Marselo wa Tanja

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Marcellus wa Tanja)
Picha takatifu ya Marselo na Kasiani wa Tanja katika kanisa la Kiorthodoksi la Rabat, Moroko.

Marselo wa Tanja (au Marselo akida) alikuwa askari Mkristo huko Tanja (leo nchini Moroko) aliyefia dini yake kwa kukatwa kichwa katika dhuluma ya kaisari Diocletian mwanzoni mwa karne ya 4.

Tarehe inayotajwa na mapokeo ni 3 Desemba 298[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 30 Oktoba[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Geoffrey Ernest Maurice de Sainte-Croix, Christian Persecution, Martyrdom, and Orthodoxy, Oxford University Press, 2006, p. 172:"we must admit that we know nothing of the date or the circumstances of his execution"
  2. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.