Homo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Homo
Fuvu la kichwa katika Mkusanyo wa Palantolojia wa Makumbusho ya Kitaifa ya Ethiopia
Fuvu la kichwa katika Mkusanyo wa Palantolojia wa Makumbusho ya Kitaifa ya Ethiopia
Uainishaji wa kisayansi
Domeni: Eukaryota
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Primates (Wanyama wanaofanana kiasi na binadamu)
Familia ya juu: Hominoidea (Wanyama kama binadamu)
Familia: Hominidae (Walio na mnasaba na binadamu)
Nusufamilia: Homininae (Wanaofanana sana na binadamu)
Kabila: Hominini
Jenasi: Homo
Linnaeus, 1758
Ngazi za chini

Spishi 12:

Uenezi wa binadamu nje ya Afrika, kufuatana na ADN ya dutuvuo (mitokondria). Duara za rangi mbalimbali zinamaanisha maelfu ya miaka kabla ya leo.
Uenezi wa binadamu nje ya Afrika, kufuatana na ADN ya dutuvuo (mitokondria). Duara za rangi mbalimbali zinamaanisha maelfu ya miaka kabla ya leo.

Homo ni jenasi ambayo katika uainishaji wa kisayansi inajumlisha binadamu na spishi zilizokwishakoma zilizofanana naye sana kibiolojia. Wanasayansi wamependekeza zaidi ya spishi 12 za jenasi Homo.

Jina Homo ni la Kilatini, likiwa na maana ya "mtu", na kwa asili linahusiana na neno humus, "ardhi".[1]

Historia ya awali[hariri | hariri chanzo]

Uenezi wa jenasi Homo kwa wakati na mahali.
Homo katika miaka 600,000 ya mwisho (kutoka chini kwenda juu). [2] Homo heidelbergensis anaonyeshwa akigawanyika kati ya Waneanderthal, Wadenisova na H. sapiens. Baada ya H. sapiens kuenea kuanzia miaka 200,000 iliyopita, Waneanderthal na Wadenisova na wengineo wasiojulikana bado wanaonyeshwa kuungana na kumezwa na H. sapiens. Pia inaonyeshwa michanganyiko mingine iliyoweza ikawatokea Waafrika wa kisasa.

Jenasi hiyo imekadiriwa kuanza kuwepo miaka milioni 2.1 - 2.8 iliyopita[3][4] kutokana na spishi mojawapo ya nusukabila Australopithecina (siku hizi linatumika pia jina Hominina) iliyokuwepo kuanzia miaka milioni 5.6 hadi 1.2 iliyopita.

Spishi ya kwanza ya jenasi hiyo inawezekana ilikuwa ile ya Homo habilis, yaani mtu mwenye uwezo wa kutengeneza vifaa. Mabaki yake yalipatikana huko Oltupai (Tanzania). Huyo anafikiriwa kutokana na Australopithecus garhi ambaye kabla yake alikuwa ameanza kutengeneza vifaa kwa mawe.

Hata hivyo mnamo Mei 2010 huko Afrika Kusini yalipatikana mabaki ya Homo gautengensis, spishi inayofikiriwa na wengine kuwa ya kale kuliko Homo habilis[5], lakini wengine wanaijumlisha katika jina Homo habilis. Tena wataalamu wengine wanaona spishi hizo mbili hazistahili kuitwa Homo, ila Australopithecus.

Kutokana na Homo habilis (au Australopithecus habilis) alipatikana miaka milioni 2 iliyopita Homo erectus aliyekuwa wa kwanza kusimama daima juu ya miguu yake miwili, kuwinda na kumudu moto, na ambaye alienea kote Asia na Ulaya (aliyebaki Afrika anaitwa pia Homo ergaster) kabla ya kugawanyika katika nususpishi au spishi mpya mbalimbali kama Homo georgicus, Homo antecessor, Homo heidelbergensis, wa kwanza kujenga makazi ya kudumu na kuzika wafu, n.k. Kwa jumla Homo erectus alidumu zaidi ya miaka milioni moja. Wengi wanaona spishi nyingi zilizopendekezwa kuwa nususpishi tu za Homo erectus.

Miaka 800,000–200,000 iliyopita, wakati wa mabadiliko makubwa ya hali ya hewa, ubongo wa jenasi hiyo ulikua sana na kupata uwezo wa kufanya mambo mengi mapya katika mahusiano na katika kukabili mazingira ambayo yalizidi kubadilika na kudai maitikio tofauti ili kudumisha uhai wa jenasi yenyewe.

Kufikia miaka 100,000 au 50,000 hivi iliyopita, spishi zote za jenasi Homo zilikuwa zimekoma, isipokuwa Homo sapiens aliyekuwa ametokana na Homo heidelbergensis miaka 300,000 hivi iliyopita.

Baadhi ya wataalamu wanahesabu Homo neanderthalensis na mtu wa Denisova kama nususpishi za Homo sapiens zilizoweza kuzaliana na watu wa kisasa waliotokea Afrika.[6][7][8]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. dhghem The American Heritage Dictionary of the English Language: Fourth Edition. 2000.
  2. The horizontal axis represents geographic location; the vertical axis represents time in thousands of years ago. Based on Schlebusch et al., "Southern African ancient genomes estimate modern human divergence to 350,000 to 260,000 years ago" Science, 28 September 2017, DOI: 10.1126/science.aao6266, Fig. 3 Archived 14 Januari 2018 at the Wayback Machine. (H. sapiens divergence times) and Stringer, C. (2012). "What makes a modern human". Nature 485 (7396): 33–35. Bibcode:2012Natur.485...33S. PMID 22552077. doi:10.1038/485033a.  (archaic admixture).
  3. Stringer, C.B. (1994). "Evolution of early humans". In Steve Jones, Robert Martin & David Pilbeam (eds.). The Cambridge Encyclopedia of Human Evolution. Cambridge: Cambridge University Press. p. 242. ISBN 0-521-32370-3.  Also ISBN 0-521-46786-1 (paperback)
  4. McHenry, H.M (2009). "Human Evolution". In Michael Ruse & Joseph Travis. Evolution: The First Four Billion Years. Cambridge, Massachusetts: The Belknap Press of Harvard University Press. p. 265. ISBN 978-0-674-03175-3. 
  5. "Toothy Tree-Swinger May Be Earliest Human". Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-05-02. Iliwekwa mnamo 2012-04-28.
  6. Green RE, Krause J, et al. A draft sequence of the Neandertal genome. Science. 2010 7 Mei;328(5979):710-22. doi:10.1126/science.1188021 PMID 20448178
  7. Reich D, Green RE, Kircher M, et al. (Desemba 2010). "Genetic history of an archaic hominin group from Denisova Cave in Siberia". Nature 468 (7327): 1053–60. doi:10.1038/nature09710. PMID 21179161.
  8. Reich D ., et al. Denisova admixture and the first modern human dispersals into southeast Asia and Oceania. Am J Hum Genet. 2011 Oct 7;89(4):516-28, doi:10.1016/j.ajhg.2011.09.005 PMID 21944045.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: