Ansberto wa Rouen

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Ansberto katika dirisha la kioo cha rangi katika kanisa kuu la Rouen.

Ansberto wa Rouen (pia: Auedebati, Autbati, Autbertus; Chaussy-sur-Epte, leo nchini Ufaransa, karne ya 7Hautmont, 695 hivi) alikuwa askofu wa Rouen (Ufaransa) miaka 683 - 690.

Baada ya kushika vyeo vikubwa katika ikulu alijiunga na monasteri chini ya kanuni ya Kolumbani na miaka sita baadaye akawa abati. Hatimaye alifanywa askofu hadi alipoondolewa na Meya wa ikulu akarudia maisha ya monasterini[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 9 Februari.[2]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.