Nenda kwa yaliyomo

Mbale, Uganda

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mbale)
Mahali pa Mbale katika Uganda.

Mbale ni mji wa Uganda ya kusini-mashariki mwenye wakazi 76,000 chini ya mlima Elgon. Ni makao makuu ya wilaya ya Mbale. Umbali na Jinja ni 120 km na 190 km na Kampala.

Mazingira ya Mbale kuna kahawa nyingi na pia kilimo cha mazao mengine. Hivyo uchumi wa mji umetegemea kilimo na biashara ya mazao. Kuna pia kiwanda cha maziwa.

Utamaduni

[hariri | hariri chanzo]

Eneo la Mbale ni nyumbani kwa Wagishu hasa. Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Uganda kipo mjini.

Picha kadhaa za filamu "Casino Royale" zilipigwa Mbale.