Masokwe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Sokwe (Hominoidea))
Sokwe
Sokwe Mtu
Uainishaji wa kisayansi
Domeni: Eukaryota (Viumbe walio na seli zenye kiini)
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Primates (Wanyama wanaofanana kiasi na binadamu)
Nusuoda: Haplorrhini (Wanyama wanaofanana zaidi na kima)
Oda ya chini: Simiiformes (Wanyama kama kima)
Familia ya juu: Hominoidea (Masokwe))
Ngazi za chini

Familia 2:

Masokwe (wingi wa sokwe) ni wanyama wa familia ya juu Hominoidea.

Kuna familia mbili za masokwe: Hylobatidae (masokwe wadogo au giboni) na Hominidae (masokwe wakubwa wakiwemo binadamu).

Masokwe wadogo huishi daima mitini na huteremka kwa nadra. Wana mikono mirefu ili kining'inia kutoka tawi moja hadi jingine na kutoka mti mmoja hadi mwingine. Wanatokea misitu ya tropiki ya Asia.

Masokwe wakubwa hupitisha muda pengine mrefu ardhini, orangutanu muda kidogo tu na ngagi muda mrefu sana. Takriban spishi zote zinatokea Afrika lakini orangutanu wanatokea Asia ya Mashariki.

Uainisho[hariri | hariri chanzo]

Familia ya juu Hominoidea (Masokwe)

Picha[hariri | hariri chanzo]

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.