Mwogeleaji-juuchini kibete

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Pleidae)
Mwogeleaji-juuchini kibete
Plea minutissima
Plea minutissima
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye mwili wa pingili na miguu ya kuunga wasio na ugwe wa mgongo kama wadudu, nge, buibui)
Nusufaila: Hexapoda (Arithropodi wenye miguu sita)
(bila tabaka): Dicondylia (Wadudu walio na mandibula zenye condyle mbili)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Nusungeli: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda ya juu: Paraneoptera
Oda: Hemiptera
Nusuoda: Heteroptera
Oda ya chini: Nepomorpha
Familia ya juu: Notonectoidea
Ngazi za chini

Familia 2; jenasi 26, 7 katika Afrika:

Waogeleaji-juuchini vibete ni wadudu wadogo sana wa maji wa familia Helotrephidae na Pleidae katika oda ya chini Nepomorpha ya oda Hemiptera wanaoogelea mgongo ukiwa chini. Pleidaei ina spishi 41, ambazo 3 zinatokea katika Afrika, na Helotrephidae ina spishi nyingi, nyingi sana katika Asia ya Kusini na Kusini-mashariki na 23 katika Afrika. Wadudu hawa ni mbuai.

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

Wadudu hawa wana ukubwa wa mm 1.5-3.5[1][2]. Mwili wao una umbo la duaradufu na mgongo wa mbenuko wa juu, unaofanana na mbawakawa wadogo sana. Miguu ya nyuma si mirefu sana, haina nywele na haifai sana kuogelea, ikitumiwa zaidi kwa kusota kati ya mimea ya maji. Spishi kadhaa zina mabawa yaliyopunguka na kwa hivyo haziwezi kuruka. Walakini, spishi nyingi zina mabawa yaliyokua kikamilifu, lakini hata hivyo haziruki vizuri sana. Katika Helotrephidae, kichwa na pronoto zimeunganishwa[3].

Biolojia[hariri | hariri chanzo]

Waogeleaji-juuchini vibete wakiogelea, hutumia miguu yao ya nyuma. Ingawa hiyo haina umbo kama ile ya waogeleaji-juuchini wakubwa zaidi, inafanya kazi vizuri kwa sababu ya udogo wa wadudu hawa. Hata hivyo, mara nyingi sana, hutambaa kati ya uoto wa majini au kwenye miamba iliyo chini ya maji. Ili kupumua, hukusanya hewa kutoka kwenye uso wa maji, ambayo huhifadhiwa kati ya nywele fupi kwenye upande wao wa tumbo (Pleidae) au chini ya mabawa ya mbele (Helotrephidae). Hutokea katika maji matamu tulivu yenye mimea, ingawa baadhi ya Helotrephidae huishi kwenye miamba chini ya maporomoko ya maji. Chakula chao ni gegereka wadogo, viluwiluwi wa mbu na invertebrata wengine wadogo, hata wadudu mkia-fyatuo wa maji ambao huwanyakua usoni kwa maji. Kama vile kunguni-maji wengine, huingiza mate ndani ya mbuawa wao ili kuyeyusha tishu, ambazo kisha hufyonza. Waogeleaji-juuchini vibete hawashiki mbuawa wadogo kuliko wao, kama vidudu-gurudumu, kwa sababu miguu yao mifupi ya mbele haiwezi kuwashughulikia.[4].

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Helotrephidae

  • Esakiella acuminata
  • Esakiella buea
  • Esakiella chinai
  • Esakiella didyi
  • Esakiella eremita
  • Esakiella gereckei
  • Esakiella goldenschmidti
  • Esakiella hancocki
  • Esakiella hungerfordi
  • Esakiella hutchinsoni
  • Esakiella madli
  • Esakiella marlieri
  • Esakiella milloti
  • Esakiella mutsoriai
  • Esakiella nairobi
  • Esakiella nimbae
  • Esakiella rivularius
  • Esakiella starmuehlneri
  • Esakiella wenchiana
  • Idiocoris lithophilus
  • Paralimnotrephes villiersi
  • Paskia minutissima
  • Pseudohydrotrephes moramongae

Pleidae

  • Paraplea piccanina
  • Paraplea pullula
  • Plea minutissima

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://bugguide.net/node/view/49815
  2. Zettel, H. (2002) The Helotrephidae (Insecta: Heteroptera) of the Philippine Islands. Annalen des Naturhistorischen Museums in Wien. Serie B. 104: 45-97
  3. Zettel, H., Papácek, M. & Kovac, D. (2011) Guide to the aquatic Heteroptera of Singapore and Peninsular Malaysia: VII. Family Helotrephidae. The Raffles Bulletin of Zoology 59: 171-179.
  4. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2022-12-17. Iliwekwa mnamo 2022-12-17.