Lambo la Mtera

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Bwawa la Mtera)

7°08′10.3″S 35°59′12.6″E / 7.136194°S 35.986833°E / -7.136194; 35.986833Coordinates: 7°08′10.3″S 35°59′12.6″E / 7.136194°S 35.986833°E / -7.136194; 35.986833

Bwawa la Mtera, 2012.

Lambo la Mtera ni lambo lililojengwa miaka ya 1970 kati ya mkoa wa Iringa na mkoa wa Dodoma (Tanzania) ili maji ya mto Ruaha Mkuu yaweze kutumika kuzalisha umeme (80 MW) kabla hayaendelea likielekea lambo la Kidatu.

Bwawa la Mtera ni bwawa la kufua umeme kubwa zaidi lililopo nchini (km 56 x 15).

Historia[hariri | hariri chanzo]

Bwawa hili lina ukubwa wa kilomita za mraba 660 kwa uwezo kamili. Bwawa hili lina urefu wa kilometa 56 na upana wa kilometa 15 na linalishwa na mto Ruaha Mkuu na Mto Kisigo. Madhumuni ya kujengwa kwa bwawa hili ni kudhibiti kiwango cha maji katika eneo la chini la mto Ruaha lililowekwa kwa ajili ya kuzalisha umeme wa Kidatu.

Ikolojia[hariri | hariri chanzo]

Bwawa hili linachukuliwa kuwa mojawapo ya maeneo bora zaidi ya kuchunguza ndege nchini Tanzania, kwa kuwa kuna takriban miti milioni moja iliyokufa ndani yake na ina maeneo mengi ya kina. Aidha, maji mengi huwa yana samaki katika bwawa hili. Mapema miaka ya 1990 takriban tani 5000 za samaki zilivuliwa bwawani.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Öhman, May-Britt, Taming Exotic Beauties: Swedish Hydro Power Constructions in Tanzania in the Era of Development Assistance, 1960s - 1990s, Stockholm, 2007, PhD Thesis, http://www.diva-portal.org/smash/record.jsf?pid=diva2:12267

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Lambo la Mtera kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.