Kinga wa Hungaria

Kinga wa Hungaria au wa Polandi (pia Kunegunda, Kunigunda, Kioga, Zinga; Esztergom, Hungaria, 5 Machi 1224 – 24 Julai 1292) alikuwa malkia, binti mfalme Bela IV wa Hungaria, na mke wa Boleslao V wa Polandi.[1]
Familia yake asili ilizaa watakatifu mbalimbali, yeye akiwa mmojawapo. Katika ndoa yake inasadikika kwamba waliishi kama kaka na dada, ingawa mwanzoni mumewe hakupenda[2].
Pamoja na hayo, Kinga alijitahidi sana kuwatendea kwa huruma mafukara na wagonjwa, wakiwemo wakoma.
Alipofiwa mumewe (1279), aliuza mali yake yote na kugawa mapato yote kwa maskini.
Halafu alikataa madaraka yake ya kiserikali akajiunga na monasteri ya Waklara aliyokuwa ameianzisha huko Sandec (Stary Sącz), alipoishi hadi mwisho katika sala tu, asipotaka kabisa itajwe asili yake.
Papa Aleksanda VIII alimtangaza mwenye heri mwaka 1690. Halafu Papa Yohane Paulo II alimtangaza mtakatifu tarehe 16 Juni 1999.
Tangu mwaka 1695 anaheshimiwa kama msimamizi wa Polandi na Lithuania.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Profile, books.google.com; accessed 17 January 2014.
- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/91017
- ↑ Martyrologium Romanum
| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |