Mpima maji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Hydrometridae)
Mpima maji
Hydrometra stagnorum
Hydrometra stagnorum
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye mwili wa pingili na miguu ya kuunga wasio na ugwe wa mgongo kama wadudu, nge, buibui)
Nusufaila: Hexapoda (Arithropodi wenye miguu sita)
(bila tabaka): Dicondylia (Wadudu walio na mandibula zenye condyle mbili)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Nusungeli: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda ya juu: Paraneoptera
Oda: Hemiptera
Nusuoda: Heteroptera
Oda ya chini: Gerromorpha
Familia ya juu: Hydrometroidea
Familia: Hydrometridae
Billberg, 1820
Ngazi za chini

Nusufamilia 3, jenasi 10:

Wapima maji ni wadudu wadogo wa familia Hydrometridae katika oda ya chini Gerromorpha ya oda Hemiptera wanaofanana na kijiti kidogo kana kwamba kupima maji. Spishi nyingi hutembea juu ya maji sehemu ya wakati, lakini nyingine huishi katika mahali panyevu, hata ndani ya mapango. Jenasi 2 zinatokea Afrika: Heterocleptes na Hydrometra.

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

Wapima maji wana urefu wa mm 3-22[1]. Wana mwili uliorefuka na mwembamba sana, haswa spishi za jenasi Hydrometra, ambazo kichwa chao ni takriban theluthi moja ya urefu wa mwili na vipapasio vinaweza kukaribia nusu ya urefu wa mwili. Spishi zote zina miguu mirefu na sehemu za kinywa ndefu zinazoweza kupenya. Spishi nyingi hazina mabawa, ingawa baadhi zina mabawa. Wana rangi ya kijivu au kahawia.

Biolojia[hariri | hariri chanzo]

Wadudu hawa ni wa kawaida kiasi na wamepatikana duniani kote. Tofauti kubwa zaidi, hata hivyo, inapatikana ndani ya ukanda wa tropiki na Hydrometra pekee inatokea mahali pengine. Kwa kawaida hutokea kwenye nyuso za maji kwenye kingo za maziwa, mabwawa na maeneo oevu, mara nyingi ambapo samaki hawapo. Wanapendelea uoto wa majini au wanatembea polepole kwenye maji tulivu, lakini watasogea haraka wakisumbuliwa[2]. Wako mbuai na watajilisha kwa wadudu wanaoishi juu ya maji, wadudu mkia-fyatuo wakiwa mojawapo ya milo wanayopenda zaidi. Pia hufyonza wadudu walioanguka ndani ya maji. Spishi nyingi kiasi huishi katika maeneo yenye unyevunyevu, baadhi katika mapango. Wote ni wapandaji wakubwa na hupanda mimea kutafuta wadudu wa kula. Hutumia kinywa chao chenye ndaka ili kupenya mbuawa wao na kuingiza mate. Kisha hufyonza tishu zilizokuwa kiowevu[3].

Mayai hutagwa kwenye mashina ya mimea. Kwa ujumla wamegundulika kuwa na hatua tano ya lava na kuwa wapevu ndani ya wiki nne hadi sita.

Spishi kadhaa za Afrika[hariri | hariri chanzo]

  • Heterocleptes hoberlandti
  • Heterocleptes schoutedeni
  • Heterocleptes tuberculatus
  • Hydrometra aegyptia
  • Hydrometra africana
  • Hydrometra ambulator
  • Hydrometra albolineolata
  • Hydrometra bifurcata
  • Hydrometra carayoni
  • Hydrometra cavernicola
  • Hydrometra chopardi
  • Hydrometra fanjahira
  • Hydrometra goodi
  • Hydrometra grassei
  • Hydrometra isaka
  • Hydrometra madagascarensis
  • Hydrometra marani
  • Hydrometra phytophila
  • Hydrometra poissoni
  • Hydrometra rhodesiana
  • Hydrometra seychellensis
  • Hydrometra smithi
  • Hydrometra somaliensis
  • Hydrometra stagnorum
  • Hydrometra transvaalensis
  • Hydrometra turneri
  • Hydrometra ugandae
  • Hydrometra yamoussoukroi

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]