Trofimo wa Efeso

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Trofimo wa Efeso

Trofimo wa Efeso (kwa Kigiriki: Τρόφιμος ὁ Ἐφέσιος, Tróphimos ho Ephésios; alifariki Sinnada, Frigia, leo nchini Uturuki) alikuwa Mkristo kutoka mji huo wa Asia Ndogo (Mdo 20:4) aliyeongozana na Mtume Paulo na wenzake wengine katika sehemu ya safari yake ya tatu ya kimisionari hadi Yerusalemu[1].

Kwa kuwa alikuwa mtu wa mataifa (Mdo 21), Wayahudi walidhani kwamba Paulo alimuingiza mpaka ndani kabisa ya Hekalu, sehemu ambayo ilikuwa kwa taifa lao tu (Mdo 21:28). Ndiyo sababu ya jaribio la kumuua Paulo lililoishia katika miaka zaidi ya 4 ya kifungo kati ya Kaisarea Baharini na Roma (58-63).

Baada ya kurudishiwa uhuru, Paulo alimuandikia Timotheo kwamba alimuacha Trofimo huko Mileto kwa sababu ya ugonjwa.[2] Habari hiyo inahusu safari nyingine iliyofuata.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 19 Septemba[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Barclay, William (1955), The Acts of the Apostles (Philadelphia: Westminster Press).
  • Bock, Darrell L. (2007), "Acts: Baker Exegetical Commentary on the New Testament" (Ada, Michigan: Baker Publishing Group)
  • Bruce, F.F. (1977), Paul: Apostle of the Heart Set Free (Grand Rapids: Eerdmans).
  • Oster, Richard (1979), The Acts of the Apostles, Part II (Austin, Texas: Sweet Publishing Company).

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.