Basili Mzee

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Basili Mzee (alifariki Kaisarea ya Kapadokia karne ya 4) alikuwa mtoto wa Makrina Mzee, halafu mhubiri maarufu huko Caesarea Mazaca[1]. Yeye na mke wake Emelia wa Kaisarea walijulikana kwa imani yao[2] iliyowafanya wafukuziwe jangwani wakati wa dhuluma ya kaisari Maximian[3].

Familia yao ilikuwa na watoto 10, waliosaidiwa malezi na bibi yao, Makrina Mzee. Babu yao alikuwa mfiadini. Wote wawili wanaheshimiwa kama watakatifu, kama vile Basili Mkuu na watoto wao wengine 4: Makrina Kijana aliyekuwa mmonaki, Petro wa Sebaste aliyekuwa askofu na mwanateolojia huko Armenia, Naukratio aliyekuwa mkaapweke, na Gregori wa Nisa ambaye alifanywa na Basili kuwa askofu wa Nisa|mji huo akaandika vitabu bora kuhusu teolojia na maisha ya Kiroho[4][5].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[6].

Sikukuu yake huadhimishwa hasa tarehe 30 Mei pamoja na mke wake [7].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.