Eusebius wa Vercelli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Eusebi wa Vercelli)
Bikira Maria katika utukufu pamoja na Malaika Gabrieli, na watakatifu Eusebius wa Vercelli (ameketi), Sebastiano na Roko katika mchoro wa Sebastiano Ricci.
Sehemu ya Codex Vercellensis, inayodhaniwa kuwa iliandikwa na Eusebius mwaka 370.

Eusebius wa Vercelli (kisiwa cha Sardinia, 2 Machi 283 hivi – Vercelli, Piemonte, 1 Agosti 371) alikuwa askofu wa Kanisa Katoliki katika karne ya 4, wa kwanza katika mji huo wa Italia Kaskazini.

Alikusanya mapadri wa jimbo lake kuishi kimonaki na kuimarisha Ukristo katika eneo lote karibu na milima ya Alpi.

Pamoja na Atanasi wa Aleksandria alitetea imani katika umungu wa Yesu dhidi ya Waario na kwa ajili hiyo aliteswa na kupelekwa na kaisari Konstans uhamishoni Palestina, Kapadokia na hadi jangwa la Misri.

Miaka 8 baadaye aliweza kurudi jimboni mwake akaendelea na umisionari wake pamoja na kuimarisha waumini katika imani sahihi [1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 2 Agosti[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Maandishi yake[hariri | hariri chanzo]

  • Toleo jipya la maandishi yake linapatikana katika gombo la 9 la Corpus Christianorum - Series Latina.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • N. Everett, "Narrating the Life of Eusebius of Vercelli", in R. Balzaretti and E.M. Tyler (eds), Narrative and History in the Early Medieval West (Turnhout, 2006: Brepols), pp. 133–165.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.