Ziwa Manyara

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

3°35′S 35°50′E / 3.583°S 35.833°E / -3.583; 35.833

Ziwa Manyara.

Ziwa Manyara ni moja kati ya maziwa ya Tanzania, la saba kwa eneo. Ukubwa wake ni Km² 470. Kina chake hakizidi mita 3.7.

Linapatikana kaskazini mashariki, katika Wilaya ya Babati, Mkoa wa Manyara.

Lipo ndani ya Bonde la Ufa la Afrika Mashariki na ndani ya hifadhi ya taifa likiwa kivutio kikubwa kwa watalii kutokana na wingi wa ndege aina ya korongo walio na mvuto mkubwa kwa kila mtu. Ndege hao huonekana kama pazia kubwa jeupe nyakati za mchana wanapokuwa ziwani kujipatia chakula na mapumziko.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Manyara bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ziwa Manyara kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.