Msinduzi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Croton talaeporos)
Msinduzi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Malpighiales (Mimea kama mwenda-usiku)
Familia: Euphorbiaceae (Mimea iliyo mnasaba na mtongotongo)
Nusufamilia: Crotonoideae
Burmeist.
Jenasi: Croton
L.
Spishi: C. talaeporos
Radcl.-Sm.

Msinduzi (Croton talaeporos) ni mti wa nusufamilia Crotonoideae katika familia Euphorbiaceae. Unatokea pwani ya Kenya na Somalia ya Kusini katika misitu wazi na nyika yenye miti au vichaka.

Maelezo[1][hariri | hariri chanzo]

Spishi hii ni kichaka au mti mdogo wa urefu wa m 2-10. Gome lake ni kijivu na lina nyufa. Majani yana umbo la yai pana, msingi mviringo au wa umbo la moyo, ncha kali au butu, ukingo wenye meno ya mviringo, sm 4-16 kwa 3-15, yenye nywele chache lakini baadaye bila nywele. Maua ni meupe au njano iliyofifia yenye urefu wa mm 2-3, yenye jinsia moja au mbili, katika vishada vya urefu wa sm 8-20 (yote ya kiume au ya jinsia zilizochanganywa). Matunda mekundu au kahawia, karibu umbo la donge au ndewe tatu, mm 20-28 kwa 22-25 mm, yenye nywele.

Matumizi[hariri | hariri chanzo]

Mizizi hutumika kama dawa ya mafua na ya malalamiko ya tumbo.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Beentje, H.J. (1994) Kenya trees, shrubs and lianas. National Museums of Kenya, Nairobi.