisovyeti. Serikali ya Siad Barre mwaka 1974 ilifanya mapatano ya ushirikiano na Umoja wa Kisovyeti na manowari za Kisovyeti zilipewa nafasi katika Berbera ikawa kituo cha kijeshi cha Kisovyeti. Ushirikiano huo ulifarakana tangu mwaka 1977 kwa sababu ya vita kati ya Somalia na Ethiopia na Wasovyeti walichagua kusimama upande wa Ethiopia. Barre alitafuta msaada wa Marekani na tangu 1981 Berbera ikawa kituo cha kijeshi cha Marekani.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Somaliland bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Berbera kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.