Kunguni-chura

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Gelastocoridae)
Kunguni-chura
Nerthria sp. nchini Australia
Nerthria sp. nchini Australia
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye mwili wa pingili na miguu ya kuunga wasio na ugwe wa mgongo kama wadudu, nge, buibui)
Nusufaila: Hexapoda (Arithropodi wenye miguu sita)
(bila tabaka): Dicondylia (Wadudu walio na mandibula zenye condyle mbili)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Nusungeli: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda ya juu: Paraneoptera
Oda: Hemiptera
Haeckel, 1896
Nusuoda: Heteroptera
Oda ya chini: Nepomorpha
Familia ya juu: Ochteroidea
Familia: Gelastocoridae
Kirkaldy, 1897
Ngazi za chini

Nusufamilia 2; jenasi 3, 1 katika Afrika ya Mashariki:

Kunguni-chura ni wadudu wadogo wa familia Gelastocoridae katika oda ya chini Nepomorpha ya oda Hemiptera wanaofanana na vyura wadogo kwa sura na tabia. Kuna spishi takriban 120 duniani kote, isipokuwa Ulaya, lakini spishi 1 tu barani Afrika[1].

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

Kunguni-chura wana urefu wa mm 6-15. Mwili wao ni imara na una umbo la duaradufu .Miguu yao ya mbele ni imara na inatumiwa kukamata mbuawa. Miguu ya kati na ya nyuma inatumiwa kwa kuruka juu ya mbuawa[2]. Sehemu za kinywa ni imara na kama sindano. Kwa kawaida wadudu hao hawana mabawa ya nyuma na kwa hivyo hawawezi kuruka angani. Mara nyingi mabawa ya mbele yameunganishwa. Vipapasio vimefichwa katika mifuo ya uso. Rangi ni kama kamafleji na hata wanaweza kubadilisha rangi ili kuilingana na mazingira yao.

Biolojia[hariri | hariri chanzo]

Wadudu hao huishi kando ya maji kwa kawaida, lakini spishi kadhaa zimepatikana mbali na maji. Huwinda vertebrata wadogo kwa kuruka juu yao ambao wanawatoboa kwa kinywa chao na kufyonza yaliyomo.

Mayai hutagwa kwenye mchanga[3]. Tunutu (lava) hujifunika kwa tabaka la chembe za mchanga ili kutoonekana dhidi ya nyuma[4].

Spishi ya Afrika ya Mashariki[hariri | hariri chanzo]

  • Nerthra grandicollis

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Randall T. Schuh; James Alexander Slater (1996). True Bugs of the World (Hemiptera:Heteroptera): Classification and Natural History (toleo la 2). Cornell University Press. uk. 116-117. ISBN 978-0801420665. 
  2. Borror DJ, Tripplehorn CA, Johnson NF (1989) An Introduction to the Study of Insects, 6th edition. Harcourt Brace College Publishers. New York. pg 213
  3. Triplehorn, Charles A.; Johnson, Norman F. (2005). Borror and Delong's Introduction to the Study of Insects, 7th Edition (kwa English). Belmont, CA: Books/Cole, Cengage Learning. ku. 290. ISBN 978-0-03-096835-8. 
  4. Alan Weaving; Mike Picker; Griffiths, Charles Llewellyn (2003). Field Guide to Insects of South Africa. New Holland Publishers, Ltd. ISBN 1-86872-713-0.