Ziwa Eyasi
3°35′S 35°0′E / 3.583°S 35.000°E

Ziwa Eyasi (zamani pia Ziwa Njarasa, au Ziwa Hohenlohe) ni ziwa la chumvi kubwa nchini Tanzania. Liko upande wa kaskazini, karibu na Hifadhi ya Serengeti, mita 1,030 juu ya usawa wa bahari.
Eyasi ni ziwa lenye upepo mkali sana, labda kuliko maziwa yote nchini Tanzania, kwani unavuma saa 24 bila kutulia hata baadhi ya wavuvi wakubwa (wengine kutoka ziwa Nyasa, wengine kutoka ziwa Viktoria) unakuta wanashidwa na upepo, mpaka wanakimbia ziwa hilo na kwenda ziwa jirani la Manyara.
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
![]() | Makala hii kuhusu maeneo ya Tanzania bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Ziwa Eyasi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |