Nembo ya Kenya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nembo ya Kenya

Nembo ya Kenya huonyesha simba wawili wanaoshika mishale na ngao ya Maasai. Ngao huoneyesha rangi za taifa zilizogawanyika katika sehemu nne.

  • Nyeusi humaanisha watu wazaliwa Kenya
  • Kijani humaanisha kilimo na maliasili
  • Nyekundu humaanisha mapambano kupata uhuru
  • Nyeupe humaanisha umoja na usalama

Sehemu nyekundu huonyesha jogoo anayeshika shoka; hii humaanisha maisha bora. Ngao na simba wamesimama juu ya Mlima Kenya. Chini ya ngao kimeandikwa Harambee.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

http://www.kenyarchives.go.ke/emblem.htm Archived 8 Mei 2006 at the Wayback Machine.