Richard Strauss

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Richard Strauss.)

Richard Strauss (alizaliwa mjini Munich tar. 11 Juni 1864 na kufariki mjini Garmisch-Partenkirchen, Bavaria, 8 Septemba 1949) alikuwa mtunzi wa Opera na mwelekezi mashuhuri kutoka nchini Ujerumani. Huyu alipata bahati ya kuwa mashuhuri tangu yungali bwana mdogo na toni zake zilitumika katika mabendi mbalimbali katika Ulaya nzima.

Baada ya 1900 alitumia muda wake mwingi kwa kutunga opera. Moja kati ya opera zake zilizowahi kuwa maarufu ni "Der Rosenkavalier", aliitunga kunako mwaka wa 1910, na ilitamba saana.

Strauss alikuwa moja kati ya watunzi wakubwa wa mwisho kutunga muziki kwa mtindo wa Romantic. Alipenda sana muziki wa Wagner ambaye alipata athari kubwa za muziki wake, lakini pia alipenda na ule wa Mozart na kazi zake nyingi zaonyesha kuwa na ufaa mkubwa kama vile zilivyokuwa zile za muziki wa Mozart. Strauss alikuwa mwelekezi mzuri sana na mara nyingi aliekeza miziki yake mwenyewe.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Orodha ya Wanamuziki wa kipindi cha Romatiki
Alkan Balakirev Beethoven Bellini Berlioz Berwald Bizet Borodin Brahms Bruckner Chopin Cui Dvořák Elgar Field Franck Glinka Grieg Liszt Mahler Mendelssohn Mussorgsky Rachmaninoff Rimsky-Korsakov Saint-Saëns Schubert Schumann Smetana Strauss Tchaikovsky Verdi Wagner Wolf Weber