Februari

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jan - Februari - Mac
1 2 3 4 5 6 7
8 9 10 11 12 13 14
15 16 17 18 19 20 21
22 23 24 25 26 27 28
29
Kalenda ya Gregori

Mwezi wa Februari ni mwezi wa pili katika Kalenda ya Gregori. Jina lake limetokana na neno la Kilatini februare, maana yake ni "kusafisha". Mwanzoni ilikuwa mwezi wa mwisho katika kalenda ya Warumi, na kalenda hiyo ni asili ya kuongeza siku kwa mwezi wa Februari ili kusawazisha mwaka. Ndiyo maana, Februari ina siku 28 lakini katika mwaka mrefu ina siku 29. Ilitokea mara tatu katika historia Februari ilikuwa hata na siku 30.

Mwezi huo wa Februari unaanza na siku ya juma sawa na mwezi wa Machi na wa Novemba; ila katika mwaka mrefu (wenye siku 366), siku yake ya kwanza ni sawa na mwezi wa Agosti.

Simple English Wiktionary
Simple English Wiktionary
Wikamusi ya Kiswahili ina maelezo na tafsiri ya maana ya neno: