Kabichi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Brassica oleracea)
Kabichi
Aina ya kabichi
Aina ya kabichi
Kilimo cha kabichi
Kilimo cha kabichi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Brassicales (Mimea kama kabichi)
Familia: Brassicaceae (Mimea iliyo na mnasaba na kabichi)
Jenasi: Brassica
L.
Spishi: B. oleracea
(L.)
Ngazi za chini

Makundi ya kaltivari 8:

Kabichi (pia kabeji kutoka Kiingereza "cabbage") ni mboga yenye umbo la mviringo mkubwa na rangi ya kijani, nyekundu (zambarau), au nyeupe inayopandwa kwa msimu.

Kabichi inaweza kuliwa baada ya kupikwa au ikiwa mbichi na ina manufaa mengi kwa afya. Kabichi ina thamani ya juu upande wxa lishe.

Kichwa cha kabichi kwa ujumla huwa na kilo 0.5 hadi 4, na inaweza kuwa kijani, zambarau au nyeupe. Hadi mwaka 2012, kabichi nzito zaidi ilikuwa na kilo 62.71.

Kabichi inayoliwa na binadamu asili yake ni kabichi mwitu. Kabichi ilianza kupandwa huko Ulaya kabla ya mwaka 1000 KK. Katika enzi za zama za Kati, kabichi ilikuwa sehemu kubwa ya vyakula vya Ulaya.

Kwa kawaida, vichwa vya kabichi huvunwa mwaka wa kwanza wa mzunguko wa maisha ya mmea huo, lakini mimea inayotengwa kwa ajili ya mbegu inaruhusiwa kukua mwaka wa pili.

Kabichi huathiriwa na upungufu wa virutubisho kadhaa, pamoja na kuliwa na wadudu wengi, na kupatwa na magonjwa ya bakteria na ya vimelea.

Viungo vya njə[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mmea fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kabichi kama uainishaji wake wa kibiolojia, uenezi au matumizi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.