Chama cha Mpira wa Kikapu Marekani

Chama cha Mpira wa Kikapu Marekani (kwa Kiingereza: National Basketball Association au kifupi NBA) ni chama cha kitaifa cha timu za mpira wa kikapu zinazocheza katika ligi kuu huko Amerika ya Kaskazini ikijumuisha timu 29 toka Marekani na timu 1 toka Kanada. Ni moja ya ligi kubwa za kulipwa za mpira wa kikapu nchini Marekani na Kanada na ni ligi kubwa kabisa ya mpira wa kikapu duniani.
Ligi hii ilianzishwa huko New York City Juni 6, 1946, ikiitwa Chama cha Mpira wa Kikapu Amerika (BAA). Ilichukua jina lake la sasa Agosti 3, 1949 baada ya kuungana na mshindani wake Ligi ya Kitaifa ya Mpira wa Kikapu National Basketball League (NBL).
Msimu wa ligi hii huanza Oktoba na kumalizika Aprili, kila timu ikicheza michezo 82. Wachezaji wa ligi hii ni wachezaji wanaolipwa mshahara mkubwa duniani kwa kutazama wastani wa mshahara kwa mwaka.[1][2]
Chama hiki ni mwanachama wa USA Basketball (USAB),[3] chama kinachotambuliwa na [Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Kikapu]] (the International Basketball Federation - FIBA). Makao yake makuu yako Midtown Manhattan, wakati studio za NBA Entertainment na NBA TV ziko Secaucus, New Jersey.
Orodha ya timu za ukanda wa Mashariki (kwa Kiingereza: "Eastern Conference"):
- Atlanta Hawks
- Boston Celtics
- Charlotte Hornets
- Chicago Bulls
- Cleveland Cavaliers
- Detroit Pistons
- Indiana Pacers
- Miami Heat
- Milwaukee Bucks
- New Jersey Nets
- New York Knicks
- Orlando Magic
- Philadelphia 76ers
- Toronto Raptors
- Washington Wizards
Orodha ya timu za ukanda wa Magharibi (kwa Kiingereza: "Western Conference"):
- Dallas Mavericks
- Denver Nuggets
- Golden State Warriors
- Houston Rockets
- Los Angeles Clippers
- Los Angeles Lakers
- Memphis Grizzlies
- Minnesota Timberwolves
- New Orleans Pelicans
- Oklahoma City Thunder
- Phoenix Suns
- Portland Trail Blazers
- Sacramento Kings
- San Antonio Spurs
- Utah Jazz
- Michezo ya video
- NBA 06
- NBA 07
- NBA 08
- NBA 09: The Inside
- NBA 2K
- NBA Ballers
- NBA Ballers: Chosen One
- NBA Ballers: Phenom
- NBA Ballers: Rebound
- NBA Hangtime
- NBA Hoopz
- NBA Jam
- NBA Live
- NBA Showtime: NBA on NBC
- NBA Street
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ REVEALED: The world's best paid teams, Man City close in on Barca and Real Madrid. SportingIntelligence.com (May 1, 2012). Iliwekwa mnamo June 11, 2012.
- ↑ The NBA is the highest-paying sports league in the world. Iliwekwa mnamo May 20, 2015.
- ↑ Members of USA Basketball. USA Basketball (June 28, 2015). Jalada kutoka ya awali juu ya June 30, 2015. Iliwekwa mnamo June 28, 2015.
Soma zaidi[hariri | hariri chanzo]
- Rosen, Charley (2009). The First Tip-Off: The Incredible Story of the Birth of the NBA. McGraw-Hill Professional. ISBN 0-07-148785-9.
- (2007) Sports Illustrated: The Basketball Book. Sports Illustrated. ISBN 1-933821-19-1.
- Havlicek, John (2003). NBA's Greatest 1st edition. DK. ISBN 0-7894-9977-0.
- Peterson, Robert W. (2002). Cages to Jump Shots: Pro Basketball's Early Years. Lincoln: University of Nebraska Press. ISBN 0-8032-8772-0.
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
Ligi ina tovuti ya Kiingereza yenye mtazamo zaid wa kimataifa [1] yenye habari toka nje ya Marekani ya Kaskazini. Tovuti nyingine ni za Kiingereza zenye ushirikiano na vyombo vya habari nje ya Marekani kama vile Africa, Australia, Canada, India, New Zealand, na Philippines.
- Chama cha Wachezaji wa Mpira wa kikapu
- Chama cha Marefa wa Mpira wa Kikapu
- Takwimu na histori Archived 22 Februari 2011 at the Wayback Machine.
- NBA & ABA Transactions Archive
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya michezo bado ni mbegu. Je, unajua kitu zaidi kuhusu Chama cha Mpira wa Kikapu Marekani kama historia yake, uenezi au kanuni zake? Labda unaona katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine habari zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |