Kitabu cha Yuditi : Tofauti kati ya masahihisho
d {{defaultsort}} +jamii |
d Kitabu cha Yudith umesogezwa hapa Kitabu cha Yuditi: jina kamili katika Kiswahili ni Yuditi |
(Hakuna tofauti)
|
Pitio la 11:57, 1 Novemba 2008
Kitabu cha Yudith ni kimojawapo kati ya vitabu deuterokanoni vya Biblia.
Kimo katika Septuaginta na katika Agano la Kale la Kanisa Katoliki, la Waortodoksi wengi na la baadhi ya Waprotestanti, lakini si katika Tanakh ya Uyahudi wala katika Biblia ya Waprotestanti.
Hadithi hiyo, iliyoandikwa katika karne ya 1 K.K. inahusu wakati wa mfalme Nebukadreza, na vita vyake dhidi ya Israeli (karne ya 6 K.K.).
Kinyume cha matarajio, Yudith, mwanamke wa kabila la Yuda, aliweza kupata ushindi kwa imani na ushujaa wake.
Habari hiyo ya ajabu ilipata mwangwi kwa wingi katika sanaa mbalimbali.
Wengi wanaona katika Yudith kielelezo cha Bikira Maria katika mapambano dhidi ya shetani, hasa kutokana na maneno yafuatayo: "Umebarikiwa, binti yangu, usoni pa Mungu Aliye Juu, kuliko wanawake wote duniani. Na ahimidiwe Bwana Mungu, Muumba mbingu na nchi, aliyekuongoza hata ukampiga kichwa mkuu wa adui zetu" (Yudith 13:18).
Kama vitabu vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.
Mwanzo Kutoka Walawi Hesabu Kumbukumbu Yoshua Maamuzi Ruthu Samueli I Samueli II Wafalme I Wafalme II Mambo ya Nyakati I Mambo ya Nyakati II Ezra Nehemia TobitiDK YuditiDK Esta Wamakabayo IDK Wamakabayo IIDK Yobu Zaburi Methali Mhubiri Hekima DK Yoshua bin SiraDK Wimbo Ulio Bora Isaya Yeremia BarukDK Ezekieli Danieli Hosea Yoeli Amosi Obadia Yona Mika Nahumu Habakuki Sefania Hagai Zekaria Malaki - Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.