Gaudensi wa Brescia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Gaudensi wa Brescia (alifariki 410 BK) anakumbukwa kama askofu wa Brescia (Italia Kaskazini) kuanzia mwaka 387 hadi kifo chake.

Mhubiri maarufu, rafiki wa Yohane Krisostomo, aliwekwa wakfu na Ambrosi wa Milano, ingawa kwanza alitaka kukataa cheo cha uaskofu[1] akachangia juhudi za kukamilisha uenezi wa Ukristo kote Italia baada ya Kaisari Theodosi I kuufanya dini rasmi ya Dola la Roma.

Vimetufikia vitabu vyake ishirini na viwili[1] na hotuba kumi[2]. Aliandika pia nyaraka nyingi za kichungaji.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu na babu wa Kanisa.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 25 Oktoba[3].

Tazama pia

Tanbihi

  1. 1.0 1.1 CATHOLIC ENCYCLOPEDIA: St. Gaudentius
  2. http://saints.sqpn.com/saintg25.htm Archived 20 Aprili 2008 at the Wayback Machine. Patron Saints Index: Saint Gaudentius
  3. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.