Alfa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alfabeti ya Kigiriki
Herufi za kawaida
Α α Alfa 1 Ν ν Ni 50
Β β Beta 2 Ξ ξ Ksi 60
Γ γ Gamma 3 Ο ο Omikron 70
Δ δ Delta 4 Π π Pi 80
Ε ε Epsilon 5 Ρ ρ Rho 100
Ζ ζ Dzeta 7 Σ σ ς Sigma 200
Η η Eta 8 Τ τ Tau 300
Θ θ Theta 9 Υ υ Ipsilon 400
Ι ι Iota 10 Φ φ Phi 500
Κ κ Kappa 20 Χ χ Khi 600
Λλ Lambda 30 Ψ ψ Psi 700
Μ μ Mi 40 Ω ω Omega 800
Herufi za kihistoria1
Digamma 6 San 90
Stigma 6 Sho 90
Heta 8 Koppa 90
Sampi 900
1 Viungo vya Nje:
Alfabeti_ya_Kigiriki#Viungo_vya_Nje

Alfa (kwa Kiingereza: alpha) ni herufi ya kwanza ya Alfabeti ya Kigiriki. Inaandikwa Α (herufi kubwa ya mwanzo) au α (herufi ndogo ya kawaida).

Katika Ugiriki ya Kale ilihesabiwa pia kama namba "1".

Jinsi ilivyo kawaida na herufi mbalimbali za Kigiriki inatumiwa kama kifupi kwa ajili ya dhana mbalimbali katika hesabu na fisikia. Kundinyota hili limejulikana hasa kama jina la pembe ya kwanza katika pembetatu.

Katika astronomia inatumiwa kuanza hesabu ya nyota katika kundinyota. Kwa mfano nyota yetu jirani katika ulimwengu inaitwa "Alfa Centauri". Imeitwa hivyo kwa sababu inang'aa kushinda nyota zote za kundinyota ya Centaurus. Inayofuata ni "beta Centauri" na kadhalika.

Alfa ikiwa herufi ya kwanza ya alfabeti ya Kigiriki hutumiwa pia kwa kutaja mwanzo. Hivyo ni kinyume cha mwisho au omega. Usemi wa Biblia ya Kikristo hujulikana kuhusu Mungu kuwa ni "Alfa na Omega, mwanzo na mwisho" (Ufunuo wa Yohane 21:6).