Justin mfiadini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha takatifu ya Kirusi ya Mt. Justin.

Justin (pia Yustino Shahidi; Kiing. Justin Martyr; alizaliwa Flavia Neapolis, leo Nablus, Palestina, 103 hivi - Roma, Italia, kati ya 162 na 168) alikuwa mwanafalsafa ambaye, kisha kuongokea hekima halisi katika ukweli wa Yesu, aliishika katika mwenendo wa maisha yake, aliifundisha chuoni, akieneza na kutetea Ukristo hata kwa maandishi maarufu, na hatimaye akakamilisha ushahidi wake kwa kuuawa katika dhuluma ya kaisari Marko Aureli wa Dola la Roma.

Ni kwamba, baada ya kumpatia kaisari huyo utetezi wa Wakristo, alitolewa kwa mtawala Rusticus akakiri imani mbele yake na kwa ajili hiyo aliuawa pamoja na wanafunzi wake sita (Karitoni, Karito, Evelpisto, Gerasi, Peoni na Liberiani) [1].

Hati za mateso yao zimetunzwa hadi leo[2].

Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki, Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki, Walutheri na Waanglikana kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Juni[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Maandishi yake[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Iustini opera, 1636

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.