Emelia wa Kaisarea

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Emelia wa Kaisarea (alifariki Kaisarea ya Kapadokia 30 Mei 375) alikuwa mke wa mhubiri maarufu Basili Mzee huko Caesarea Mazaca. Wote wawili walijulikana kwa imani yao iliyowafanya wafukuziwe jangwani wakati wa dhuluma ya kaisari Maximian[1].

Familia yao ilikuwa na watoto 10, waliosaidiwa malezi na bibi yao, Makrina Mzee. Babu yao alikuwa mfiadini. Wote wawili wanaheshimiwa kama watakatifu, kama vile Basili Mkuu na watoto wao wengine 4: Makrina Kijana aliyekuwa mmonaki, Petro wa Sebaste aliyekuwa askofu na mwanateolojia huko Armenia, Naukratio aliyekuwa mkaapweke, na Gregori wa Nisa ambaye alifanywa na Basili kuwa askofu wa mji huo akaandika vitabu bora kuhusu teolojia na maisha ya Kiroho.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[2].

Sikukuu yake huadhimishwa hasa siku ya kifo chake pamoja na mume wake[3] au siku nyingine.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.