Agape

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sehemu ya mfululizo wa makala kuhusu mapendo

Moyo katika mapokeo ya Ulaya
ni mchoro unaowakilisha mapendo.
Vipengele Msingi
Mapendo kadiri ya sayansi
Mapendo kadiri ya utamaduni
Upendo (fadhila)
Upendo safi
Kihistoria
Mapendo ya kiuchumba
Mapendo ya kidini
Aina za hisia
Mapendo ya kiashiki
Mapendo ya kitaamuli
Mapendo ya kifamilia
Mapendo ya kimahaba
Tazama pia
Mafungamano ya binadamu
Jinsia
Tendo la ndoa
Maradhi ya zinaa
Siku ya wapendanao

Agape ni neno la lugha ya Kigiriki (ἀγάπη, agape) lenye maana ya "upendo". Ni muhimu hasa katika maandiko ya Agano Jipya na maandiko mengine ya Ukristo, unaojitambulisha kama dini ya upendo.

Kigiriki kina maneno mbalimbali kwa jambo linaloitwa "upendo" katika lugha mbalimbali ambazo zina neno moja tu. Kwa hiyo "agape" inataja maana ya pekee ya "upendo" ambayo ni upendo wa kindugu au upendo wa Mungu. Upande mwingine wa upendo kwa Kigiriki ni "philia" (undugu, pendo lisilo la kingono) na mwingine ni "eros" ambayo ni mapenzi yenye tabia ya kingono.

Agape ni aina ya upendo isiyotafuta faida wala tamaa wala ridhaa.

Katika maandiko ya Kikristo agape inamaanisha:

  • Upendo wa Mungu hasa Kristo kwa binadamu na uumbaji wake
  • Upendo wa binadamu kwa Mungu
  • Upendo wa binadamu kwa mtu mwingine

Chanzo kwa Wakristo ni amri (kiasili ya Agano la Kale) jinsi inavyopatikana kwa mfano katika Luka 10:27:

"Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe"

Wakati mwingine namna ya pekee ya kuadhimisha Chakula cha Bwana huitwa "agape".

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Agape kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.