Mwigulu Nchemba
| Mwigulu Nchemba | |
| Aliingia ofisini 13 Novemba 2025 | |
| Rais | Samia Suluhu |
|---|---|
| mtangulizi | Kassim Majaliwa |
| Muda wa Utawala 31 Machi 2021 – 3 Novemba 2025 | |
| Rais | Samia Suluhu |
| mtangulizi | Philip Mpango |
| Muda wa Utawala 2 Mei 2020 – 31 Machi 2021 | |
| Rais | John Magufuli |
| mtangulizi | Augustine Mahiga |
| aliyemfuata | Palamagamba Kabudi |
Waziri wa Mambo ya Ndani | |
| Muda wa Utawala 11 Juni 2016 – 1 Julai 2018 | |
| Rais | John Magufuli |
| mtangulizi | Stephen Wassira |
| aliyemfuata | Alphaxard Lugola |
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi | |
| Muda wa Utawala Novemba 2015 – Juni 2016 | |
| Rais | John Magufuli |
| aliyemfuata | Charles Tizeba |
| Aliingia ofisini Novemba 2010 | |
| mtangulizi | Juma Hassan Killimbah |
| tarehe ya kuzaliwa | 7 Januari 1975 Makunda, Wilaya ya Iramba |
| utaifa | Mtanzania |
| chama | CCM |
| mhitimu wa | University of Dar es Salaam |
Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (alizaliwa Makunda, Wilaya ya Iramba, Mkoa wa Singida, Tanzania, 7 Januari 1975) ni mtaalamu wa uchumi na mwanasiasa wa CCM nchini Tanzania , ambaye amehudumu kama Mbunge aliyechaguliwa wa Jimbo la Iramba Magharibi tangu mwaka 2010. Mnamo Novemba 13, 2025, Rais Samia Suluhu alimteua kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, akimrithi Kassim Majaliwa. Kabla ya uteuzi wake huo, alihudumu kama Waziri wa Fedha na Mipango katika Baraza la Mawaziri la Tanzania tangu 31 Machi 2021.
Historia na elimu
[hariri | hariri chanzo]Nchemba alisoma Shule ya Msingi Makunda, kisha kuhamia Shule ya Sekondari Ilboru kwa ajili ya elimu ya kati. Alimalizia masomo yake ya A-Level katika Shule ya Sekondari Mazengo, akihitimu mwaka 2000 akiwa na stahiki sawa na Diploma ya Shule ya Sekondari. Mnamo mwaka 2001 alikubaliwa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akihitimu shahada ya Kwanza ya Uchumi mwaka 2004. Baadaye alipata Shahada ya Uzamili ya Uchumi mwaka 2006, pia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Baadae alipata Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Uchumi kutoka chuo hicho hicho.[1] [2]
Kazi na siasa
[hariri | hariri chanzo]Amechaguliwa kuwa mbunge wa Iramba Magharibi mwaka 2010 akarudishwa bungeni kwa kipindi cha 2015 – 2020. Kwanza, alihudumu kama naibu waziri wa fedha. Baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2015, Rais John Magufuli alimteua kuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi. Mwaka 2016 alibadilishwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Wakati huo, wizara yake ilihusishwa na changamoto kadhaa, ikiwa ni pamoja na ulaji rushwa, matumizi mabaya ya fedha, na ongezeko la ajali barabarani ingawa mhusika hakujulikana[3]. Rais pia alitaja mkataba wa Lugumi ambapo polisi walipata hasara ya Tsh bilioni 30, pamoja na kashfa ya mkataba wa vifaa vibovu katika idara ya NIDA, uigizaji wa magari na malori 700 kwa polisi, na mkataba usio halali wa sare za polisi. Zaidi ya hayo, jinsi Nchemba alivyoshughulika na kanisa la KKKT kufuatia barua ya maaskofu ya Pasaka 2018 iliongeza wasiwasi wa rais dhidi yake[4].
Mnamo Februari 2019, Nchemba aliumia katika ajali ambapo gari lake liligonga pundamilia wawili barabarani[5].
Tarehe 2 Mei 2020, aliteuliwa kuwa waziri wa Sheria na Katiba kufuatia kifo cha waziri Augustine Philip Mahiga[6]. Mnamo 31 Machi 2021, baada ya kuundwa kwa Baraza la Mawaziri la Sita la Tanzania, Dk. Philip Mpango alipandishwa kuwa Makamu wa Rais, na Nchemba akachukua wadhifa wa Waziri wa Fedha na Mipango. Mnamo 4 Julai 2023, aliendelea kushikilia wadhifa wa Waziri wa Fedha, huku Wizara ya Mipango ikiwekwa chini ya Ofisi ya Rais. Hatimaye, aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania mnamo 13 Novemba 2025 kufuatia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Hitilafu ya kutaja: Invalid
<ref>tag; no text was provided for refs named3R - ↑ The Citizen Reporter (1 Aprili 2021). "What Mwigulu Nchemba brings to the table as finance minister". The Citizen (Tanzania). Dar es Salaam. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-04-02. Iliwekwa mnamo 2 Aprili 2021.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ Why Nchemba was sacked from Home Affairs docket Ilihifadhiwa 15 Julai 2020 kwenye Wayback Machine., The Citizen, 3 Julai 2018, iliangaliwa Mei 2020
- ↑ Out in the cold, which way Mwigulu?, The Citizen, 4 Julai 2018, iliangaliwa Mei 2020
- ↑ Tanzania’s former Home Affairs Minister cheats death as car hits donkeys, The Citizen, 13 Februari 2019, iliangaliwa Mei 2020
- ↑ President Magufuli reinstates Mwigulu Nchemba to cabinet, The Citizen, 2 Mei 2020
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]| Ofisi za Kisiasa | ||
|---|---|---|
| Alitanguliwa na Kassim Majaliwa |
Waziri Mkuu wa Tanzania 2025- |
Akafuatiwa na [[]] |
| Makala hii kuhusu kuhusu mwanasiasa wa Tanzania bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mwigulu Nchemba kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |