Kunguni-maji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Nepomorpha)
Kunguni-maji
Mwogeleaji-juuchini (Notonecta glauca)
Mwogeleaji-juuchini (Notonecta glauca)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye mwili wa pingili na miguu ya kuunga wasio na ugwe wa mgongo kama wadudu, nge, buibui)
Nusufaila: Hexapoda (Arithropodi wenye miguu sita)
(bila tabaka): Dicondylia (Wadudu walio na mandibula zenye condyle mbili)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Nusungeli: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda ya juu: Paraneoptera
Oda: Hemiptera
Haeckel, 1896
Nusuoda: Heteroptera
Ngazi za chini

Oda za chini 2 za kunguni-maji, familia za juu 11:

Kunguni-maji ni wadudu wadogo hadi wakubwa wa oda za chini Gerromorpha na Nepomorpha katika oda Hemiptera ya nusungeli Pterygota (wenye mabawa) ambao huishi majini. Mabawa yao ya mbele ni nusu magumu na nusu kama viwambo. Kunguni hao hula wadudu wengine ama hai au waliokufa, na spishi kubwa hula samaki na amfibia wadogo pia.

Mifano ya wadudu hao ni wendamaji na kunguni-bahari (familia Gerridae), wapima maji (Hydrometridae), nge-maji (Nepidae), waogeleaji-juuchini (Notonectidae), kunguni-makasia (Corixidae), kunguni-maji wakubwa (Belostomatidae), kunguni-maji watambaazi (Naucoridae), kunguni-chura (Gelastocoridae)

Biolojia[hariri | hariri chanzo]

Kundi la kunguni-maji lina spishi ndogo sana (mm 2) na spishi kubwa sana (sm 12) zilizomo miongoni mwa wadudu wakubwa kabisa duniani. Spishi za Gerromorpha hutembea juu ya maji au huishi katika mahali panyevu, lakini zile za Nepomorpha huogelea chini ya maji kwa kawaida.

Takriban spishi zote ni mbuai wa wadudu wengine na spishi kubwa vilevile mbuai wa samaki na amfibia wadogo, lakini hula mizoga pia. Spishi nyingine hula mimea ya majini au dutu za mimea. Sehemu za kinywa zina umbo la kutoboa mbuawa ili kufyonza damu yake. Spishi fulani, kama nge-maji na kunguni-makasia, zinaweza kutoboa ngozi ya watu na kuuma sana.

Spishi kadhaa za Afrika ya Mashariki[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]