Jeromu Emiliani
Jump to navigation
Jump to search
Jeromu Emiliani (1486 – 8 Februari 1537) alikuwa padri na mtawa nchini Italia.
Ametambuliwa na Kanisa Katoliki kuwa mtakatifu na msimamizi wa mayatima.
Sikukuu yake ni tarehe 8 Februari[1].
Maisha[hariri | hariri chanzo]
Jeromu Emiliani alizaliwa mjini Venisi huko Italia mwaka 1486.
Kwanza alikuwa askari, lakini baadaye akaacha kazi hiyo ili ajitoe mhanga kuwahudumia maskini; akawapa mali yake yote.
Baada ya kupata upadri (1518) alianzisha Utawa wa Makleri ulioitwa Wasomaska, ili kuwasaidia mayatima na maskini.
Alifariki Somasca, karibu na mji wa Bergamo, mwaka 1537.
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- "Sala ya Kanisa - Vipindi vya Liturjia", Toleo la Tatu 1996, Ndanda - Peramiho: Benedictine Publications, uk.1283
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- St. Jerome Emiliani. Catholic Encyclopedia.
- Sanamu yake kama mwanzilishi katika Basilika la Mt. Petro (Vatikani).
![]() |
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |